BENJAMINKAMINYOGE.BLOGSPOT.COM

Friday, March 11, 2011

EARTH QUACKE JAPAN

Japan yatikiswa na tetemeko na kimbunga na kuharibu mali kadhaa ikiwemo majengo na miundo mbinu mbali mbali.

YUKO WAPI HUYU ?

KUNA UWEZEKANO UNAMFAHAMU MTU HUYU,MI SIMFAHAMU KABISA.

DAVIES MWAPE

Davies Mwape ni moja kati ya wachezaji hatari katika ligi kuu ya msimu huu,ni mshambuliaji mwenye uwezo mkubwa wa kufumania nyavu za adui na mbinu kuwatoka walinzi wa timu pinzani,viongozi wa Yanga mtunzeni mchezaji huyu msije mkamfanyia AMBANI

Thursday, March 10, 2011

LOLIONDO STOP

Mch.Ambilikile Mwasapile akiwawekea dawa baadhi ya watu waliofika kwa ajili ya kupatiwa huduma hiyo,lakini hata hivyo serikali imesimamisha huduma hiyo kwa ajili ya kufanya uchunguzi na usalama wa dawa hiyo

SIMBA YAZIKALIA AZAM NA YANGA

Timu ya Simba ambao ni mabingwa watetezi wa ligi kuu ya Tanzania bara jana walifanikiwa kuongoza ligi kwa kuifunga Ruvu shooting ya Pwani kwa bao 1-0 dakika ya 87 likifungwa na mchezaji Ally Ahmed 'Shiboli' aliyeingia dakika ya 79 kuchukua nafasi ya Mbwana Samata aliyebanwa vilivyo na mabeki wa Ruvu,sasa Simba imefikisha pointi 41 baada kucheza michezo 18,ikifuatiwa na Yanga yenye pointi 39 huku Azam ikiwa na pointi 37 

Tuesday, March 08, 2011

Mchungaji AMBILIKILE MWASAPILE (kulia) akihojiwa na waandishi wa habari waliofika nyumbani kwake,mchungaji huyo amekuwa akitoa dawa kikombe kimoja kwa kila mgonjwa

WATU WAFURIKA KWA MCHUNGAJI

Umati wa watu unaendelea kufurika kwa mchungaji mstaafu mzee Ambilikile Mwasapile wilayani Ngorongoro,watu wamekuwa wakitoka sehemu mbambali kwa ajili ya kufuata tiba ya magonjwa mbalimbali ambayo yamekuwa hayatibiki hospitalini

Monday, March 07, 2011

LIVERPOOL YAWACHINJA MANCHESTER UTD.

LIVERPOOL jana imeweza kuwashikisha adabu Manchester United baada ya kuwafunga mabao 3-1,magoli ya liverpool yaliwekwa kimiani na Dirk Kuyt.

SIMBA NA YANGA NGUVU SAWA

Timu  zenye upinzani wa jadi kwenye soka la bongo Simba na Yanga jana zilitoka sare ya kufungana bao 1-1

Friday, March 04, 2011

CRDB WAFUNGUA TAWI JIPYA MWANJELWA- MBEYA

Waziri wa maji,Profesa Mark Mwandosya (watatu kushoto) akikata utepe kufungua tawi jipya la benki ya CRDB eneo la Mwanjelwa jijini MBEYA,kushoto ni mwenyekiti wa bodi ya benki hiyo bw.Martin Mmari,kulia ni mama Mwandosya,kufunguliwa kwa tawi hilo kutawasaidia wakazi wa jiji la Mbeya ambao walikuwa wakipanga foleni kwenye tawi pekee lililokuwa mjini Mbeya.

Wednesday, March 02, 2011

SOKO LA BIG BROTHER UBUNGO LAVUNJWA

Soko la big brother eneo la ubungo limevunjwa jana usiku ili ujenzi wa stend wa mabasi yaendayo kasi,hapa ni baadhi ya wafanyabiashara wakiangalia mabaki ya vibanda vyao.

GADAFFI ANG'ANG'ANIA MADARAKANI

  • Kiongozi wa Libya Muamar Gadaffi ameendelea kung'ang'ania madaraka,licha ya kuwepo kwa maandamano ya kumtaka kuachia madaraka hayo ya urais ambayo ameshikilia kwa zaidi ya miaka arobaini,amekuwa ahamini kinachotokea kwenye taifa lake kutokana na jinsi utawala wake kutowapa uhuru waandishi wa habari na redio.


WAZIRI MKUU AKIWA NA MABALOZI WA UFARANSA NA UINGEREZA

Waziri mkuu Mh.Mizengo Pinda ( kushoto) akiwa na balozi wa Ufaransa bwana Jacques Champagne De Labriolle na balozi wa Uingereza bibi Dianne Corner wakati wa mkutano wa wataalam wa uchumi leo jijini Dar es salaam.

Tuesday, March 01, 2011