BENJAMINKAMINYOGE.BLOGSPOT.COM

Saturday, October 29, 2011

YANGA YAICHAPA SIMBA 1-0


Mabingwa watetezi wa Tanzania bara leo wameichapa Simba bao 1-0 kwenye mchezo wa ligi kuu uliyofanyika uwanja wa Taifa,Yanga walipata bao hilo dakika ya 72 kupitia kwa mshambuliaji wao wa kimataifa Davies Mwape baada ya walinzi wa Simba kufanya makosa,mchezo huo ulianza kwa kasi na Simba kutawala kipindi cha kwanza,Simba walipoteza nafasi kadhaa kipindi cha kwanza.
Kipindi cha pili Yanga walijipanga na kubadili mchezo na hivyo kuwafanya waibuke na ushindi huo.
Michezo mingine ya ligi hiyo imechezwa huko Mwanza kati ya Toto African na Coastal Union matokeo ni 0-0,huko Dodoma ilikuwa ni kati ya Polisi na Oljoro matokeo ni 0-0,kwa matokeo haya bado hayabadili msimamo wa ligi bado Simba inaongoza ligi ikiwa na alama 27,ikifuatiwa na Yanga yenye alama 24,Azam 21.

Monday, October 24, 2011

MANCHESTER CITY YAWAFANYIA VIBAYA MANCHESTER UNITED NDANI YA OLD TRAFFORD


Timu ya Manchester City leo imevunja mwiko wa Manchester United baada ya kuwaadhibu kwa goli 6-1 kwenye uwanja Old Trafford.
Manchester Utd imekuwa na rekodi ya kutofungwa kwenye uwanja wa nyumbani lakini leo imeweza kutokea tena idadi kubwa ya magoli.

Thursday, October 20, 2011

GADAFFI AFA KISHUJAA

Aliyekuwa rais wa Libya Muamar Gadaffi leo ameuawa na jeshi la waasi lililom
muondoa madarakani baada ya kumshika na kumjeruhi kwenye mji wake alikozaliwa na kupelekea kifo chake.
 Gadaffi tofauti na marais wengine yeye aliendelea kubakia nchini kwake pamoja na sehemu ya nchi kushikiliwa na waasi,aliendelea na kuishi kwenye mji wa Sirte ambako ndiko alikozaliwa.

Tuesday, October 18, 2011

HUU NDIO USAFIRI WA MLOWO-KAMSAMBA WILAYANI MBOZI.


Pamoja na ajali nyingi kugharimu maisha ya watu,lakini bado watu wamekuwa wakijisahau na kuvunja sheria za usalama barabarani kama inavyoonekana hapa gari ya mizigo ikiwa imebeba abiria wengi kupita kiasi na wengine kukaa juu ya mabomba.

Sunday, October 16, 2011

LIVERPOOL YAWATOA ULIMI NJE MANCHESTER UNITED


Timu ya Liverpool ikicheza kwa maelewano jana iliweza kutoka sare na Manchester Utd kwa kufungana bao 1-1 kwenye uwanja Anfield,Liverpool walipata bao dakika ya 67 kupitia kwa Steven Gerrald na Manchester walisawazisha dak.80 kupitia kwa Chicharito.
Liverpool walitawala mchezo huo kwa kiasi kikubwa na kuwafanya walinzi wa Man kuwa na wakati mgumu.

Saturday, October 15, 2011

LIGI DARAJA LA KWANZA,PRISON YAANZA VIBAYA MBEYA


Timu ya Tanzania Prison leo imeanza vibaya baada ya kufungwa bao 1-0 na timu ya Mbeya City Council,bao la Mbeya City limefungwa na Yona Ndabila kwa njia ya penati kipindi cha kwanza,hadi mapumziko Prison walikuwa nyuma kwa bao 1

Tuesday, October 11, 2011

TUWE NA MOYO WA KUJITOLEA DAMU KWA AJILI YA KUWASAIDIA WAGONJWA MAHOSPITALINI

Darling Lyatuu naye akichangia damu siku ya leo chini ya uangalizi wa mtaalamu wa kitengo cha taifa cha damu salama bi.Joyce Yonael Msuya.