BENJAMINKAMINYOGE.BLOGSPOT.COM

Tuesday, January 17, 2012

WAKULIMA HAWA WANAHITAJI MSAADA WA SOKO LA BIDHAA ZAO

 Wakina mama wa kijiji cha Mshewe Mbalizi wilaya ya Mbeya vijijini wakiuza maembe kwa bei ya shilingi 500/= kwenye plastiki,ambayo ni bei isiyoendana na wingi wa bidhaa hiyo,tunawaomba wale wote wenye uwezo wa kujua soko liliko wawasaidie wakulima
 Wakina mama wakiwa na watoto wao wakisubiri wateja wa maembe kijiji hapa kama walivyokutwa na kamera yetu.

Hili ni ambalo wakina mama hawa huuzia biashara zao za matunda

Moja ya matunda yaliyopo mashambani yakisubiriwa kuvunwa matunda yanajulikana kama maparachichi au matakapela pia yanapatikana kwenye kijiji hiki.


Wednesday, January 11, 2012

Dr.WILBORD SLAA AITEKA MBEYA LEO


Dr.Slaa akiwapungia mkono wananchi wakati akiondoka kwenye viwanja vya shule ya msingi Nzovwe  jijini Mbeya


Tuesday, January 10, 2012

MESSI MCHEZAJI BORA WA DUNIA 2012






  Mchezaji wa Barcelona na timu ya taifa ya Argentina Leone Messi amefanikiwa kutwaa tuzo ya mwanasoka bora wa dunia kwa mara ya tatu,Messi ameiwezesha timu yake ya Barcelona kutwaa mataji ya klabu bingwa Ulaya,klabu bingwa ya Dunia na ubingwa wa Hispania,amekuwa akipachika mabao muhimu na kutengeneza magoli kwa pasi zake za uhakika.



Wachezaji wa Barcelona wakishangilia ubingwa wa UEFA champion league.

Monday, January 09, 2012

DON AND YAMAVILLA DUKA LINALOWASAIDIA WAKULIMA KWA KIASI KIKUBWA WILAYANI MBOZI

                      DON AND YAMAVILLA AGRO CHEMICAL

Duka la pembejeo na madawa ya kilimo lililopo mji mdogo wa Mlowo,linalojulikana kama DON & YAMAVILLA AGRO CHEMICAL limekuwa ni msaada mkubwa kwa wakulima wa eneo hilo na vijiji vya jirani,kutokana na kuuza mbolea,madawa ya kilimo na kutoa ushauri juu ya matumizi ya madawa kwenye mimea.

Baadhi ya madawa yaliyoko kwenye duka hilo ambalo linamilikiwa na Dominick Mwamwezi,ambaye amesema duka hilo linatoa huduma nyingi kwa wateja ikiwemo huduma ya M-Pesa  na Tigo pesa kwa ajili ya kuwasaidia wateja wake.


Thursday, January 05, 2012

SUDAN KUSINI YATANGAZA JONGLEI YAKUMBWA NA MAAFA YA KIBINADAMU

 Baraza la mawaziri Sudan kusini limetangaza janga hilo katika mkutano maalum ambapo kundi la wapiganaji 6000 la kabila Luo nuer lilishambulia baadhi ya miji ikiwemo Lukangol na Pibor wiki iliyopita,na kuchoma mahema na kusababisha maelfu kukimbia maeneo hayo
Naibu katibu mkuu wa umoja wa mataifa anayeshughulikia masuala ya kibinadamu bi.Valerie Amos katika mkutano na waziri wa masuala ya kijamii  wa Sudan Amira Al Fadel Mohammed huko Khartoum.