BENJAMINKAMINYOGE.BLOGSPOT.COM

Sunday, April 29, 2012

SIMBA YAWATUMIA SALAMU YANGA.


Timu ya Simba ya Dar es salaam,kwa mara nyingine imeendeleza ubabe wake baada ya kuwachapa El-Ahly ya Sudan kwa mabao 3-0,kwenye mchezo wa kombe la shirikisho,uliochezwa uwanja wa taifa jijini Dar es salaam.
Simba walipata mabao yao kupitia kwa Haruna Moshi dk.67,Patrick Mafisango dk.77 na Emanuel Okwi dk.84,kwa matokeo hayo yanaipa Simba asilimia kubwa ya kuingia robo fainali ya michuano hiyo na El-Ahly kuwa na deni la bao 4-0 kwenye mchezo wa marudiano utakaochezwa Sudan kati ya mei 11 au 12,baada ya kuvaana na watani wao wa jadi Yanga ambao wanaonekana kupoteana mchezo huo utachezwa mei 5 kuhitimisha ligi kuu ya Tanzania bara.

SIMBA YAWATUMIA SALAMU YANGA.


Timu ya Simba ya Dar es salaam,kwa mara nyingine imeendeleza ubabe wake baada ya kuwachapa El-Ahly ya Sudan kwa mabao 3-0,kwenye mchezo wa kombe la shirikisho,uliochezwa uwanja wa taifa jijini Dar es salaam.
Simba walipata mabao yao kupitia kwa Haruna Moshi dk.67,Patrick Mafisango dk.77 na Emanuel Okwi dk.84,kwa matokeo hayo yanaipa Simba asilimia kubwa ya kuingia robo fainali ya michuano hiyo na El-Ahly kuwa na deni la bao 4-0 kwenye mchezo wa marudiano utakaochezwa Sudan kati ya mei 11 au 12,baada ya kuvaana na watani wao wa jadi Yanga ambao wanaonekana kupoteana mchezo huo utachezwa mei 5 kuhitimisha ligi kuu ya Tanzania bara.

MLIPUKO WATOKEA KANISANI NAIROBI


Waumini wa kanisa la God's House of Miracle leo asubuhi wamekumbwa na dhahama baada ya mlipuko kutokea kanisani wakati wa ibada na kuuwa mtu mmoja na wengine zaidi ya saba kujeruhiwa.
Kanisa hilo lipo maeneo ya mtaa wa Ngara,jijini Nairobi,mlipuko huo unasadikiwa ni wa guruneti ambalo bado halijajulikana limetegwa na nani?

MLIPUKO WATOKEA KANISANI NAIROBI


Waumini wa kanisa la God's House of Miracle leo asubuhi wamekumbwa na dhahama baada ya mlipuko kutokea kanisani wakati wa ibada na kuuwa mtu mmoja na wengine zaidi ya saba kujeruhiwa.
Kanisa hilo lipo maeneo ya mtaa wa Ngara,jijini Nairobi,mlipuko huo unasadikiwa ni wa guruneti ambalo bado halijajulikana limetegwa na nani?

Wednesday, April 25, 2012

CHELSEA YATINGA FAINALI KWA MGONGO WA BARCELONA.


Timu ya Chelsea imeingia fainali ya klabu bingwa ulaya baada ya kufungana FC Barcelona 2-2 kwenye uwanja wa Nou Camp kwenye mchezo wa nusu fainali.
Chelsea imefanikiwa kuingia fainali kwa jumla ya mabao 3-1,wiki mbili zilizopita ilipata ushindi wa goli 1-0 jijini London kwenye uwanja wa Stamford Bridge.
Magoli ya Barca yalifungwa na Sergio na Iniesta na Chelsea walisawazisha kupitia Lamires na Tores.

ZAO LA PARETO HATARINI KUTOWEKA


Zao la pareto ni miongoni mwa mazao ambayo wakulima wamekuwa wakiacha na kupunguza kuyalima,huenda ni kutokana na bei yake kuwa chini au soko kusumbua.
Kamera yetu ilipita maeneo ya wilaya ya Makete,kata ya Matamba na kuona zao hilo likiwa kwenye shamba la ekari moja ndani ya kijiji kizima huku kukiwa na mazao kama mahindi,ngano,maharage na alzeti kwa wingi.

Tuesday, April 24, 2012

UPONDAJI WA KOKOTO WAZIDI KUONGEZEKA MBEYA.


Kutokana na ugumu wa maisha,vijana wengi wamekuwa wakijishughulisha na kazi mbalimbali jijini Mbeya,ikiwemo kuponda kokoto pembezoni mwa barabara kuu,kamera yetu ilipita maeneo ya Ilomba jijini Mbeya na kukuta wajasiliamali wakiponda kokoto na kuuza kwa kipimo cha debe kwa sh.1500/= bila kujali jua kali lililokuwa likiwaka na kuwa kandokando ya barabara jirani na kituo cha mafuta.
Tunawaomba viongozi na taasisi mbalimbali kuweza kuwasaidia wajasiliamali hawa kuwaboreshea mazingira yao ya kazi kwa kutoa mikopo au kuwapatia vifaa vya kujikinga wanapofanya kazi zao.

Wednesday, April 18, 2012

SIMBA BINGWA KWA 92%


Timu ya Simba ya Dar es salaam leo imejiwekea mazingira mazuri ya kutwaa ubingwa wa Tanzania bara baada ya kuwafunga JKT ruvu jumla ya mabao 3-0 kwenye uwanja wa Taifa.
Mabingwa watetezi timu ya Yanga imepoteza dira baada ya kupokea kichapo cha bao 1-0 kutoka kwa Kagera Sugar,tunaweza kusema Yanga imevuliwa ubingwa kwani hata wakishinda mechi zao zilizobaki watafikisha pointi 52 ambazo Simba wameshavuka kwa sasa wana pointi 56 ambazo Yanga hawawezi kuzifikia.

MKUU WA WILAYA AFUNGUA KONGOMANO LA MADEREVA MBEYA.


Mkuu wa wilaya ya Mbeya,ndg Evance Balama akiongea na baadhi ya madereva wa mjini Mbeya kwenye ukumbi wa JM Hotel.
Bwana Balama aliwaasa madereva hao kujiendeleza kielimu na kuzingatia sheria za usalama barabarani.

MARCIO MAXIMO AKUTANA NA MHESHIMIWA RAIS NCHINI BRAZIL

m

Aliyekuwa kocha mkuu wa Taifa stars mbrazil Marcio Maximo alikutana na mheshimiwa rais Jakaya Kikwete jijini Sao Paulo na kusalimiana naye,kabla ya kuongea na waandishi wa habari ambao walikuwa wakimuuliza kuhusu mpango wake wa kuja nchini tena kwa ajili ya kuifundisha Yanga au Azam lakini hata hivyo alikanusha uvumi huo.

Monday, April 16, 2012

MWENYEKITI WA VIJANA CCM MKOA WA ARUSHA AHAMIA CHADEMA

Mwenyekiti wa vijana wa CCM mkoa wa Arusha ameamua kujitoa kwenye chama hicho na kujiunga na Chadema,hii ni ishara ambayo si nzuri kwa chama cha mapinduzi baada ya vijana wengi kuanza kujiingiza kwenye siasa na kujiunga na kambi ya upinzani.

Sunday, April 08, 2012

TUNAWATAKIA PASAKA NJEMA.


Kwa niaba ya mtandao huu,tunawatakia wakristo na wananchi wote sikukuu njema ya Pasaka,tukiwakumbusha kutenda yaliyo mema siku zote za maisha za maisha yetu.

Saturday, April 07, 2012

STEVEN KANUMBA AFARIKI DUNIA.


Kanumba enzi za uhai wake
Msanii na mwigizaji maarufu nchini Steven Kanumba amefariki dunia usiku wa kuamkia leo.
Kifo cha Kanumba kimewashitua watu wengi nchini na nchi jirani

SIMBA HAO 16 BORA KOMBE LA SHIRIKISHO


Timu ya Simba ya Dar es salaam jana ilifanikiwa kusonga mbele kwenye michuano ya kombe la shirikisho licha ya kufungwa bao 3-1 na Es Satif kwenye uwanja wa May 8 mjini Satif-Algeria.
Simba wakicheza pungufu baada ya mlinzi wake kucheza faulo ya kizembe na kutolewa kwa kadi nyekundu dk.8,walibanwa sana wapinzani wao na kujipatia magoli hayo matatu.
Simba walitulia dak 7 za mwisho na kuweza kupata goli dk.92 likiwekwa kimiani na Emanuel Okwi na kuwafanya Simba kusonga mbele kwa faida ya goli la ugenini,wiki mbili zilizopita Simba walishinda 2-0 jijini Dar es salaam.

Friday, April 06, 2012

RAIS WA MALAWI BINGU WA MUTHARIKA AFARIKA DUNIA.


Rais wa Malawi BINGU WA MUTHARIKA amefariki dunia leo hii nchini alikopelekwa kwa ajili ya matibabu baada ya kupata mshituko wa moyo akiwa ofisini kwake hapo jana.
Rais Bingu wa Mutharika alizaliwa 24/02/1934 na alionyesha nia ya kuwa kiongozi toka mwanzoni mwa miaka ya 1990 na hatimaye ndoto yake ilitimia na kuwa rais wa nchi hiyo kupitia uchaguzi uliopita.
Habari hizi ni kwa hisani ya Nyasa Times.

Thursday, April 05, 2012

MHESHIMIWA LEMA AVULIWA UBUNGE ARUSHA MJINI NA MAHAKAMA

Mbunge wa Arusha mjini Godbless Lema amevuliwa ubunge wa jimbo la Arusha mjini baada kushindwa kesi iliyokuwa inamkabili toka alipotangazwa kuwa mbunge wa jimbo hilo.
  Kesi hiyo ilikuwa ni ya kupinga matokeo ambayo ilifunguliwa na wapinzani wake kwenye uchaguzi uliofanyika mwaka 2010.

Wednesday, April 04, 2012

TFF YAWASHIKA YANGA PABAYA


Yanga sasa inaonekana kuchanganyikiwa baada ya kupokwa ushindi dhidi ya Coastal Union baada ya kumchezesha beki wake Nadir Haroub 'Canavaro' ambaye alikuwa ana kadi nyekundu aliyopata baada ya vurugu kwenye mchezo dhidi ya Azam na kusababisha baadhi ya wachezaji wa Yanga kufungiwa kabla ya adhabu hizo kusimamishwa na Tibaigana.

Monday, April 02, 2012

JOSHUA NASSARI MBUNGE MPYA ARUMERU KUPITIA CHADEMA.


Joshua Nassari ameibuka mshindi katika uchaguzi mdogo wa ubunge jimbo la Arumeru baada kumbwaga mpinzani wake wa karibu Sioi Sumari kwa zaidi ya kura 5000.
Uchaguzi ulifanyika kufuatia kifo cha aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo mh.Jeremiah Sumari wa CCM,uchaguzi huo umefanyika jana licha ya kukumbwa na matukio madogodogo ya wanachama kulinda kura na vituo vya kuhesabia kura hizo.
Baadhi ya watu wako mitaani wakishangilia ushindi huo.