BENJAMINKAMINYOGE.BLOGSPOT.COM

Wednesday, June 27, 2012

WAHAMIAJI HARAMU 42 WAFARIKI.


Zaidi ya watu 40 wamefariki kwa kukosa hewa wakiwa ndani ya lori lililokuwa likiwasafirisha,marehemu hao inasemekana ni raia wa Ethiopia waliokuwa wakielekea Malawi kinyume na taratibu za uhamiaji,marehemu hao wamegundulika mkoanI Dodoma baada ya kutelekezwa porini na wafanyakazi wa gari husika ambalo mpaka sasa halijajulikana.
Naibu waziri mambo ya ndani mh.Pereira Silima amethibitisha na kusema wengine waliopona tayari wanashikiliwa na jeshi la Polisi nchini.

Thursday, June 14, 2012

SIKU YA WACHANGIA DAMU DUNIANI


Hawa nia baadhi ya wananchi waliojitokeza kuchangia damu siku ya leo ambayo ni siku ya wachangia damu duniani. Nilibahatika kuongea na mmoja kati ya wachangiaji hao na kuniambia kuwa amekuwa akitoa mara kwa mara hata anapokuwa nje ya nchi.
Pia bi. Jaqueline Cypirian na Jamal Abdallah walisema wanafurahia kuchangia damu na kuwataka wananchi wengine kuwa na moyo wa huruma dhidi ya wahitaji wa damu.

Tuesday, June 05, 2012

POSTA YAKABIDHI T-SHIRT KWA AJILI YA WACHANGIA DAMU.


Meneja wa tawi la Posta Mbeya,Bw.Humphrey Julius(kushoto) akimkabidhi moja ya T-shirt kiongozi wa mpango wa Taifa wa Damu salama Ndg.Kundaeli Sariah,hafla hiyo imefanyika leo kwenye ofisi za mpango wa Taifa wa Damu Salama nyanda za juu kusini,jijini Mbeya na kuhudhuriwa na baadhi ya wafanyakazi wa Benki ya posta na damu salama.
Ndg.Sariah ameishukuru Benki ya Posta na kuwataka wananchi kujitokeza kwa wingi kuchangia damu na kuzitaka taasisi nyingine kujitolea vitu mbalimbali kwa ajili ya wachangia damu.
Sherehe za siku ya wachangiaji damu kitaifa itafanyika mjini Moshi na kanda ya nyanda za juu kusini itafanyika mjini Songea tar.14/06/2012,
KILA MCHANGIAJI DAMU NI SHUJAA