BENJAMINKAMINYOGE.BLOGSPOT.COM

Monday, February 13, 2012

ZAMBIA MABINGWA WA AFRIKA 2012


Timu ya taifa ya Zambia(Chipolopolo) imefanikiwa kutwaa kombe la mataifa ya Africa usiku baada ya kuwashinda Ivory Coast kwa mikwaju ya penati 8-7.
Timu hizo zilicheza kwa dakika 120 na matokeo kuwa 0-0 na hivyo kuingia kwenye matuta ambapo kila ilipiga penati 9,Zambia ilikosa moja na Ivory Coast ilipoteza 2.
Shukrani za pekee zimuendee golikipa wa Zambia Kenedy Mwene, ambaye alikuwa nyota wa mchezo kwa dakika zote na kuweza kuokoa penati 1 kutokana na umahiri wake.

Sunday, February 12, 2012

WHITNEY HOUSTON AFARIKI


Mwanamuziki maarufu nchini Marekani amefariki usiku wa jana,mwanadada huyo ambaye alikuwa akihusishwa na utumiaji wa madawa ya kulevya lakini aligeuka na kuanza kupinga utumiaji wa madawa hayo kwa watu wengine.
Mwanadada amekuwa na sifa za uvumilivu kwenye mahusiano yake ya kimapenzi licha ya kupitia mikasa mbalimbali lakini aliweza kuvumilia pamoja na umilionea aliyokuwa nao.

Thursday, February 09, 2012

TIMU YA TAIFA YA ZAMBIA YAINGIA FAINALI MICHUANO YA AFRIKA.


Timu ya taifa ya Zambia (Chipolopolo) imefanikiwa kuingia fainali ya michuano ya mataifa ya Afrika, baada ya kuwafunga Ghana(Black Star) kwa bao 1-0,
Zambia walipata bao lao kupitia kwa kupitia kwa Emanuel Mayuka dakika ya 78 na kuwafanya Zambia kuingia fainali,katika mchezo mwingine wa nusu fainali Ivory Coast wameifunga Mali bao 1-0.
Sasa Zambia watakutana na Ivory Coast katika mchezo wa fainali utakaochezwa kesho kutwa na Ghana watawakabili Mali katika kuwania nafasi ya tatu.

Wednesday, February 08, 2012

UCHAFUZI WA MAZINGIRA


Gari ya kubeba taka likiwa limebeba takataka ambazo zinaendelea kuungua na hivyo kusababisha moshi kusambaa barabarani na kuleta athari kwa watu,mbali na hilo pia inaweza kutokea ajali ya moto iwapo taka hizo zikiendelea kupulizwa na upepo.

UCHAFUZI WA MAZINGIRA


Gari ya kubeba taka likiwa limebeba takataka ambazo zinaendelea kuungua na hivyo kusababisha moshi kusambaa barabarani na kuleta athari kwa watu,mbali na hilo pia inaweza kutokea ajali ya moto iwapo taka hizo zikiendelea kupulizwa na upepo.

UCHAFUZI WA MAZINGIRA


Gari ya kubeba taka likiwa limebeba takataka ambazo zinaendelea kuungua na hivyo kusababisha moshi kusambaa barabarani na kuleta athari kwa watu,mbali na hilo pia inaweza kutokea ajali ya moto iwapo taka hizo zikiendelea kupulizwa na upepo.

UCHAFUZI WA MAZINGIRA


Gari ya kubeba taka likiwa limebeba takataka ambazo zinaendelea kuungua na hivyo kusababisha moshi kusambaa barabarani na kuleta athari kwa watu,mbali na hilo pia inaweza kutokea ajali ya moto iwapo taka hizo zikiendelea kupulizwa na upepo.

Wednesday, February 01, 2012

MVUA NI NEEMA TATIZO SISI


Kutokana ni miundo mbinu mibovu mvua imekuwa kama kero kwa wakazi wa Soweto jijini Mbeya,wamekuwa wakipata taabu kwenye maeneo ya barabara zinazoingia na kutoka mitaa hiyo kutokana na maji kujaa na kuhathiri mpaka maeneo ya biashara.kama inavyoonekana kwenye picha.

MTI HUU UNAWEZA UKASABABISHA AJALI.


Mti huu matawi yake yameingia barabarani na kusababisha mtu unayetembea kwa miguu usiweze kuliona gari linalokuja mbele au nyuma kutokana na matawi yaliyozidi na kuingia mpaka barabarani kwenye barabara ya Uhindini kuelekea Soko matola jijini Mbeya,wahusika inabidi walishughulikie suala hili mapema kabla madhara hayajatokea.

JIJI LETU MBEYA LEO


Picha hii ni moja ya mitaa ya jiji la Mbeya.