BENJAMINKAMINYOGE.BLOGSPOT.COM

Sunday, August 26, 2012

SENSA YAENDELEA NCHINI KWA UTULIVU MKUBWA


Mheshimiwa Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na familia yake wakishiriki zoezi la kuhesabiwa na kujibu maswali ya makarani wa sensa kwa utulivu mkubwa.
Wewe mwananchi ambaye bado hujafikiwa na makarani wa Sensa fuatilia kwa Mwenyekiti wako wa mtaa ili uhakikishe unahesabiwa kwa ajili ya maendeleo ya taifa letu,kuhesabiwa kwako ndio kunalifanya taifa lielewe idadi ya watu na kupanga maendeleo na huduma za kijamii kwa eneo husika-JITOKEZE KUHESABIWA KWA MAENDELEO YETU YA BAADAYE.

Friday, August 24, 2012

YANGA NDANI YA IKULU YA RUANDA


Rais Paul Kagame akiongea na wachezaji na viongozi wa timu ya Yanga ambao ni mabingwa wa Afrika mashariki na kati walipomtembelea Ikulu ya Ruanda,jijini Kigali jana.
Pia timu hiy6 imetembelea makaburi ya watu waliouawa mwaka 1994 kwenye mauaji ya Kimbari nchini humo,mbali na hayo timu hiyo imekuwa kivutio kikubwa kwa wapenzi wa soka wa nchini humo.

Tuesday, August 21, 2012

WAZIRI MKUU WA ETHIOPIA MELES ZENAWI AMERIKI.


Waziri mkuu wa Ethiopia Meles Zenawi amefariki dunia jana usiku nchini Belgium alikokuwa akipatiwa matibabu.
Bwana Zenawi aliingia madarakani mwaka 1991 baada ya mapinduzi yaliyomuondoa madarakani Mengistu Hailemariam na kusababisha nchi hiyo kuingia kwenye mapigano ya kikabila na majirani zao Eriteria na baadaye akaweza kuleta amani nchini humo mpaka kifo chake hofu imetanda imetanda miongoni mwa wananchi kuwa huenda machafuko ya kikabila yakazuka tena baada ya kifo chake.
Makamu waziri mkuu wa nchi hiyo bw.Hailemariam Deselagan ndio ataongoza nchi hiyo mpaka wakati wa uchaguzi mwaka 2015.

Sunday, August 19, 2012

RAIS J.M.KIKWETE ASWALI SWALA YA IDD KINONDONI MUSLIM


Mstahiki Meya wa manispaa ya Kinondoni Yusuph Mwenda akimpokea Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya muungano Dr.Jakaya Mrisho Kikwete alipofika kwenye viwanja vya Msikiti wa Kinondoni Muslim kwa ajili ya swala ya Idd-el-fitr leo.

RAIS J.M.KIKWETE ASWALI SWALA YA IDD KINONDONI MUSLIM


Mstahiki Meya wa manispaa ya Kinondoni Yusuph Mwenda akimpokea Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya muungano Dr.Jakaya Mrisho Kikwete alipofika kwenye viwanja vya Msikiti wa Kinondoni Muslim kwa ajili ya swala ya Idd-el-fitr leo.

MAKAMU WA RAIS ASWALI SALA YA IDD-EL-FITR MNAZI MMOJA.


Makamu wa Rais Dr.Mohammed Gharib Bilal leo ameswali sala ya Idd kwenye viwanja vya Mnazi mmoja,jijini Dar es salaam,swala hiyo imehudhuriwa na watu wengi akiwemo Rais mstaafu Alhaji Ally Hassan Mwinyi.

EID MUBARAK


MTANDAO HUU UNAWATAKIA KHERI NA FANAKA YA SIKUKUU YA EID-EL-FITR WATANZANIA NA WAISLAMU WOTE DUNIANI,TUDUMISHE AMANI NA UPENDO-SIKUKUU NJEMA.

SIMBA B YANYAKUA UBINGWA WA ABC SUPER 8 KWA KUWACHAPA MTIBWA 4-3.


Timu ya Simba B leo imetwaa ubingwa wa Super 8 cup baada ya kuwafunga Mtibwa goli 4-3 kwenye uwanja wa Taifa,Dar es salaam.
Timu ya Simba B ambayo inaonyesha kandanda safi iliingia fainali kwa kuwatoa Azam FC kwa goli 2-1 na Mtibwa waliwatoa Jamhuri kwa 5-1,kivutio cha mchezo wa leo alikuwa Christopher Edward ambaye alifunga magoli matatu (hat trick) na kuweza kuchangia ushindi huo wa Simba B.
Nao wapenzi wa soka wamefurahishwa na kikosi cha Simba B na kuomba timu nyingine kuiga mfano huo,wengine wamedai kikosi hicho ni zaidi ya timu yao ya wakubwa na kama wakipambanishwa wanaweza kuwatia aibu kaka zao wa Msimbazi.

SIMBA B YANYAKUA UBINGWA WA ABC SUPER 8 KWA KUWACHAPA MTIBWA 4-3.


Timu ya Simba B leo imetwaa ubingwa wa Super 8 cup baada ya kuwafunga Mtibwa goli 4-3 kwenye uwanja wa Taifa,Dar es salaam.
Timu ya Simba B ambayo inaonyesha kandanda safi iliingia fainali kwa kuwatoa Azam FC kwa goli 2-1 na Mtibwa waliwatoa Jamhuri kwa 5-1,kivutio cha mchezo wa leo alikuwa Christopher Edward ambaye alifunga magoli matatu (hat trick) na kuweza kuchangia ushindi huo wa Simba B.
Nao wapenzi wa soka wamefurahishwa na kikosi cha Simba B na kuomba timu nyingine kuiga mfano huo,wengine wamedai kikosi hicho ni zaidi ya timu yao ya wakubwa na kama wakipambanishwa wanaweza kuwatia aibu kaka zao wa Msimbazi.

Wednesday, August 15, 2012

TAIFA STARS NGUVU SAWA NA BOTSWANA 3-3.


Timu ya Taifa stars leo imetoka sare na timu ya taifa ya Botswana baada ya kufungana bao 3-3 kwenye mchezo wa kirafiki uliochezwa jijini Gaborone.
Magoli ya Taifa Stars yamefungwa na Erasto Nyoni,Mwinyi Kazimoto na Mrisho Ngassa.

PATRICE MUAMBA AJIUZULU SOKA


Mchezaji wa Bolton ya Uingereza ametangaza kujiuzulu soka kutokana na ushauri wa madaktari waliomfanyia upasuaji mdogo wa moyo nchini Belgium.
Muamba ametangaza uamuzi huo leo hii na kusema kwa sasa anaangalia afya yake na pia amewashukuru madaktari wote waliohangaikia uhai wake kwa muda ambao ulikuwa ni mgumu kwake baada ya kupoteza fahamu kwa muda mrefu.

SIMBA B YAILAZA AZAM FC NA KUTINGA FAINALI YA SUPER8 ABC.


Timu ya Simba B imeweza kuwaduwaza Azam leo kwa kuwafunga bao 2-1 kwenye mchezo wa nusu fainali uliofanyika uwanja wa Taifa.
Azam wakiwa na baadhi ya wachezaji wakongwe walishindwa kulimudu gwaride la watoto hao na kuambulia vumbi,magoli ya Simba yamefungwa na Rashid Idrisa na Christopher Edward wakati la Azam likifungwa na Zahor Pazi
Mechi nyingine ya nusu fainali ilipigwa saa nane mchana kati ya Mtibwa Sugar na Jamhuri ya Zanzibar,Mtibwa wamepata ushindi wa bao 5-1 dhidi ya Jamhuri,kwa maana hiyo Mtibwa watacheza na Simba fainali Jumamosi.

Tuesday, August 14, 2012

MABAKI YA HELKOPTA ZA UGANDA YAPATIKANA MLIMA KENYA


Mabaki ya helkopta mbili za Uganda yamepatikana mlima Kenya,helkopta hizo ziliondoka nchini Uganda jumapili zikiwa zinaelekea nchini Somalia kuongeza nguvu kwenye jeshi la kulinda amani la Afrika.
Mpaka sasa chanzo cha ajali hiyo hakijajulikana.

MABAKI YA HELKOPTA ZA UGANDA YAPATIKANA MLIMA KENYA


Mabaki ya helkopta mbili za Uganda yamepatikana mlima Kenya,helkopta hizo ziliondoka nchini Uganda jumapili zikiwa zinaelekea nchini Somalia kuongeza nguvu kwenye jeshi la kulinda amani la Afrika.
Mpaka sasa chanzo cha ajali hiyo hakijajulikana.

Monday, August 13, 2012

TETEMEKO IRAN LAHARIBU VIJIJI 12.


Nchi ya Iran imekumbwa na tetemeko la ardhi lenye ukubwa wa 6.4 na 6.5 na kusababisha uharibifu wa vijiji 12 na kusababisha vifo vya zaidi ya watu 250 na wengine wakiwa wamefukiwa na vifusi,jitihada za kuwatafuta watu waliofukiwa na vifusi zinaendelea.

Sunday, August 05, 2012

ANDY MURRAY AMSHINDA ROGER FEDERAR NA KUTWAA DHAHABU


Mcheza tenisi wa Uingereza Andy Murray amefanikiwa kutwaa medali ya dhahabu kwenye michezo ya Olmpiki inayoendelea nchini Uingereza baada ya kumchapa mchezaji maarufu duniani Roger Federar kwa seti 6-1,6-0,6-4 kwenye uwanja wa Wimbledon.
Naye Serena Williams amemfunga Maria Sharapova kwa seti 6-0,6-2 na kujinyakulia medali ya Dhahabu,michezo ya leo imewakutanisha magwiji wa Tenisi duniani,furaha zaidi ni Andy Murray ambaye amekuwa na kiu ya kumufunga Federar kwa muda mrefu na hatimaye amefanikiwa