BENJAMINKAMINYOGE.BLOGSPOT.COM

Wednesday, September 19, 2012

MTIBWA YAICHAKAZA YANGA 3-0


Timu ya Mtibwa Sugar FC leo wamewafunga Mabingwa wa Afrika mashariki na kati Yanga kwa bao 3-0 kwenye mchezo wa ligi kuu ya Vodacom.
Yanga ikiwa imesheheni wachezaji wake nyota,walishindwa kuwadhibiti Mtibwa ambao safu ya kiungo ilionekana kucheza vizuri chini ya Shabaan Kisiga na Shaban Nditi.
Matokeo mengine ni kama ifuatavyo:-
Toto African 2-Azam 2
Prison 1-Coastal 1
African Lyon 2-Polisi 1
JKT Oljoro 0-Kagera 0
Simba 2-JKT Ruvu 0
Ruvu Shooting 1-Mgambo 0

Tuesday, September 04, 2012

DAUD MWANGOSI AZIKWA LEO TUKUYU MBEYA.


Katibu mkuu wa taifa wa CHADEMA akiweka shada la maua kwenye kaburi la Daud Mwangosi ambaye alikuwa mwandishi wa kituo cha televisheni Chanel Ten,ambaye aliuawa juzi katika vurugu kati ya polisi na wananchi wanaosadikiwa na wanachama wa Chadema huko Nyololo wilayani Mufindi.
Marehemu Daud Mwangosi amezikwa kijijini kwao Busoka,Tukuyu,watu wengi wamehudhunishwa na kifo hicho na kulitupia lawama jeshi la polisi.

DAUD MWANGOSI AZIKWA LEO TUKUYU MBEYA.


Katibu mkuu wa taifa wa CHADEMA akiweka shada la maua kwenye kaburi la Daud Mwangosi ambaye alikuwa mwandishi wa kituo cha televisheni Chanel Ten,ambaye aliuawa juzi katika vurugu kati ya polisi na wananchi wanaosadikiwa na wanachama wa Chadema huko Nyololo wilayani Mufindi.
Marehemu Daud Mwangosi amezikwa kijijini kwao Busoka,Tukuyu,watu wengi wamehudhunishwa na kifo hicho na kulitupia lawama jeshi la polisi.

Sunday, September 02, 2012

MENAS ZENAWI AZIKWA LEO


Waziri Mkuu wa Ethiopia Menas Zenawi amezikwa leo jijini Addis Ababa.
Mazishi hayo yamehudhuriwa na viongozi mbalimbali kutoka nje ya Ethiopia,mmoja wa viongozi hao Rais Paul Kagame wa Ruanda alimuelezea marehemu kuwa katika uongozi wake alileta maendeleo nchini humo na bara la Afrika kwa ujumla.

MJASILIAMALI WA KATAVI


Pamoja na kuwepo kwa ushindani wa soko za bidhaa zetu kwenye masoko ya nje,bado Tanzania tuna nafasi ya kuibua vipaji vilivyo vijijini na kuviendeleza,kamera yetu ilimkuta fundi huyu wa vinu(pichani) akitengeneza vinu vidogo kwa kutumia nyenzo duni.
Bidhaa kama hizi zimekuwa zikitumika majumbani na baadhi ya watalii wakinunua kama mapambo au ukumbusho wao kutembelea Afrika,inatakiwa mipango mizuri ya kuwawekea wabunifu wetu misingi mizuri ili kuwafanya wasonge mbele

YANGA YAICHAPA COASTAL UNION 2-1


Mabingwa wa Afrika mashariki na kati Yanga ya Dar es salaam jana wameweza kuwafunga Coastal union ya Tanga 2-1 kwenye mchezo wa kirafiki uliochezwa uwanja wa taifa.
Coastal walipata goli lao dakika ya 16 likifungwa na Razak Khalfan goli hilo lilidumu hadi dakika ya 84 pale beki wa Coastal Phil Kaira alipojifunga,bao la pili lilifungwa na Said Bahanuzi dakika ya 86.
Yanga iliwachezesha wachezaji wake wapya akiwemo Twite.

MBUYU TWITE APATA MAPOKEZI MAKUBWA.


Mchezaji wa Yanga raia wa DRC ameingia Nchini kwa mapokezi makubwa kutoka kwa mashabiki wa klabu hiyo,ambao walikuwa wakimsubiri kwa muda mrefu.
Mashabiki hao walimpatia jezi namba 4 yenye jina la Rage ambaye ni mwenyekiti wa Simba kama kumdhihaki Rage ambaye alimsajili mchezaji huyo na baadaye mchezaji huyo kurudisha fedha na kusajili Yanga kwa kitita kikubwa zaidi.
Pamoja na mapokezi makubwa aliyopata mchezaji huyo,wadau wa soka wamemtaka kufanya kile kilichomleta mashabiki huwa hawachelewi kubadilika katika mchezo wa soka na kumuona si chochote.