BENJAMINKAMINYOGE.BLOGSPOT.COM

Saturday, October 13, 2012

MTOTO AZUA BALAA MBAGALA KWA KUKOJOLEA QU-RAAN


Mtoto wa kidato cha kwanza amezua balaa na kusababisha kuvunjika kwa amani kwa muda eneo la Mbagala-Kizuiani, kutokana na kitendo cha kukojolea Qu-raan wakati alipokutana na mtoto mwenzie ambaye alikuwa na kitabu hicho na kuanza ubishi uliopelekea mtoto kufanya kitendo hicho ambacho kimetokana na utoto na kusababisha watu wazima kupandwa na jazba na kuanzisha maandamano yaliyopelekea uharibifu wa vitu mbalimbali yakiwemo makanisa na magari.