BENJAMINKAMINYOGE.BLOGSPOT.COM

Saturday, April 27, 2013

BARCELONA NA REAL MADRID UGONJWA MMOJA WAPIGWA NNE NNE NA WAJERUMANI.


Real Madrid chini ya special coacher Jose Maurinho jana imepata kipigo kikubwa kutoka kwa Borussia Dortmund cha goli 4-1,kwenye nusu fainali ya klabu bingwa Ulaya.
Magoli ya Dortmund yote yamefungwa na Robert Lewandoski huku goli la kufutia machozi la Real Madrid likifungwa na Christian Ronaldo
Nao Barcelona juzi walikutana na kipigo kama hicho cha goli 4-0,kutoka kwa Bayern Munich,mechi za marudiano zitachezwa tarehe 30 na 31/05/2013 nchini Hispania.

Thursday, April 18, 2013

BI.KIDUDE AFARIKI DUNIA


Msanii mkongwe hapa nchini Fatma Baraka (Bi.Kidude) amefariki na atazikwa leo huko kijijini kwao Katumba Unguja.
Bi.Kidude alikuwa ni muimbaji wa nyimbo za taarab na mpiga ngoma maarufu,ambaye alikuwa maarufu ndani na nje ya nchi alikuwa kipenzi cha watu wengi kutokana na uwezo wake wa kulishambulia jukwaa pamoja na umri wake kuwa mkubwa.

Thursday, April 04, 2013

CANAAN HIGH SCHOOL-MLOWO MBOZI.


Ni moja ya shule nzuri zilizopo wilayani Mbozi,shule ipo eneo la Mlowo kilomita 1.2 toka barabara kuu iendayo Tunduma,shule ina walimu wazuri kwa masomo yote na mazingira mazuri kwa wanafunzi.
Pia ina Hosteli kwa ajili ya wavulana na wasichana,inapokea wanafunzi kutoka sehemu mbalimbali,wahi sasa ili hupate nafasi kwenye shule hii yenye ubora mkubwa.