BENJAMINKAMINYOGE.BLOGSPOT.COM

Tuesday, November 11, 2014

ZAMBIA IS HOLDINGS A STATE FUNERAL FOR PRESDENT MICHAEL SATA WHO DIED LAST MOUNTH IN A UK HOSPITAL AT THE AGE OF 77

                               There was a deafening wailing when the coffin come into the stadium
 Tens of thousands of people are attending  the Catholic mass of the National Heroes Stadium in the Capital,Lusaka.
 Regional leaders are amongst those who have come to pay their respects
 Known as "King Cobra" for his venomous tongue,Mr Sata was elected Zambia Presdent in 2011.
 The country is now being run by an acting Presdent,and fresh elections are expected in January 2015

Monday, November 10, 2014

SIMBA YAZINDUKA USINGIZINI YAWACHAPA RUVU SHOOTING 1-0

  Timu ya Simba SC imefanikiwa kupata ushindi wa kwanza kwenye ligi kuu ya Vodacom kwa kuwafunga RUVU SHOOTING goli 1-0 kwenye uwanja wa Taifa,goli hilo pekee limefungwa na Emmanuel Okwi baada golikipa kuutema mpira uliopigwa na Elias Maguri.
  Simba ikiwa imeingia uwanjani kwa mara ya saba ndio ushindi wake wa kwanza baada ya kutoka sare michezo sita mfulululizo na sasa wamefikisha alama tisa,huku Mtibwa Sugar wakiwa wanaongoza ligi kwa alama 15,wakifuatiwa na Azam na Yanga zenye alama 13 kila moja.
Matokeo mengine yalikuwa kama ifuatavyo:-

.Yanga 2-Mgambo 0

.Azam 2-Coastal 1

.Stand UTD 1-Mbeya City 0

.Polisi Moro 1-Prison 0

.Mtibwa 1-Kagera 1

.JKT Ruvu  2-Ndanda 0

Ligi hiyo itaendelea tena D
esemba 26 baada kusimama kwa ajili ya michezo ya Chalenji na Uhai Cup.

Emmanuel Okwi akishangilia goli alilofunga
Kocha Patrick Phiri akimpongeza Okwi kwa kuweza kuipatia timu ushindi
Mashabiki wa Simba wakiwa na furaha ya ajabu baada ya ushindi

Wednesday, October 29, 2014

RAIS WA ZAMBIA MICHAEL SATA AFARIKI JIJINI LONDON

  Kifo chake kimetokea siku chache baada ya Zambia kusherehekea miaka 50 ya uhuru wa nchi hiyo. Mwanasiasa huyo mkongwe aliingia madarakani mwezi Septemba 2011 baada ya kuongoza chama chake cha Patriotic Front, na kumshinda Rupiah Banda, ambaye alikuwa rais wakati huo na chama chake cha Movement for Multi-Party Democracy, kikiwa madarakani kwa miaka ishirini.
 Michael Chilufya Sata alizaliwa mwaka 1937 katika mji wa Mpika, eneo ambalo lilikuwa wakati huo ni Northern Rhodesia. Muumini wa dini ya Kikristo ya madhehebu ya Katoliki, alifanya kazi kama afisa polisi, mfanyakazi wa reli na mwanachama wa chama cha wafanyakazi wakati wa utawala wa kikoloni. Baada ya Zambia kupata uhuru wake, pia aliishi kipindi fulani mjini London, akiwa mfanyakazi wa reli, na kurejea Zambia, akiwa na kampuni ya teksi.
 Akiwa mwenye sauti ya mkwaruzo yakiwa ni matokeo ya kuvuta sigara kwa muda mrefu, Bwana Sata aliibuka katika siasa na kupata umaarufu katika miaka ya 1980. Haraka akapata sifa ya kuwa gavana mwenye kuchapa kazi kwa bidii, wakati akiongoza jimbo la Lusaka na mtu wa utekelezaji kwa vitendo.
 Lakini pia alijulikana kama mtu wa kutoa amri, mtu asiyeendekeza urafiki na mkali na wapinzani wake walisema jina alilopewa la bandia la "King Cobra" alikuwa anastahili kuitwa hivyo. Kwa mara ya kwanza alionekana kama mtu ambaye angetekeleza ahadi za kupambana na rushwa na kupata ufumbuzi wa tatizo la ajira na kuleta ustawi wa jamii. Lakini kipindi chake madarakani kiligubikwa na kuuzima upinzani wa kisiasa na kudorora kwa uchumi. Bwana Sata ni rais wa pili wa Zambia kufariki dunia akiwa madarakani baada ya Levy Mwanawasa.
Rais Michael Sata Enzi za uhai wake

Saturday, October 25, 2014

JKT RUVU YAVUNJA MWIKO WA AZAM,YAWACHAPA 1-0

  Timu ya JKT RUVU leo imefanikiwa kuwachapa mabingwa wa Tanzania bara Azam FC goli 1-0,ambao msimu uliopia walimaliza ligi bila kupoteza mchezo,kwenye uwanja wao wa Chamazi.
  Na huko Shinyanga,wenyeji Stand United wamekula kichapo cha goli 3-0 kutoka kwa Yanga ya Dar es salaam,Stand United waliingia uwanjani kwa kujiamini sana na hivyo kuipa Yanga wakati mgumu na kutoa mipira mingi ya kona ambazo hazikuzaa matunda.
  Yanga walifanikiwa kupata goli la kwanza lililofungwa na Santos Jaja na kwenda mapumziko wakiwa mbele kwa goli hilo.
  Kipindi cha pili Yanga walifanya mabadiliko kwa kuwatoa Jaja,Coutinho na Niyonzima na nafasi zao kuchukuliwa na Hussein Javu,Jerison Tegete na Nizar Khalfan mabadiliko hayo yaliiwezesha Yanga kupata mabao mawili zaidi yakifungwa na Jerison Tegete dakika ya 73 na 87 hadi mwisho wa mchezo Yanga 3-Stand UTD O
  Michezo mingine iliyochezwa leo na matokeo yake:-
.Azam FC 0-JKT Ruvu 1
.Prisons 1-Simba 1
.Kagera Sugar 1-Coastal 1
.Ndanda 0-Mgambo 1
Ruvu shooting 1-Polisi Moro 0
Kesho kutakuwa na mechi moja kati ya Mbeya City na Mtibwa Sugar uwanja wa Sokoine Mbeya.

Kikosi cha Yanga kikiwa tayari kwa mchezo

Wednesday, October 22, 2014

OSCAR PISTORIUS JAILED FOR FIVE YEARS

  Oscar Pistorius will spend his first day behind bars on Tuesday after he was sentenced to five years’ jail for killing his girlfriend, Reeva Steenkamp. Looking distressed, the Paralympian clasped the hands of family members as a police officer led him from the dock down 23 steps – paint peeling off the handrail – to holding cells below the high court in Pretoria, the capital of South Africa. The national prosecuting authority said Pistorius, 27, would go to prison immediately and would be eligible to be considered for parole after serving a third of his sentence. His uncle, Arnold Pistorius, indicated the sprinter would not appeal. The amputee athlete, known as the “Blade Runner”, stood staring straight ahead as judge Thokozile Masipa announced his sentence for culpable homicide. There was a muted reaction from the families on the front bench of the public gallery after a trial that has otherwise provided high emotion and drama. Masipa rejected many of the defence team’s arguments and described the evidence of one of their witnesses, social worker Annette Vergeer, as “slapdash and disappointing”. She said she had no reason to believe that South Africa’s prisons would not be able to cater for the needs of a disabled person such as Pistorius. “It would be a sad day for this country if an impression was created that there is one law for the poor and disadvantaged and another for the rich and famous,” she noted. Masipa said a judge must strive for a sentence “neither too light nor too severe”, ruling that “a non-custodial sentence will send a wrong message to the community”. Referring to the Steenkamp family, the judge said: “Nothing I do or say today can reverse what happened to the deceased or her family on 14 February 2013”, but she hopes her judgment would provide some form of closure. Steenkamp’s father, Barry, said afterwards: “I’m pleased that it’s over.” The Steenkamps’ lawyer, Dup de Bruyn, told Agence France-Presse that the sentence would probably be served as two years in prison and three years under house arrest. “In effect, he gets three years’ correctional supervision and two years’ direct imprisonment.” De Bruyn said Steenkamp’s parents were satisfied with the decision. “They feel it’s right.” Pistorius killed Steenkamp, 29, in the early hours of Valentine’s Day last year when he shot her through the bathroom door at his home in Pretoria. He insisted he thought he was firing at an intruder. Pistorius was also given a three year sentence, suspended for five years, for a firearms offence. Prison’s grim record The Pretoria prison in which Oscar Pistorius will spend at least the next 10 months counts among its more illustrious alumni the South African short-story master Herman Charles Bosman, who was sent there in 1926 after shooting and killing his stepbrother. Like Pistorius, Bosman claimed it was an accident, but Bosman was convicted of murder and only escaped death row after a reprieve. His resulting prison memoir, Cold Stone Jug, was described by Doris Lessing as “the saddest of all prison books”. Today Kgosi Mampuru, previously known as Pretoria Central Prison, but renamed to honour a Bapedi chief hanged there in 1883 after being convicted of murder, public violence and revolt, is home to Clive Derby-Lewis and Janusz Walus, convicted of the 1993 assassination of the ANC leader Chris Hani. Derby-Lewis has twice been attacked by other inmates, most recently in March this year. His lawyer said at the time: “It is safer to go to war than to be in the Kgosi Mampuru prison”. Pistorius may hope his experience is more similar to that of the Waterkloof Two, Frikkie du Preez and Christoph Bekker, who were sent to the prison after being convicted of killing a homeless man in 2001. A video of the two emerged earlier this year that appeared to show them drinking alcohol and using mobile phones and computers in their cell, prompting a public outcry and forcing an investigation by Correctional Services. Inmates at Kgosi Mampuru have already told the South African newspaper The Times that a mobile phone was waiting for Pistorius. One prisoner said they had been following his trial on TV using mobile satellite devices, and that the athlete would be protected by his fame and money.
Oscar Pistorius and Reeva Steenkamp

Monday, October 20, 2014

DALILI ZA UGONJWA WA EBOLA

 Symptoms of Ebola virus infection are similar to those produced by other hemorrhagic fever viruses and include fever, fatigue, malaise, reddened eyes, weakness, joint pain, muscle pain, headache, nausea, vomiting, and diarrhea. Additional Ebola symptoms include a loss of appetite and often stomach pains.

Saturday, October 18, 2014

YANGA NA SIMBA HAKUNA MBABE

  Mchezo namba 27 wa Ligi Kuu ya Vodacom uliowakutanisha watani wa jadi Young Africana kutoka eneo la Jangwani na Simba SC kutoka eneo la msimbazi jijini Dar es salaam umemalizika kwa suluhu ya bila kufungana (0-0), mtanange uliofanyika jioni ya leo kwenye dimba la Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
 Young Africans ilingia uwanjani chini ya kocha wake Marcio Maximo kusaka pointi tatu hali kadhalika Phiri wa Simba akisaka alama tatu pia hali iliyopelekea mchezo huo kuwa mgumu kutikisika kwa nyavu za pande zote mbili. Kocha mbrazil alimtumia mshambuliaji Jaja akisaidiwa na Coutinho, Ngasa, Niyonzima na viungo Mbuyu Twite na Hassan Dilunga huku Phiri akimtumia Maguri kama mshambuliaji kiongozi akisaidiwa na Kiemba, Ndemla, Chanongo na Okwi.
 Young Africans ilifanya mashambuizi kadhaa langoni mwa Simba kupitia kwa washambuliaji wake hali kadhalika wapinzani nao walifanya hivyo pia lakini mashambulizi ya timu zote mbili yalikuta yakiishia mikononi kwa walinda mlango wa timu zote. Mpaka dakika 45 zakipindi cha kwanza zinamalizika, Young Africans 0 - 0 Simba SC. 
 Kipindi cha pili kilianza kwa timu zote kufanya mabadiliko kwa lengo la kusaka bao la mapema katika mchezo wa huo, lakini kutokua makini kwa washambuliaji wa timu zote kulifanya milango kuendelea kuwa migumu kufunguka. Andrey Coutinho alikosa nafasi mbili za kuipatia Young Africans bao baada ya kupokea krosi nzuri ambazo alishindwa kuzitumia vyema kuukwamisha mpira wavuni na kukuta michomo yake ikiokolewa na mlianda mlango wa Simba SC Manyika Peter. Simba ilifanya mashambulizi langoni wa Young Africans kupitia kwa washambuliaji wake Okwi, Maguri na Chanongo lakini jitihada zao hazikuzaa matunda na kukuta mipira yao ikiishia mikononi wa mlinda wa Deo Munish "Dida" na mingine kupaa juu ya lango au kuokolewa na walinzi. Mpaka dakika 90 za mchezo zinamalizika, Young Africans 0 - 0 Simba SC. 
 Young Africans: 1. Dida, 2. Juma Abdul/Telela, 3. Oscar, 4. Cannavaro, 5. Yondani, 6. Twite, 7.Dilunga, 8.Niyonzima/Msuva, 9.Jaja/Kizza, 10.Ngasa, 11. Coutinho 
Kikosi cha Yanga
 
Golikipa wa Simba Peter Manyika Jr. akiokoa moja ya hatari langoni kwake huku washambuliaji wa Yanga wakiwa jirani naye.
Simba SC: 1. Manyika, 2. Gallas, 3. Mohamed, 4. Isihaka, 5. Owino, 6.Mkude/Seseme, 7.Chanongo, 8/Ndemla/Kisiga, 9.Maguri, 10.Kiemba/Messi, 11.Okwi 

  Matokeo ya michezo mingine
Mbeya City 0-Azam FC 1

Coa
stal 2-Mgambo 0
Ndanda
1-Ruvu Shooting 3
Mtibwa 0-Polisi 0

Kagera 0-Stand Utd 0

Thursday, October 09, 2014

MARAIS WA MATAIFA YALIYOATHIRIKA NA EBOLA WAOMBA MSAADA

Marais wa Liberia ,Sierra Leone na Guinea,mataifa matatu yalioathirika vibaya na Ebola wanataka msaada zaidi ili kuwasaidia kukabiliana na ugonjwa wa Ebola. Rais wa Sierra Leone Ernest Bai Koroma ameiambia banki ya dunia katika mkutano mjini Washington kwamba jamii ya kimataifa haijachukua hatua za dharura kwa kuwa watoto wanaendelea kuwa mayatima,huku madaktari na wauguzi wakifariki. Naibu wa shirika la afya duniani Bruce Aylward ameuambia mkutano huo kwamba Ebola imesambaa katika miji yote mikuu ya mataifa hayo matatu yalioathirika pakubwa na kwamba ulikuwa unaenea kwa kasi katika kila eneo. Afisa mkuu wa matibabu nchini Marekani Thomas Frieden amesema kuwa mlipuko wa Ebola hauwezi kufananishwa na ugonjwa mwengine tangu kuzuka kwa ugonjwa wa ukimwi.

Tuesday, October 07, 2014

DIKTETA WA ZAMANI HAITI JEAN CLAUDE DUVALIER AFARIKI

  Kiongozi wa zamani wa utawala wa kimabavu wa Haiti, Jean Claude 'Baby Doc' Duvalier, amefariki kutokana na mshtuko wa moyo, akiwa na umri wa miaka 63. Duvalier alitawala taifa hilo maskini la bahari ya Caribean kuanzia 1971 hadi kupinduliwa kwake na wananchi 1986. Kama babake, 'Papa Doc' Duvalier, Baby Doc alitawala kwa ukatili akitumia hasa kikosi maalum cha polisi wanamgambo maarufu kwa jina la 'Tonton Macoutes', katika kuwakandamiza wananchi. Wanamgambo hao wanatuhumiwa kwa mauwaji na kutoweka kwa mamia ya watu kisiwani humo. Baada ya kuishi miaka 25 uhamishoni Ufaransa, Baby Doc alirudi nyumbani 2011 kufuatia tetemeko kubwa kabisa la ardhi kuwahi kutokea nchini humo 2010. Aliporudi nyumbani alifunguliwa mashtaka ya ulaji rushwa, utumiaji mbaya wa utawala wake pamoja na ukatili ulotendeka chini ya utawala wake.

RAIS UHURU KENYATTA KIZIMBANI THE HAGUE

  Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta ameondoka nchini humo leo kuelekea The Hague ili kuhudhuria kikao juu ya kesi inayomkabili katika mahakama ya kimataifa –ICC
  Jumatatu Bw. Kenyatta alitoa hotuba isiyo ya kawaida kwa wabunge na maseneta iliyopeperushwa moja kwa moja kupitia vyombo vya habari na kwenye mtandao wa internet.   Katika hotuba hiyo Bw. Kenyatta alimkabidhi madaraka ya muda naibu rais William Ruto ili aweze kwenda Uholanzi bila kuacha pengo la madaraka. Alisema anakwenda kwenye mahakama hiyo kama mwananchi wa 'kawaida' na kusisitiza kuwa kamwe hana hatia. Yeye pamoja na naibu rais Ruto, wanashtakiwa kwa kuchochea ghasia za baada ya uchaguzi mkuu mwaka wa 2007, ambapo maelfu ya wakenya waliuawa na wengine wengi kulazimika kutoroka manyumbani mwao. Katika uchaguzi huo, rais wa zamani Mwai Kibaki na aliyekuwa Waziri Mkuu Raila Odinga walikuwa wanagombania urais. Bwana Kenyatta hata hivyo na mgombea mwenza William Ruto walichaguliwa na Wakenya kuongoza taifa hilo na kuapishwa mwezi Aprili mwaka 2013. Wote wawili wamekanusha kuhusika na ghasia hizo na wameshirikiana na mahakama hiyo ya ICC. Ni mara ya kwanza kwa rais anayehudumu kuwa katika mahakama hiyo ya kimataifa. Kesi ya Bw. Kenyatta itasikilizwa Jumatano.

ALIYEBADILI JINSIA ASHINDA KESI KENYA

  Mwanamke aliyebadili jinsia yake ya kiume na kuwa mwanamke na kutaka jina lake kubadilishwa kwenye cheti chake cha mtihani ameshinda kesi yake dhidi ya baraza la kitaifa la mitihani nchini Kenya.    Mahakama imelazimisha baraza hilo kumpa Adrey Mbugua cheti kipya kinachoonyesha hali yake mpya ya kijinsia hasa kwa kuwa anapokea matibabu ya kufanikisha jinsia yake kubadilika kabisa. Bi Mbugua alilishitaki baraza la kitaifa la mitihani nchini humo kwa kukataa kubadililisha utambulisho wa jinsia yake kwenye cheti hicho kutoka kwa Mwanamme na kumtambua kama mwanamke licha ya amri iliyotolewa katika gazeti rasmi la serikali. Jaji Weldon Korir amelipatia baraza hilo hadi siku 45 kubadilisha jina la Adrey katika cheti hicho kutoka kwa 'Andrew Mbugua' na utambulisho wa mwanamume na kulibadilisha kuwa jina la kike la 'Audrey Mbugua' bila ya kuweka jinsia yoyote. Jaji alisema kuwa jinsia ya Adrey kwenye cheti hicho haiongezi thamani yoyote kwa matokeo yake wala alama alizopata Audrey na kuondolewa kwake vile vile hakuna athari yoyote. Aliongeza kuwa Audrey ameonyesha kuwa yuko tofauti na hivyo ndivyo anavyopaswa kutambuliwa. 'Audrey ni mwanadamu ambaye anajitambua kwama mwanamke wala sio kama mwanamume jinsia aliyozaliwa nayo,'' alisema jaji. Jaji alisema kuwa katiba ya nchi inaamrisha watu kuwaheshimu wengine kama ipasavyo bila ubaguzi wowote na kwamba heshima hiyo inahusu mambo mengi ikiwemo mtu anavyotaka kutambuliwa. Aliongeza kuwa ili Audrey kuhisi kuwa sawa anapaswa kukubalika kama alivyo na kumyima haki hiyo ya kubadilisha jina lake katika chati chake itakuwa ukiukwaji wa haki zake za kibinadamu. Wakili wa Audrey, aliambia mahakama kuwa mteja wake alizaliwa na kasoro ya kijinsia na kwamba anaendelea kupokea matibabu.

Monday, October 06, 2014

SIERRA LEONE REPORTS RISE IN EBOLA DEATHS

  The number of deaths caused by Ebola has reached 678 in Sierra Leone, according to the country's health ministry. WHO officials are still verifying the rapid spike figures. Ebola has claimed 678 lives in Sierra Leone, officials in the West African country's capital Freetown reported on Sunday. The figure is a significant increase on the 557 deaths the health ministry reported the day before. Last week, Sierra Leone communicated to the World Health Organization (WHO) that there had been 575 Ebola deaths and 48 more cases where Ebola may have been the cause of death - a total of 632. The figures have, however, caused some confusion because the health ministry reported 557 deaths on Saturday, implying that there were 121 more cases between Saturday and Sunday. The numbers have not yet been verified by the WHO. In all, the WHO has verified 3,431 Ebola-related deaths in Liberia, Sierra Leone and Guinea. Out of these, 2,069 have died in Liberia alone because of the infection which causes severe bleeding, fever and diarrhea. West Africa needs more help Meanwhile, Liberia's ambassador to Germany, Ethel Davis, called on Monday for more contributions to stop the disease from spreading and said that "if the virus were not stopped, it would cross the borders of countries dealing with the infection." Speaking in Berlin, Davis said that West Africa needed more help or else it "would be lost" without any assistance to combat the tropical fever. German aid organization ISAR has constructed quarantine stations in the Liberian capital, Monrovia, with facilities to treat 44 patients infected with the Ebola virus. However, ISAR chief Thomas Laackmann told German news agency DPA that more needs to be done. "Even now, patients are being sent back from hospitals and people are dying on the streets every day," he said. Donations not forthcoming Donations from the German public to combat Ebola have not been easy to come by. Manuela Rossbach of the aid organization Aktion Deutschland Hilft lamented meager collections of only 90,000 euros ($113,000) compared to more generous contributions for other catastrophes. The German government is also planning to airlift supplies from Senegal to Ebola-affected countries. The aid would include medicines and supplies worth 17 million euros. German soldiers have also been asked to volunteer to help in Ebola-affected areas. Aid organization ASB has also begun a project aimed at Ebola prevention and creating awareness about the virus in Gambia, which is vulnerable to the disease because of its proximity to Senegal and because of its lack of medical supplies.

JULES BIANCHI APATA AJALI KWENYE MASHINDANO YA JAPAN GRAND PRIX

  Katika Mashindano ya mbio za magari ya langa langa ya Formula One dereva wa Ufaransa, Jules Bianchi, yuko katika chumba cha wagonjwa mahututi baada ya kuumia vibaya kichwa chake kutokana na ajali ya kugongana na dereva mwingine katika mashindano ya Japan Grand Prix. Madaktari wa upasuaji wanaendelea kumhudumia dereva huyo mwenye umri wa miaka 25, ambaye alipoteza fahamu wakati alipofikishwa hospitalini hapo. Bianchi alipoteza uelekeo wa gari lake kutokana na mvua kubwa iliyokuwa ikinyesha, hata hivyo ajali hiyo iliyosababishwa na mwendo kasi mkubwa. Dereva wa Uingereza Lewis Hamilton alitangazwa mshindi katika mashindano hayo.

Sunday, October 05, 2014

YANGA YAICHAPA JKT RUVU 2-1

Kikosi cha timu ya Young Africans chini ya kocha mbrazil Marcio Maximo leo kimeendeleza wimbi la ushindi katika michezo ya Ligi Kuu ya Vodacom baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya timu ya maafande wa jeshi la Kujenga Taifa nchini  JKT Ruvu mchezo uliofanyika kwenye dimba la Uwanja wa Taifa jijin Dar es salaam. Young Africans iliingia uwanjani leo ikiwa na kumbukumbu ya ushindi  wa mabao 2-1 dhidi ya maafande wa jeshi la Magereza nchini Tanzania Prisons iliyoupata mwishoni mwa wiki na ikatumia chachu hiyo hiyo kupata ushindi kama huo katika mchezo wa leo. Mlinzi wa kati wa timu ya Young Africans Kelvin Yondani "Cotton" aliipatia timu yake bao la kwanza dakika ya 32 ya mchezo kwa shuti kali akiitumia vizuri pasi nzuri ya kiungo Haruna Niyonzima aliyewatoka walinzi wa JKT Ruvu na kumpasia Yondani ambaye pia ndiye alianzisha mashambulizi ya bao hilo toka langoni mwa Yanga na kufunga bao lake la kwanza ndani ya klabu ya Young Africans. Washambuliaji wa Young Africans wakiongozwa na Geilson Santos "Jajaj", Saimon Msuva na Andrey Coutinho walikshindwa kuzitumia nafasi walizozipata kutokana na kutokua makini na mipira kuokolewa na walinzi wa JKT.  JKT Ruvu walicharuka na kucheza kwa nguvu kwa kukamia na kukuta wachezaji wake wakipewa kadi za njano baada ya kuwachezae vibaya wachezaji wa Young Africans wakiwemo Jaja, Niyonzima na Msuva. Kipindi cha pili kilianza kwa timu zote kufanya mabadiliko ambapo Young Africans iliwaangiza Mrisho Ngasa, Nizar Khalfani na Salum Telela waliochukua nafasi za Andrey Coutinho, Haruna Niyonzima na Edward Charles aliyeumia mabadilko ambayo yalileta tija kwa kikosi cha Maximo. Dakika ya 73 ya mchezo kiungo Haruna Niyonzima aliipatia Young Africans bao la pili kwa mpira wa adhabu kufuatia kiungo Hassan Dilunga kuchezewa madhambi nje kidogo ya eneo la hatari na Niyonzima kupiga mpira uliojaa moja kwa moja wavuni na kumuacha mlinda lango wa JKT Ruvu Chove akiduwaa. Young Africans iliendelea kulishabulia lango la JKT kwa mpira wa speed kupitia kwa Msuva na Ngasa lakini mipira yao ya mwisho haikuwa na madhara na kukuta harakati zao zikiishia mikononi mwa golikipa Chove wa JKT Ruvu. Dakika ya 88 ya mchezo kiungo wa Jabir Aziz aliipatia timu yake ya JKT Ruvu bao la kufutia machozi kwa shuti kali baada ya kuitumia vyema pasi ya Amos Mgisa aliyewazidi ujanja walinzi wa Young Africans na kumkuta mfungaji alipiga shuti kali na kumuacha golikipa Dida akiruka bila mafanikio. Mpaka dakika 90 za mchezo zinamalizika, Young Africans 2 - 1 JKT Ruvu Stars, matokeo ambayo yanaipeleka timu ya Young Africans mpaka kwenye nafasi ya tatu ya msimamo wa Ligi Kuu ya Vodacom 2014/2015.  Young Africans: 1. Deo Munish "Dida", 2. Juma Abdul, 3.Edward Charles/Salum Telela, 4. Nadir Haroub "Cananavao" (C), 5.Kelvin Yondani, 6.Mbuyu Twite 7.Hassan Dilunga, 8.Haruna Niyonzima/Nizar Khalfani 9.Geilson Santos "Jaja" 10.Andrey Coutinho/Mrisho Ngasa 11.Saimon Msuva
  Mchezo mwingine ulichezwa huku Manungu Turiani kati ya Mtibwa na Mgambo JKT,Mtibwa wamepata ushindi wa goli 1-0 na kufikisha pointi 9 na kuweza kuongoza ligi wakifuatiwa Azam yenye pointi 7 

Saturday, October 04, 2014

SIMBA YATOKA SARE NA STAND UNITED

  Timu ya Simba ya Dar es salaam leo imelazimishwa sare na Stand United ya Shinyanga kwenye uwanja wa Taifa ambapo Simba walikuwa wenyeji kwenye mfululizo wa ligi kuu ya Vodacom.
  Simba walianza mchezo huo kwa kasi na kuwafanya Stand United kucheza mchezo huo kwa hofu kubwa na kuwafanya Simba kutawala mchezo huo kwa kipindi kirefu lakini safu ya ushambuliaji haikuwa makini na kupoteza nafasi kadhaa za kufunga.
  Lakini hata hivyo Simba ilifanikiwa kupata goli dakika ya 35 likifungwa na Shaaban Kisiga kutokana na uzembe mkubwa wa walinzi wa Stand United,furaha ya Wanasimba hao ilikatizwa dakika ya 44 na Heri Mohamed aliposawazisha goli hilo kwa kumalizia krosi iliyochongwa kutoka kushoto na kufanya matokeo kuwa 1-1 hadi mwisho wa mchezo.
  Hii ni sare ya tatu mfululizo kwa Simba na kuwafanya na pointi 3 kwa michezo mitatu waliocheza,mchezo wa kwanza walitoa sare ya 2-2 na Coastal Union uwanja wa Taifa,mchezo wa pili 1-1 na Polisi Moro uwanja wa Taifa na mchezo wa tatu ndio huu wa leo hali inayoonekana sio nzuri hasa watavyotoka nje ya uwanja wa Taifa ambao wanautumia kama uwanja wa nyumbani.
  Michezo mingine iliyochezwa leo na matokeo yake ni:-
.Coastal Union 2-Ndanda FC 1
.Tz Prison 0- Azam 0
.Polisi Moro 1 Kagera 1
.Ruvu Shooting 0- Mbeya City 0
Michezo mingine miwili itaendelea kesho kati ya Yanga na JKT Ruvu uwanja wa Taifa na Mtibwa na Mgambo JKT uwanja wa Mkwakwani Tanga.

Monday, September 29, 2014

YANGA SASA YAANZA LIGI

  Baada ya kupoteza mchezo wa kwanza kwa kufungwa na Mtibwa Sugar wiki iliyopita,Yanga wamefanikiwa kupata ushindi wa goli 2-1 dhidi ya Tanzania Prison ya Mbeya kwenye mchezo uliochezwa uwanja wa Taifa Dar es salaam.
  Mchezo ulianza kwa Yanga kumiliki kipindi cha kwanza idara zote na kufanikiwa kupata goli dakika ya 34 likifungwa na Mbrazil Andre Coutinho goli hilo lilidumu hadi mapumziko.
  Kipindi cha pili Prison walirudi na kufanya mashambulizi ya kushitukiza na kufanikiwa kusawazisha bao hilo dakika ya 62,kabla ya Simon Msuva kuipatia Yanga goli la pili dakika ya 67 kwa kichwa kufuatia pasi ya Mrisho Ngassa hadi mwisho wa mchezo Yanga 2-Prison 1.
  Katika mchezo mwingine huko Chamazi Complex timu ya Kagera Sugar iliibuka na ushindi wa goli 2-0 dhidi ya JKT Ruvu.

Kikosi cha Yanga
Shabiki maarufu wa Yanga na Taifa stars anayejulikana kwa jina la Ally Yanga akiwa na wenzake uwanja wa Taifa

Saturday, September 27, 2014

DAMPO JIRANI NA SHULE NI UKATILI KWA WATOTO

Eneo lililofanywa dampo
  Shule ya msingi Simike jijini Mbeya ipo katika wakati mgumu kutokana na kuwa jirani na sehemu ya kutupia takataka ambazo zinaweza kuhatarisha afya za wanafunzi hao hasa yanapotokea magonjwa ya mlipuko.
  Kumekuwa na kiasi kikubwa cha takataka ambazo zimekuwa zikitupwa bila kuondolewa kwa wakati na hivyo kufanya eneo hilo kuwa mrundikano mkubwa wa taka jirani na shule hiyo na kuwa na harufu mbaya na hewa nzito.
  Mamlaka husika zinapaswa kuangalia maeneo ya kutupia taka au kuzitoa mapema hasa maeneo ambayo yako jirani na watoto au shule ili kuwanusuru watoto na maradhi wanayoweza kuyapata,
tunaamini kwa hili linawezekana kama wahusika wakijipanga vizuri.
Lundo la taka
Huu ndio ukuta wa shule ambao uko jirani na sehemu hii ya kutupia taka.

POLISI MORO YAWABANIA SIMBA

  Timu ya Polisi ya Morogoro leo imeilazimisha timu ya Simba ya Dar es salaam sare ya goli 1-1 kwenye mchezo wa pili wa ligi kuu ya Vodacom, mchezo huo umechezwa uwanja wa Taifa Dar es salaam ambapo Simba walikuwa wenyeji.
  Mchezo huo ulianza kwa simba kutawala kipindi cha kwanza na kuwawezesha kupata goli lililofungwa na Emmanuel Okwi na kuenda mapumziko wakiwa mbele kwa goli moja,kipindi cha pili Polisi Morogoro waliingia uwanjani wakiwa wamebadilika na kufanya mashambulizi ya kushtukiza na kusawazisha goli kupitia kwa Dan Mruanda aliyepokea pasi ya Salum Machaku na kumchambua golikipa wa Simba Hussein Sharrif na kuukwamisha mpira wavuni kiufundi.
Polisi walionyesha kandanda safi baada ya kuingia kwa Christopher Edward na Seleman Selembe na kukosa magoli mawili ya wazi ambayo yangeweza kupeleka majonzi mtaa wa Msimbazi.
Matokeo mengine ya ligi kuu ya Vodacom kwa leo:-
 .Azam FC 2-Ruvu Shooting 0
 .Mtibwa 3-Ndanda FC 1
 .Mgambo JKT 0-Stand UTD 1
 .Mbeya City 1-Coastal 0
  Ligi hiyo itaendelea kesho kwa mechi mbili ambapo uwanja wa Taifa Dar es salaam Yanga watawakaribisha Tanzania Prisons ya Mbeya na JKT Ruvu watakuwa wenyeji wa Kagera Sugar kwenye uwanja wa Chamazi Complex.
Mpaka sasa Didier Kavumbagu wa Azam anaongoza kwa kupachika magoli akiwa na magoli manne kwa mechi mbili .

Hiki ni kikosi cha polisi Morogoro kabla ya ligi kuu

Monday, September 22, 2014

STAND UNITED WAMILIKI WAKE NI WAPIGA DEBE NA MAKONDA KIHALALI,TUNAJIFUNZA NINI?SISI WENYE MAKAMPUNI.


Hiki ndio kikosi cha Stand United
 UKITUA katika Mkoa wa Shinyanga, hususan maeneo ya stendi ya zamani ya mabasi ya mikoani na wilayani, utakutana na shamrashamra za makonda, madereva na wapiga debe ambao wanaendelea na shughuli zao za kujipatia riziki. Lakini hao makonda, wapiga debe, mawakala na madereva, ndiyo chachu na mafanikio ya Stand United, kwani wao ndiyo waanzilishi na wamechangia kwa kiasi kikubwa kuifanya timu hiyo ifike hapo ilipo tangu ilipoanzishwa mwaka 2012.  Stand inaongozwa na viongozi wenye uchungu na mpira na uchu wa mafanikio katika soka, ndiyo maana wamefanikiwa kwa kiasi fulani. Wanaendesha timu huku wakiendelea na majukumu yao ya kila siku na kazi zao, ingawa wanahakikisha kila kitu kinakuwa kinaenda sawa kabisa bila tatizo katika mabasi wengine maduka yanayozunguka eneo hilo la stendi. Unapofika Stand, unakutana na makamu mwenyekiti wa timu hiyo, Masumbuko Charles ambaye ni mmoja wa mawakala wa basi la Loquman ambalo linafanya kazi ya kusafirisha abiria kutoka wilaya za Meatu na Bariadi hadi mkoani Dodoma. Licha ya Masumbuko kuwa na majukumu mengi, timu inapofanya mazoezi huwezi kumkosa. “Uwepo wangu katika timu hii ni furaha kwa sababu ilikuwa ndoto yetu hapa tangu muda na imefanikiwa kutimia kwa kiasi mpaka hapa tulipofika, tutapigana kwa sababu mwanzo tulikuwa tunasumbuliwa na ukata lakini tumetimiza ndoto kwa kiasi,” anaeleza Masumbuko. Rashid Daghesh ambaye ni kocha wa kwanza wa Stand kwa sasa ni mjumbe wa kamati kuu ya timu hiyo huku aliyekuwa msaidizi wake Aman Vincent akiwa ndiye mwenyekiti wa timu kwa sasa. Rashid, pamoja na majukumu ya timu aliyonayo, pia ni wakala wa mabasi ya Ruska ambayo yanafanya shughuli zake mkoani humohumo. “Kitu ambacho naweza kujivunia Stand United ni pamoja na kuifanya timu kuwa hapa ilipofika sasa, kwa sababu zamani wakati nacheza timu yangu haikuwa na bahati ya kufika ligi kuu, sasa imepiga hatua, ni jambo la kheri,” anasema Rashid.  Mohamed Ally Hemed ‘Dulla’ yeye ni mmoja wa wadau walioanza kuisapoti timu tangu inaanza, akiwa ni mfanyakazi wa hapo na anamiliki basi la Bedui Ruska ambalo ameamua kuweka jina kubwa la timu katika basi hilo. “Naipenda sana timu hii popote iendapo huwa naisapoti kwa kiasi kikubwa tangu tumeanza kuichangia Sh 500 kipindi hicho,” anaeleza. Araf Nassor akiwa ni Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Stand United naye ni wakala wa mabasi ya Ruska lakini akiwa pia ni mmoja wa waasisi wa timu. “Timu imepiga hatua kwa kiasi kikubwa lakini napenda kuwaambia Watanzania kuwa, Stand United si timu ya wahuni, wala wafanya fujo, sisi ni watu wa malengo, ndiyo maana tumefika hapa, japo ukata kwa sana lakini tunapigana kuendesha timu,” anasema Nassor. Je, mashabiki wanaisapoti vipi timu? “Timu ilipokuwa ikienda mikoani, kipindi hicho walikuwa wanagharamiwa na timu kwa kupitisha mabakuli na kuchangisha na hawa mashabiki wetu wapo katika makundi mawili, Full Shangwe ambao muda wote wanaishangilia timu pamoja na Babu Kubwa, wote hawa ni mashabiki wa timu yetu. “Pia kwa sasa baada ya kupanda, mtashuhudia Bendi ya Stand ikitoa burudani katika michezo yake tofauti wakati ligi kuu itakapokuwa ikiendelea,” anafafanua Nassor. Hao ni baadhi ya wadau na viongozi wa Stand United ambao wamekuwa na timu tangu inaanza mpaka hapo ilipofikia, ingawa haikuwa kazi rahisi kufika hapo walipofika.

COASTAL UNION YAIGOMEA SIMBA

Timu ya Coastal Union ya Jijini Tanga imelazimisha sare ya goli 2-2 dhidi ya Simba kwenye uwanja wa Taifa Dar es salaam,ikiwa ni mchezo wa kwanza wa ligi kuu ya Tanzania bara.
  Simba ilikianza kipindi cha kwanza kwa kasi na kujipatia magoli mawili yaliyofungwa na Shaaban Kisiga na Amisi Tambwe,mabao yalidumu hadi mapumziko.
Coastal walirudi kipindi cha pili wakiwa na machungu na kufanikiwa kusawazisha magoli yote na hivyo kuwanyima Simba ushindi ambao tayari walikuwa na uhakika nao hadi kipenga cha mwisho timu hizo zimetoka 2-2.

Saturday, September 20, 2014

YANGA YAANZA LIGI YA VPL KWA KUCHAPWA 2-0 NA MTIBWA

Timu ya Yanga ya Dar es salaam leo imeanza ligi kuu ya Tanzania bara kwa kufungwa goli 2-0 na Mtibwa Sugar kwenye uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.
Wenyeji wa mchezo huo wakicheza kwa kujiamini na kufanya mashambulizi ya kushitukiza waliduwaza Yanga dakika ya 15 ya mchezo baada ya Mussa Hassan Mgosi kupachika bao la kwanza kwa kuwazidi ujanja walinzi wa Yanga.
Baada ya bao hilo Yanga walikuja juu na kulisakama lango la wapinzani wao na kupata goli ambalo mwamuzi wa mchezo huo alikataa na kutoa penati kwa Yanga ambayo iliota mbawa,penati hiyo ilipigwa na Mbrazil Jaja na kumgonga miguuni golikipa Said Mohamed muda mfupi baadaye Yanga waliweza tena kupata goli lakini mwamuzi aligoma kwa madai mfungaji alikuwa ameotea.
Timu hizo zilienda mapumziko huku Mtibwa ikiwa mbele kwa goli 1-0,kipindi cha pili Yanga waliingia na kutawala mchezo huo lakini bahati haikuwa yao kwani dakika ya 83 Ame Ally aliifungia Mtibwa goli la pili hadi mwisho wa mchezo Mtibwa 2 Yanga 0
Michezo mingine iliyochezwa leo na matokeo yake:-
.Azam 3-Polisi Moro 0
.Ndanda FC 4-Stand Utd 1
.Mgambo JKT 1-Kagera 0
.Ruvu shooting 0-Prisons 2
.Mbeya City 0-JKT Ruvu 0
Ligi hiyo itaendendelea kesho kwa mchezo mmoja kati ya Simba na Coast Union uwanja wa Taifa Dar es salaam.

UHARIBIFU WA MAZINGIRA KWA KUKATA MITI WAZIDI KUPAMBA MOTO RUKWA

Katika hali isiyokuwa ya kawaida wananchi wa kijiji cha Mtakuja njia iendayo Kapele Kasusu wilayani Sumbawanga wamekuwa wakikata misitu ili kupata maeneo ya kulima ulezi.
Wananchi hao wamekuwa wakifanya uharibifu mkubwa wa mazingira kutokana na kulima mazao ya muda mfupi ambayo faida yake ni ndogo ukilinganisha na misitu hiyo,wanachohitaji ni kupewa elimu juu ya utunzaji wa mazingira hususani ukataji miti ovyo,inabidi juhudi za haraka zichukuliwe ili kuinusuru hali hiyo ambayo inaweza kuli
fanya eneo hilo kukosa mvua kwa miaka ya baadaye.
Hizi ni baadhi ya picha ya msitu huo unaoshambuliwa kwa kasi.

Hii ni miti ambayo imeangushwa
Msitu ukiwa umekatwa na wananchi kwa ajili ya kilimo cha ulezi.

Saturday, September 06, 2014

WATU ZAIDI YA 30 WAFARIKI KWENYE AJALI MUSOMA LEO

 Zaidi ya watu 30 wamefariki kwenye ajali iliyohusisha magari matatu eneo la Sabasaba mjini Musoma leo,ajali hiyo imetokea leo mchana kwa kuhusisha mabasi mawili ya Mwanza Coach na J4 Express na gari ndogo aina ya Nissan Terrano baada ya J4 Express kuigonga ubavuni Nissan hiyo kuisukumia mtoni kabla ya kukutana uso kwa uso na Mwanza Coach nje kidogo ya daraja.
 Sababu kubwa ni mwendo kasi wa mabasi hayo ambayo yalikutana kwenye daraja ambalo ni jembamba na kusababisha maafa kwa abiria na wengine kujeruhiwa.
  Haraka za madereva wa mabasi zimekuwa ni vyanzo vya ajali nyingi ambazo zingeweza kuepukika lakini imekuwa ni kawaida kwa madereva kujifanya kama hawajui nini kinaweza kutokea kutokana na mwendokasi wao na hii imekuwa ikichangiwa hata na baadhi ya abiria wanaojifanya wana haraka za kuwahi biashara zao na kuwakejeli madereva wanaokwenda mwendo wa taratibu.
Hii ni sehemu ya mabaki ya basi baada ya ajali
Baadhi ya wananchi wakiangalia kwa hudhuni moja ya basi lililopata 

Saturday, August 30, 2014

YANGA YATANGAZA KAMATI YA NIDHAMU,MAADILI NA SHERIA.

  TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
 Mwanasheria Sam Mapande, Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya YANGA –(Utawala Bora) anapenda kutoa taarifa kupitia vyombo vya habari kwa wana YANGA,ameunda Kamati ndogo chini ya Kamati ya Utendaji wa YANGA zifuatazo:
1) KAMATI YA MAADILI Wajumbe:   1) Fimbo, Mgongo Prof. (Advocate) 2) Kabudi, Mpalamaganda Prof. (Advocate)  3) Njaa, Salehe Ramadhani (Advocate) 4) Rashidi, Tausi Abdallah (Advocate) 5) Tenga, Cathbert (Advocate)
 2) KAMATI YA NIDHAMU Wajumbe:
  1) Karua, Tedy  2) Lamlembe, Roger 3) Kihanga, Pascal  4) Mahenge, Burton Yesaya 5) Mudhihir, Mudhihir (Advocate) 3)
 KAMATI YA SHERIA NA KATIBA  Wajumbe:
   1) Fimbo, Mgongo Prof. (Advocate) 2) Gikas, Farija (Advocate) 3) Kabisa, Jessica (Advocate) 4) Kabudi, Mpalamaganda Prof. (Advocate)  5) Kambamwene, January (Advocate) 6) Lupogo, Herman (Advocate) 7) Madibi, Richard (Advocate) 8) Mahenge, Burton Yesaya 9) Mgongolwa, Alex (Advocate) 10) Mkucha, Elisha (Advocate) 11) Mudhihir, Mudhihir (Advocate) 12) Njaa, Salehe Ramadhani (Advocate) 13) Rashidi, Tausi Abdallah (Advocate) 14) Tenga, Cathbert (Advocate) 15) Tenga, Ringo Dr. (Advocate) 16) Vedasto, Audax (Advocate 4)
 KAMATI YA UCHAGUZI Wajumbe:
  1)  Kajole, Mustafa  2)  Lundenga, Hashim Ibrahim  3)  Makele, Bakili  4)  Mlelwa, Daniel    5) Ngongolwa, Alex (Advocate) Ifahamike kwamba, kutakuwa na nyongeza ya uteuzi wa Wajumbe wengine wa Kamati za YANGA zilizotajwa hapo juu. Mwanasheria Sam Mapande, Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya YANGA – (Utawala Bora) atakuwa Mwenyekiti wa Kamati zilizotajwa hapo juu. Kamati ya Utendaji ya YANGA, ina karibisha Wajumbe waliotajwa katika Kamati zilizotajwa hapo juu kwa dhamira njema kuwa watasaidia kujenga YANGA bora, na wanaomba ushirikiano kutoka kwa wanaYanga wote ili Wajumbe walioteuliwa waweze kutenda kazi zao vyema kwa manufaa ya YANGA. (YANGA DAIMA MBELE NYUMA MWIKO) (BENO NJOVU) KATIBU MKUU WA YANGA

Friday, August 29, 2014

AJALI KUBWA YATOKEA MBALIZI MBEYA

 Wimbi la ajali limezidi kulikumba jiji la Mbeya baada ya leo kutokea ajali eneo la Mbalizi na kugharimu maisha ya watu wasiopungua kumi na wengine zaidi ya sita wakijeruhiwa.
 Ajali hiyo imehusisha gari ya abiria(daladala) na lori dogo aina ya TATA, na kuleta simanzi kubwa kwa wakazi wa Mbalizi na maeneo ya jirani.
Wananchi wa Mbalizi wakiwa wamepigwa butwaa baada ya ajali iliyosababisha vifo vya watu.

Sunday, August 24, 2014

EL-MERREIKH MABINGWA AFRIKA MASHARIKI NA KATI 2014

  Timu ya El-merreikh ya Sudan imefanikiwa kutwaa ubingwa wa Afrika mashariki na kati kwa kuwafunga APR ya Rwanda kwa bao 1-0,bao pekee la El-merreikh limefungwa na Allan Wanga dakika ya 25 ya mchezo na kuwafanya APR kushindwa kufurukuta mbele ya mashabiki wao na kunyang'anywa tonge mdomoni na wasudan hao.
  Mechi ya kutafuta mshindi wa tatu ilichezwa mapema na Police Rwanda wamepata nafasi hiyo kwa kuitoa KCCA ya Uganda kwa penati 4-2.

Wachezaji wa El-merreikh wakishangilia ushindi dhidi ya APR.

Tuesday, August 19, 2014

BIOGESI KWA MAISHA BORA

 Biogesi ni nishati itokanayo na kinyesi cha wanyama ambacho huchachuka ndani ya mtambo wa biogesi na kuweza kutumika kwa kupikia na kuwasha taa.
  FAIDA ZA BIOGESI:- .Haina moshi wala harufu mbaya
. Hupunguza madhara yanayosababishwa na moshi wa kuni au mkaa kama vile macho kuwa mekundu na kukohoa.
 .Huokoa muda Hupunguza muda wa kutafuta kuni hivyo kufanya shughuli nyingine za maendeleo.
 Mtandao huu umekutana na mtaalamu wa kutengeneza mtambo wa biogesi maeneo ya Mbinga Kigonsela bw.Linus Komba na kuelezea jinsi mtambo huu ulivyo rafiki wa mazingira,na kuwataka wananchi wa Tanzania hususani wale wanaoishi vijijini kuwasiliana naye ili aweze kuwasaidia na kuwafanya waendelee kuyatunza mazingira kwa kutokata miti,mnaweza kuwasiliana naye kwa simu yake ya mkononi +255 762 045 808,unaweza kuwasiliana naye na yuko tayari kuwafikia sehemu yeyote kwa ajili ya ushauri na matengenezo YATUNZE MAZINGIRA ILI UWAACHIE VIZAZI VIJAVYO SEHEMU NZURI YA KUISHI
Huu ndio mtambo wa biogesi ukiendelea kujengwa
Bw.Benjamin James akipata maelekezo kutoka kwa mafundi
Bw.Linus Komba akitoa maelezo kuhusu mtambo wa biogesi
Mafundi wakiendelea na kazi ya kukamilisha mtambo huo.

Sunday, August 17, 2014

MANCHESTER UNITED YAANZA VIBAYA EPL,YAPIGWA NYUMBANI

Ligi kuu ya Uingereza imefunguliwa huku matokeo yakiiduwaza Manchester United baada ya kukubali kichapo cha bao 2-1 wakiwa nyumbani,matokeo ambayo hawajawahi kuyapata kwenye mechi za ufunguzi toka mwaka 1972.
Matokeo yalikuwa kama ifuatavyo:-
Man United 1-Swansea City 2 West Brom 2-Sunderland 2 Stoke City 0 -Aston Villa 1 Leicester City 2 Final Everton 2 QPR 0-Hull City 1 West Ham 0 -Tottenham 1 Arsenal 2-Crystal Palace 1 Sunday, August 17 Liverpool 3:30 PM Southampton Newcastle 6:00 PM Man City Monday, August 18 Burnley FC 10:00 PM Chelsea Saturday, August 23 Aston Villa 2:45 PM Newcastle Chelsea 5:00 PM Leicester City Swansea City 5:00 PM Burnley FC Crystal Palace 5:00 PM West Ham Southampton 5:00 PM West Brom Everton 7:30 PM Arsenal Sunday, August 24 Hull City 3:30 PM Stoke City Tottenham 3:30 PM QPR Sunderland 6:00 PM Man United Monday, August 25 Man City 10:00 PM Liverpool All times are in East Africa Time

Wednesday, August 13, 2014

REAL MADRID YATWAA EUROPEAN SUPER CUP

Ronaldo akishangilia moja ya gola lake


Mabingwa wa kihistoria wa UEFA CHAMPION LEAGUE,Real Madrid wamefanikiwa kuongeza kikombe kingine kwenye maktaba yao baada ya kuifunga Sevilla ya Spain bao 2-0 kwenye mchezo uliofanyika uwanja wa Cardiff,mabao ya Real Madrid yakifungwa na mchezaji hatari Christiano Ronaldo dakika ya 30 na 49.
  Sevilla walikuwa kama timu iliyokata tamaa kabla ya kuingia uwanjani kutokana na Real Madrid kuwa na washambuliaji wenye gharama kubwa na uwezo mkubwa uwanjani kama Gareth Bale,James,Kloose

Ronaldo na wenzake wakifurahia ushindi

Sunday, August 10, 2014

MAONESHO YA KILIMO KUFANYIKA MJINI NI KUMNYIMA MKULIMA ELIMU NA MAARIFA YA KILIMO.

 Wakulima wa mazao mbalimbali wamekuwa hawapatiwi elimu juu ya uzalishaji wa mazao yao,na hivyo kulazimika kufanya kilimo cha mazoea na kujikuta wakiendelea kupata mavuno kidogo.
Pia kufanyika maonesho ya kilimo maeneo ya mjini kila mara ni kumnyima mkulima maarifa zaidi ya kilimo.
Ikiwa maonesho haya yakiwa yanafanyika vijijini yanaweza kuwafanya wakulima kubadilishana ujuzi na kujifunza mambo mengi zaidi kutoka maeneo mbalimbali ya nchi yetu,kuliko kufanyika kila wakati mjini na kuyafanya kuwa ya kibiashara zaidi na kutembelewa na watu wasiokuwa walengwa na kuwaacha wakulima wakibaki vijijini kwa kunywa pombe na kucheza ngoma na kuona hiyo ndio furaha ya sikukuu ya wakulima.

Shamba la miti lililoko Vwawa Mbozi
Ndizi zikiwa zimeandaliwa kwa ajili ya kusafirishwa huko Ushirika Tukuyu

Moja ya shamba la mpunga wilayani Kyela
Kakao wilayani Kyela
Shamba la mahindi Ruanda Mbozi.
Shamba la miparachichi Itipingi Njombe.

KAGAME CUP 2014

Gor Mahia FC 1-2 KCC FC KCC FC opened their 2014 Kagame Cup campaign with victory after coming from a goal down to beat KPL champions Gor Mahia 2-1in the second of the day’s game played at Amahoro stadium. Uganda Cranes striker Daniel ‘Mzee’ Sserunkuma gave the Kenyan champions a deserved lead in the 27th minute before substitute Brian Majwega equalised for the Ugandan champions seven minutes after recess and later Umony netted the winner in the 88th minute. Gor Mahia started the brighter side and dominated proceedings launching numerous attacks on the KCC FC goal but goalie Yasin Mugabi was up to the task whenever called upon. Bobby Williamson’s charges however got a deserved lead after Musa Muhammad beat Namwanja Simon down the left to cross for Sserunkuma who tapped home despite a forest of legs inside the 18 yard area. The goal saw KCC FC coach George ‘Best’ Nsimbe react by substituting in the inefficient Steven Bengo for Brian Majwega but the Kenyan champions held on to their first half lead in a dominant display. After recess, Nsimbe made another change bringing on Brian Umony for Herman Wasswa. The Ugandan side started to dominate the game at this time and deservedly equalised through Majwega tapping home a fine cross from Tom Masiko. The Ugandan side was in ascendency at the moment but couldn’t break a resilient Gor backline manned by David Owino. At the other end, Gor Mahia threatened with Sserunkuma and later Timothy Otieno forcing a double save from Yasin Mugabi. With two minutes left on the clock, Brian Majwega broke down the left on a counter move and his low cross met Umony who slid the ball at the far corner past Onyango for KCC FC’s winner. KCC FC now top group B with maximum points and return to action on Sunday against Atletico at Nyamirambo. Last modified onFriday, 08 August 2014 18:34 200

Friday, August 08, 2014

YANGA KUTOSHIRIKI KAGAME CUP KUTAPOTEZA WAPENZI WAPYA WA NDANI NA NJE YA TANZANIA

 Yanga ni moja ya timu kubwa ukanda huu wa Afrika mashariki na kati na pengine ndio inaweza ikawa timu yenye washabiki wengi kwa ukanda huu wa Afrika mashariki.
 Kitendo cha timu hii kuwa matatizo ya maramara na shirikisho la soka la Afrika mashariki na kati(CECAFA) na kuifanya timu hii kuondolewa kushiriki michuano ya kombe la Kagame,kuna uwezekano mkubwa wa timu kupoteza wapenzi wapya kwa sababu hamna mtu anayependa kujiingiza kwenye kitu ambacho kina matatizo kila mara,na athari zake haziwezi kuonekana leo hii inaweza ikaonekana miaka ishirini ijayo au zaidi,kwa sababu wapenzi wapya ni wale ambao wana umri wa miaka mitano hadi kumi.
Wakisherekea ubingwa
Kikosi cha Yanga