
Timu ya Simba ya Dar es salaam jana ilifanikiwa kusonga mbele kwenye michuano ya kombe la shirikisho licha ya kufungwa bao 3-1 na Es Satif kwenye uwanja wa May 8 mjini Satif-Algeria.
Simba wakicheza pungufu baada ya mlinzi wake kucheza faulo ya kizembe na kutolewa kwa kadi nyekundu dk.8,walibanwa sana wapinzani wao na kujipatia magoli hayo matatu.
Simba walitulia dak 7 za mwisho na kuweza kupata goli dk.92 likiwekwa kimiani na Emanuel Okwi na kuwafanya Simba kusonga mbele kwa faida ya goli la ugenini,wiki mbili zilizopita Simba walishinda 2-0 jijini Dar es salaam.
No comments:
Post a Comment