BENJAMINKAMINYOGE.BLOGSPOT.COM

Friday, June 12, 2015

CHRISTOPHER LEE - DIES AT THE AGE OF 93.


The ultimate on-screen villain has died at the age of 93

 Celebrated Hollywood actor Sir Christopher Lee has died at the age of 93, leaving fans to remember his legacy as the film industry's go-to bad guy.
Known for his well-spoken, powerful voice and his wide-ranging talents (heavy metal Christmas songs, anyone?), Lee was knighted in 2009 and received a Bafta Fellowship in 2011. Not to mention the fact that he has grossed more than $8.3 billion worldwide, making him one of the most successful actors of all-time.
While his favourite performance was as Muhammad Ali Jinnah in 1998 and he believed his best film to be The Wicker Man, his turns in the likes of Lord of the Rings, James Bond, Star Wars and The Curse of Frankenstein will live long in the memory. 

Here’s our pick of the Christopher Lee movies you must see right away:

Christopher Lee as Scaramanga in Man With The Golden Gun Christopher Lee as Scaramanga in Man With The Golden Gun The Man With the Golden Gun
As Scaramanga in the 1974 Bond film The Man With the Golden Gun Lee, who incidentally was the real-life step cousin of 007 author Ian Fleming, barely broke a sweat as the smooth wielder of the gilded pistol.
Lee played the freelance assassin as a plummy-voiced, steely and unflappable killer who is more than a match for the MI5 agent. His eyebrow acting (as ever) is to be applauded in this case.
 
The Wicker Man
Lee’s turn in cult British horror film The Wicker Man would haunt him for the rest of his career.
As the evil ruler Lord Summerisle converts the inhabitants of a small Scottish island away from Christianity back to the “old gods” of paganism – and lures a hapless police officer to become a human sacrifice.
Using his natural charm (and those twinkly eyes) to great effect, Lee’s villain even calmly explains to his victim the reason for his impending demise. All the more terrifying for his apparent zeal.
Christopher Lee as Count Dooku Christopher Lee as Count Dooku Star Wars
Playing another iconic villain, Lee was appeared in two of the Star Wars prequels as sith Lord Count Dooku. Even in his old age, Lee did much of the Lightsaber fighting himself – being an accomplished sword fighter himself - with one duel with Yoda being particularly fierce.
Long-time collaborator Peter Cushing had also previously starred in the Star Wars series but in episode 4, a New Hope.
Christopher Lee as Saruman Christopher Lee as Saruman
Lord of the Rings
After spending the Nineties avoiding massive blockbusters, Lee’s return would become one of his most-beloved roles. Saruman, as many of you know, is the terrifying white wizard-turned-evil in the Lord of the Rings trilogy.
Lee was a huge fan of the series and said he read the books each year. He was also the only cast member to ever meet JRR Tolkien, who at the time gave him his blessing to one day play Gandalf.
On set Lee would often discuss folklore with director Peter Jackson and help fellow actors speak Elvish, a language he spoke. You can watch him filming his final scene as Saruman below.

Christopher Lee as The Creature in 1957's The Curse of Frankenstein Curse of Frankenstein

This 1957 gothic Terrence Fisher horror earned mixed reviews from critics but proved popular with moviegoers and influenced the directorial royalty of Martin Scorsese and Tim Burton.

Lee’s gruesome portrayal of Victor Frankenstein’s psychotic monster created from scavenged human body parts will not be easily forgotten, for better or for worse.
Christopher Lee as the bloodsucking vampire Count Dracula in 1958's Horror of Dracula Dracula
Lee’s most iconic role was arguably as bloodsucking vampire Count Dracula in the 1958 horror movie. Few could do the guaranteed-to- give-you-nightmares villain thing quite like Lee – those bloody lips and hungry fangs still give us the shivers more than 50 years later. And as for that moment when Dracula peels away his decaying skin…terrifying.

Monday, June 08, 2015

BARCELONA MABINGWA ULAYA 2014/15


BARCELONA ndiyo mabingwa wapya wa Ligi ya Mabingwa Ulaya, hiyo siyo habari mpya kwa sasa lakini habari ni kuwa kwa nini Barcelona?


Wapo ambao wamekuwa wakimtazama Lionel Messi kuwa ndiye nguzo muhimu kwa timu hiyo kutwaa mataji matatu msimu huu, hilo ni kweli lakini hali halisi ni kuwa Barcelona imeshinda taji hilo kwa kuwa kila mtu kwenye timu kafanya kazi yake vizuri.

Messi amekuwa akionekana zaidi kwa kuwa uwezo wake ni wa kipekee na amekuwa akionyesha makubwa zaidi hata ya wenzake lakini baada ya kuanza msimu kwa kuyumba, hatimaye Barcelona ilianza kuelewana na kufanya kila mtu kucheza kwa kiwango cha juu.


Ushirikiano wa Messi, Neymar na Luis Suarez unastahili pongezi za kipekee kwa kuwa hawakuwa wachoyo, ndiyo maana hata juzi wawili kati yao walifunga huku mmoja akitengeneza mabao.

Fainali vs Juventus
Katika fainali ya juzi dhidi ya Juventus ambapo Barcelona ilishinda 3-1, usiku kipa chipukizi Marc-André ter Stegen, 23, hakuwa na kazi kubwa lakini alionyesha kujiamini, anaonyesha dalili za kuwa kipa bora miaka ijayo, hasa kama ataendelea kubaki klabuni hapo.

Mabeki wote walikuwa kwenye ubora wao, Dani Alves kama kawaida alisaidia mashambulizi kwa kupanda, japokuwa mara kadhaa alijisahau na Juventus kupata nafasi ya kupiga krosi kadhaa kutoka upande wake.

Gerard Pique ndiye beki aliyecheza vizuri kuliko wote, alipanda kusaidia mashambulizi, aliokoa vizuri, alicheza mipira ya juu na aliwapanga wenzake vizuri. Javier Mascherano alianza kwa kupaniki lakini baadaye alitulia na kuonyesha ubora wake.

Jordi Alba kama ilivyo kwa Alves alipanda mara nyingi na kuchangia bao la kwanza, hakuwa na kazi nzito ya kukaba.

Katika safu ya kiungo, ushirikiano wa Sergio Busquets na Ivan Rakitić ulikuwa na maana, wao ndiyo waliozima mashambulizi ya Juventus kutokea katikati.

Mkongwe Andrés Iniesta ndiye aliyekuwa injini ya Barcelona, kwa kuwa vijana wake wawili nyuma walifanya kazi nzuri, hiyo ilimrahisishia kuuchezea mpira, kuiendesha timu, kutoa pasi zenye macho na kuituliza Barcelona hasa mwanzoni mwa kipindi cha pili ambapo walionekana kupoteana kiasi.

Messi inawezekana hakuonyesha yale makeke yake ya kuukokota mpira na kuwapangua wapinzani lakini yeye na Iniesta ndiyo waliokuwa mafundi mitambo.

Messi alianza kutengeneza bao la kwanza kwa pasi yenye macho, kisha akatengeneza la pili ambalo lilitokana na ule uwezo wake binafsi ambao unajulikana.

Suarez licha ya kuwa staika wa kati lakini alifanya kazi nzuri ya kuwasumbua mabeki wa Juventus, kuna muda alirejea katikati ya uwanja ili kumsumbua Andrea Pirlo pindi Juventus walipokuwa wakimiliki mpira.

Kocha wa Barcelona, Luis Enrique alipanga kikosi kizuri na mbinu zake zilifanikiwa. Mabadiliko aliyoyafanya yalikuwa na maana kubwa na faida, Jérémy Mathieu aliingia kuzuia, Juventus wakapanda kujua wapinzani wao wamezidiwa, wakajikuta wanapigwa la tatu kwa shambulizi la kushtukiza.

Xavi Hernandez aliingia kuituliza timu na akafanikiwa kwa hilo, Pedro ni mjanjamjanja na ndiye aliyesaidia bao la tatu.
Moja ya vituko baada ya mechi kuisha ni mlinzi wa Barcelona Gerald Pique akikata nyavu kwa kutumia mkasi

Pique akiwa kajifunika nyavu
Messi akiwa anashangilia kwa kulibeba kombe la Ulaya
Neymar akilibusu kombe

Thursday, May 21, 2015

MASHABIKI WA SOKA WAHUDHUNISHWA NA MATOKEO YA TAIFA STARS KWENYE COSAFA CUP.

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhm9LxZHCAuvoeLFUnpW6Fole9Yr6FftQj5cPUQT9nifi0CwuTdFMpVdB9U5lPJ83rxZ5_02Ls1rpPBssbygTteQ887Rx3w_-Ff0m0ATDDwHWwxQvkB8fVh0xsq7blkhBo-MA3Ha350hnGF/s1600/unnamed+%252828%2529.jpg
Timu ya mpira wa miguu Tanzania(Taifa stars)inayoshiriki michuano ya COSAFA nchini Afrika kusini,imewahudhunisha baadhi ya mashabiki wake baada ya kufungwa goli 2-0 na Madagascar ambayo inakadiriwa kuwa ni timu isiyo na uwezo wa kuichapa Taifa Stars kutokana na kiwango chake na vilabu vya nchi hiyo kuwa cha chini,mechi hiyo ilichezwa kwenye uwanja Royal Bafokeng jijini Rustenburg.
 Matokeo haya yamekuja siku chache baada kufungwa na Swaziland goli 1-0 na hivyo kuamsha hasira za mashabiki wengi wa soka nchini ambao wamekuwa wakimtupia lawama kocha wa timu hiyo Mart Nooij kuwa hayuko makini na kikosi anachochagua huku akiwaacha wachezaji wenye uwezo.
  Huku wengine wakisema ni bora timu ipewe mwalimu mzawa kuliko walimu wa nje ambao hawana mabadiliko yeyote kwa timu na wengine wakimkumbuka Marcio Maximmo kuwa alileta hamasa kwa timu ya Taifa na hivyo kuifanya iwavutie watu wengi nje na ndani ya nchi.

Wednesday, May 20, 2015

Kipindupindu chaua wakimbizi wa Burundi nchini Tanzania

Wakimbizi wa Burundi wakiwa katika kijiji cha Kagunga mkoani Kigoma,Tanzania, May 17, 2015.
Wakimbizi wa Burundi wakiwa katika kijiji cha Kagunga mkoani Kigoma,Tanzania, May 17, 2015.
Mashirika ya misaada  yalisema ugonjwa wa kipindupindu na magonjwa mengine yamelipuka kwa maelfu ya wakimbizi kutoka Burundi ambao wamefurika katika kijiji kimoja nchini Tanzania kilichopo pembeni ya ziwa Tanganyika. Ofisi ya kamishna mkuu kwa   Shirika la kuhudumia wakimbizi katika Umoja wa Mataifa iliripoti Jumapili kwamba  wakimbizi wasiopungua saba wa Burundi walifariki kutokana na kuharisha kupita kiasi.
Shirika la afya Duniani-WHO lilisema kati ya watu 500 na 2,000 wanawasili kila siku katika kijiji cha Kagunga. Wakimbizi hao wamekimbia nchini mwao kwa sababu ya khofu ya ghasia za kisiasa kufuatia uchaguzi wa mwezi Juni ambao Rais wa Burundi, Pierre Nkurunziza anataka kuwania awamu ya tatu. Uamuzi wake umeibua maandamano kwa wiki tatu katika mji mkuu wa Burundi, Bujumbura na kusababisha fujo ambapo baadhi ya maafisa wa jeshi walijaribu kufanya jaribio la mapinduzi wiki iliyopita ambalo lilishindikana ndani ya muda wa siku mbili.
Waandamanaji wanaompinga Nkurunziza, May 13, 2015.Waandamanaji wanaompinga Nkurunziza, May 13, 2015.
WHO ilisema katika taarifa yake kwamba kijiji cha kagunga kina wakazi 11,382  kutokana na ongezeko la wakimbizi  dadi ya watu na ni zaidi ya  90,000 tangu mwezi April mwaka huu. Hakuna maji salama ya kutosha kwa ajili ya kunywa.
Kulingana na taarifa ya kamati ya kimataifa ya uokozi-IRC ni kwamba kijiji cha Kagunga kimezungukwa na milima hivyo basi wakimbizi lazima wasubiri boti ambayo ni chakavu yenye takribani miaka 100 na kusafiri kwa muda wa saa tatu kuelekea kwenye bandari ya Kigoma. Boti hiyo inasafirisha abiria 600 mara mbili kwa siku na kupelekea msongamano kwa watu wa nyuma na kuwepo hali ya mazingira yasiyo safi.
IRC ilisema ilitoa huduma ya madawa kwa wakimbizi wa kagunga waliopo kwenye boti na wale waliopo kwenye kambi ya muda mkoani Kigoma. Baada ya kufika Kigoma wakimbizi wasiopungua 16,000 wamekwenda kwenye kambi nyingine ya Nyarugusu, safari inayowachukua hadi saa nne kwa kesi za wagonjwa waliopatikana na kipindupindu na kuharisha, kwa mujibu wa WHO.
Rais Pierre Nkurunziza, May 17, 2015.Rais Pierre Nkurunziza, May 17, 2015.
Wakati huo huo waandamanaji katika mji mkuu wa Burundi, Bujumbura walisema wataendelea kuandamana hadi Rais Pierre Nkurunziza aachie madaraka  mwishoni mwa muhula wake wa pili.
Katiba ya Burundi inasema rais anaweza kuchaguliwa kuongoza nchi kwa awamu mbili za muhula wa miaka mitano. Nkurunziza anasema kuwa anaweza kuwania awamu ya tatu kwa sababu bunge lilimchagua kuongoza nchi kwa awamu ya kwanza. Wapinzani wanasema awamu ya tatu inakiuka katiba na mkataba wa Amani  wa Arusha, Tanzania ambao ulimaliza vita vya wenyewe kwa wenyewe mwaka 2006.