BENJAMINKAMINYOGE.BLOGSPOT.COM

Thursday, March 28, 2013

EASTER CONFERENCE YAFANA MBEYA


Baadhi ya wanafunzi wa umoja wa wanafunzi wa kikristo Tanzania-Mkoani Mbeya wakimusikiliza Mhubiri toka Dar es salaam ndg.Jackson Mndeme kwenye mkutano unaofanyika kwenye ukumbi wa St.Mary's sekondari jijini Mbeya.

Monday, March 25, 2013

TAIFA STARS YAICHINJA MOROCCO 3-1


Timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars jana imefanikiwa kuifunga kigogo cha soka Afrika Morocco bao 3-1 kwenye mchezo uliofanyika jijini Dar es salaam jana.
Taifa Stars walipata mabao yao kipindi cha pili yakifungwa na Thomas Ulimwengu na Mbwana Samata wanaochezea TP Mazembe ya DRC,sasa Stars inashika nafasi ya pili kwenye kundi lake ikiwa na pointi 6 nyuma ya Ivory Coast wenye pointi 7,Morocco ya tatu ikiwa na pointi 2,huku Gambia ikiburuza mkia.

Saturday, March 16, 2013

WASABATO MBEYA WAJITOKEZA KUCHANGIA DAMU.


Leo ilikuwa ya matendo ya huruma duniani kwa Wasabato na kukusanyika sehemu mbalimbali duniani kwa ajili ya kutoa elimu kwa watu juu ya ubaya wa matumizi ya Madawa ya kulevya,tumbaku na pombe.
Mbali na yote hayo Wasabato wa Mbeya Mjini walichukua nafasi hiyo kuchangia damu kwenye viwanja maarufu vya Ruanda Nzovwe jijini Mbeya,mmoja wa wachangiaji damu hao bw.Leonard Msendo alionekana kufurahia huduma ya uchangiaji wa damu na kuwaomba Watanzania kujitolea damu kwa ajili ya kuwasaidia wahitataji wa damu(wagonjwa) kwani damu ni tiba ambayo inapatikana kutoka kwa binadamu.
CHANGIA DAMU OKOA MAISHA-DAMU HAIUZWI HUTOLEWA BURE NA HOSPITALI ZOTE HAPA NCHINI,UKIUZIWA DAMU TOA TAARIFA KITUO CHA POLISI,MGANGA MKUU WA HOSPITALI HUSIKA AU KITUO CHA DAMU SALAMA KILICHO JIRANI NAWE.

Thursday, March 14, 2013

PAPA MPYA ATOKA ARGENTINA


 Hatimaye lile zoezi la kumchagua Papa limekamilika katika kanisa la St.Peters Basilica huko Vatican na Muargentina Jorge Mario Bergogli kuchaguliwa kuwa Papa mpya ambaye atajulikana kwa jina la PAPA FRANCIS WA KWANZA.

Sunday, March 10, 2013

SIMBA YAAMUKA USINGIZINI LEO KWA KUICHAPA COASTAL UNION 2-1


Mabingwa watetezi wa vodacom leo wamezinduka na kuichapa Coastal Union ya Tanga bao 2-1 kwenye uwanja wa Taifa Dsm.
Simba wamepata mabao ya mwishoni mwa kipindi cha kwanza kupitia kwa Mrisho Ngasa na Haruna Chanongo huku goli la kufutia machozi la Coast likifungwa na Razaq Khalfan kipindi cha pili.
Kwa matokeo hayo Simba kafikisha pointi 34 akiwa nyuma ya Azam wenye 37,huku vinara wa ligi hiyo Yanga wakiwa na pointi 45 na Coastal Union wanabaki na pointi 31 na kufanya ligi iwe ngumu kwa Azam,Simba na Coastal Union kwa mtazamo wangu Yanga hawana ugumu sana kwani wana uhakika wa nafasi moja kati ya tatu za juu,labda itokee walewe sifa na kupoteza takribani mechi nne ndio watakuwa pabaya.

YANGA YAWAADHIBU TOTO YAO


Mabingwa wa Afrika mashariki na kati Yanga ya Dar es salaam imezidi kuisukumia kwenye shimo la kushuka daraja baada ya kuifunga bao 1-0 kwenye mchezo uliochezwa uwanja wa Taifa.
Yanga walipata goli lao kupitia kwa Nizar Khalfan dakika 78,aliyeingia kuchukua nafasi ya Tegete.

Wednesday, March 06, 2013

RAIS HUGO CHAVEZ WA VENEZUELA AFARIKI DUNIA

Rais Hugo Chavez wa Venezuela amefariki jana,Rais Chavez alikuwa akisumbuliwa na maradhi ya kansa  ambayo yamesababisha kifo chake.
  Rais huyo atakumbukwa kutokana msimamo wake wa kutoyumbishwa na  baadhi ya mataifa yenye nguvu duniani

Saturday, March 02, 2013

MANCHESTER UNITED YAMUONGEZEA MKATABA RYAN GIGGS


Mchezaji mkongwe katika ligi ya Uingereza ameongezewa mkataba wa mwaka mmoja na klabu yake ya Manchester United.
Mchezaji huyo ambaye anatarajiwa kutimiza miaka 40 hivi karibuni utakuwa ni msimu wake wa 23 ndani ya Manchester united ni mmoja kati ya wachezaji waliyoipatia mafanikio klabu hiyo ya mashetani wekundu.