BENJAMINKAMINYOGE.BLOGSPOT.COM

Sunday, April 29, 2012

SIMBA YAWATUMIA SALAMU YANGA.


Timu ya Simba ya Dar es salaam,kwa mara nyingine imeendeleza ubabe wake baada ya kuwachapa El-Ahly ya Sudan kwa mabao 3-0,kwenye mchezo wa kombe la shirikisho,uliochezwa uwanja wa taifa jijini Dar es salaam.
Simba walipata mabao yao kupitia kwa Haruna Moshi dk.67,Patrick Mafisango dk.77 na Emanuel Okwi dk.84,kwa matokeo hayo yanaipa Simba asilimia kubwa ya kuingia robo fainali ya michuano hiyo na El-Ahly kuwa na deni la bao 4-0 kwenye mchezo wa marudiano utakaochezwa Sudan kati ya mei 11 au 12,baada ya kuvaana na watani wao wa jadi Yanga ambao wanaonekana kupoteana mchezo huo utachezwa mei 5 kuhitimisha ligi kuu ya Tanzania bara.

No comments:

Post a Comment