BENJAMINKAMINYOGE.BLOGSPOT.COM

Thursday, May 21, 2015

MASHABIKI WA SOKA WAHUDHUNISHWA NA MATOKEO YA TAIFA STARS KWENYE COSAFA CUP.

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhm9LxZHCAuvoeLFUnpW6Fole9Yr6FftQj5cPUQT9nifi0CwuTdFMpVdB9U5lPJ83rxZ5_02Ls1rpPBssbygTteQ887Rx3w_-Ff0m0ATDDwHWwxQvkB8fVh0xsq7blkhBo-MA3Ha350hnGF/s1600/unnamed+%252828%2529.jpg
Timu ya mpira wa miguu Tanzania(Taifa stars)inayoshiriki michuano ya COSAFA nchini Afrika kusini,imewahudhunisha baadhi ya mashabiki wake baada ya kufungwa goli 2-0 na Madagascar ambayo inakadiriwa kuwa ni timu isiyo na uwezo wa kuichapa Taifa Stars kutokana na kiwango chake na vilabu vya nchi hiyo kuwa cha chini,mechi hiyo ilichezwa kwenye uwanja Royal Bafokeng jijini Rustenburg.
 Matokeo haya yamekuja siku chache baada kufungwa na Swaziland goli 1-0 na hivyo kuamsha hasira za mashabiki wengi wa soka nchini ambao wamekuwa wakimtupia lawama kocha wa timu hiyo Mart Nooij kuwa hayuko makini na kikosi anachochagua huku akiwaacha wachezaji wenye uwezo.
  Huku wengine wakisema ni bora timu ipewe mwalimu mzawa kuliko walimu wa nje ambao hawana mabadiliko yeyote kwa timu na wengine wakimkumbuka Marcio Maximmo kuwa alileta hamasa kwa timu ya Taifa na hivyo kuifanya iwavutie watu wengi nje na ndani ya nchi.

No comments:

Post a Comment