BENJAMINKAMINYOGE.BLOGSPOT.COM

Tuesday, June 05, 2012

POSTA YAKABIDHI T-SHIRT KWA AJILI YA WACHANGIA DAMU.


Meneja wa tawi la Posta Mbeya,Bw.Humphrey Julius(kushoto) akimkabidhi moja ya T-shirt kiongozi wa mpango wa Taifa wa Damu salama Ndg.Kundaeli Sariah,hafla hiyo imefanyika leo kwenye ofisi za mpango wa Taifa wa Damu Salama nyanda za juu kusini,jijini Mbeya na kuhudhuriwa na baadhi ya wafanyakazi wa Benki ya posta na damu salama.
Ndg.Sariah ameishukuru Benki ya Posta na kuwataka wananchi kujitokeza kwa wingi kuchangia damu na kuzitaka taasisi nyingine kujitolea vitu mbalimbali kwa ajili ya wachangia damu.
Sherehe za siku ya wachangiaji damu kitaifa itafanyika mjini Moshi na kanda ya nyanda za juu kusini itafanyika mjini Songea tar.14/06/2012,
KILA MCHANGIAJI DAMU NI SHUJAA

No comments:

Post a Comment