BENJAMINKAMINYOGE.BLOGSPOT.COM

Sunday, May 19, 2013

YANGA BINGWA TANZANIA BARA


Mabingwa wa Afrika mashariki na kati timu ya Yanga imefanikiwa kutwaa ubingwa wa Tanzania Bara kwa mara ya 24 tangu ligi ihanzishwe 1965 kwa kuwafunga watani wao wa jadi Simba kwa goli 2-0.
Magoli ya mabingwa hao yalifungwa na Didier Kavumbagu dk ya 5 huku la pili likifungwa na Hamis Kiiza dk ya 63,Yanga walitawala sehemu kubwa ya mchezo huo na kushangiliwa kwa muda wote na mashabiki wake.
Simba walikosa penati dk ya 26 iliyopigwa na Mussa Mude lakini kwa umahiri wa kipa Ally Mustapha aliweza kuidaka penati hiyo.Sasa Yanga italikilisha Taifa kwenye michezo ya klabu bingwa Afrika na mshindi wa pili Azam atashiriki kombe la shirikisho Afrika.

No comments:

Post a Comment