BENJAMINKAMINYOGE.BLOGSPOT.COM

Tuesday, January 14, 2014

KCC FC MABINGWA MAPINDUZI CUP 2014


Timu ya KCC ya Uganda leo imechukua ubingwa wa kombe la mapinduzi Zanzibar baada ya kuifunga timu ya Simba ya Dar es salaam kwa goli 1-0,kwenye mchezo wa fainali uliochezwa kwenye uwanja wa Amaan,mjini Zanzibar,goli pekee la KCC limefungwa na Herman Waswa dakika ya 20.
 Kwa matokeo hayo timu ya KCC inakuwa timu ya kwanza kutoka nje ya nchi kuchukua ubingwa huo,mashindano yalikosa msisimko baada ya timu ya Yanga kujitoa dakika za mwisho na hivyo kuwakatisha tamaa wapenzi wa soka wa Zanzibar.
KCC waliingia fainali baada ya kuwachapa Azam 3-2 na Simba waliingia fainali kwa kuwachapa URA ya Uganda 2-0.

No comments:

Post a Comment