BENJAMINKAMINYOGE.BLOGSPOT.COM

Tuesday, August 19, 2014

BIOGESI KWA MAISHA BORA

 Biogesi ni nishati itokanayo na kinyesi cha wanyama ambacho huchachuka ndani ya mtambo wa biogesi na kuweza kutumika kwa kupikia na kuwasha taa.
  FAIDA ZA BIOGESI:- .Haina moshi wala harufu mbaya
. Hupunguza madhara yanayosababishwa na moshi wa kuni au mkaa kama vile macho kuwa mekundu na kukohoa.
 .Huokoa muda Hupunguza muda wa kutafuta kuni hivyo kufanya shughuli nyingine za maendeleo.
 Mtandao huu umekutana na mtaalamu wa kutengeneza mtambo wa biogesi maeneo ya Mbinga Kigonsela bw.Linus Komba na kuelezea jinsi mtambo huu ulivyo rafiki wa mazingira,na kuwataka wananchi wa Tanzania hususani wale wanaoishi vijijini kuwasiliana naye ili aweze kuwasaidia na kuwafanya waendelee kuyatunza mazingira kwa kutokata miti,mnaweza kuwasiliana naye kwa simu yake ya mkononi +255 762 045 808,unaweza kuwasiliana naye na yuko tayari kuwafikia sehemu yeyote kwa ajili ya ushauri na matengenezo YATUNZE MAZINGIRA ILI UWAACHIE VIZAZI VIJAVYO SEHEMU NZURI YA KUISHI
Huu ndio mtambo wa biogesi ukiendelea kujengwa
Bw.Benjamin James akipata maelekezo kutoka kwa mafundi
Bw.Linus Komba akitoa maelezo kuhusu mtambo wa biogesi
Mafundi wakiendelea na kazi ya kukamilisha mtambo huo.

No comments:

Post a Comment