BENJAMINKAMINYOGE.BLOGSPOT.COM

Saturday, April 11, 2015

MLOWO UNITED YAWASHUSHIA KIPIGO SHUKRANI MWALEMBE CHA GOLI 4-1

 Mlowo United timu kongwe wilayani Mbozi imewashushia kipigo cha goli 4-1 timu ya Shukrani Mwalembe FC kwenye mchezo uliochezwa uwanja wa shule ya msingi ya Mlowo.
 Mlowo United waliokuwa wenyeji wa mchezo walitawala sehemu kubwa ya mchezo huo uliohudhuriwa na mashabiki wengi,Mlowo United walijipatia magoli yao kupitia kwa wachezaji wao mahiri,goli la kwanza likifungwa na Francis Mwigani,la pili likifungwa na mshambuliaji hatari Noah Kaminyoge huku la tatu na la nne likifungwa na nyota wa mchezo huo Derick Walulya.
                                   Wachezaji wa Mlowo United wakipiga dua kabla ya mchezo.
                               Mlowo United wakisubiri kukaguliwa na mwamuzi wa pambano hilo.  
                     Wachezaji wakisalimiana na wapinzani wao pamoja na waamuzi wa mchezo huo.
                                    Wachezaji wa Mlowo United wakichukua picha ya pamoja.
  Mpaka kipenga cha mwisho kinapulizwa Mlowo United 4,Shukrani Mwalembe 1 mara baada ya mchezo niliongea na baadhi ya mashabiki wa timu zote mbili lakini waliokuwa na furaha zaidi ni shabiki wa Mlowo United Bwana Moses Lwesya ambaye amewamwagia sifa kibao wachezaji wa Mlowo United,michuano inadhaminiwa na Mbunge wa jimbo la Mbozi Mashariki Mh.Godfrey Zambi.

No comments:

Post a Comment