BENJAMINKAMINYOGE.BLOGSPOT.COM

Wednesday, April 29, 2015

YANGA BINGWA TANZANIA KWA MARA YA 25

 Timu ya Yanga ya Dar es salaam imefanikiwa kunyakuwa taji la 25 tangu kuanziswa kwa ligi kuu ya Tanzania mwaka 1965,timu hii imefanikiwa kunyakuwa ubingwa wa ligi kuu kwa msimu wa 2014/15 kwa kuwafunga Polisi morogoro 4-1 na huku ikiwa imesaliwa na mechi mbili mkononi kati ya Ndanda FC na Azam FC.
  Yanga kabla ya kumalizia mechi zake mbili zilizobaki itakwenda Tunisia kucheza mchezo wa marudiano wa kombe la shirikisho barani Afrika kati ya Etoile Du Sahel ambapo kwenye mechi ya kwanza timu hizo zilitoka sare ya goli 1-1 jijini Dar es salaam,ikumbukwe kuwa Yanga ndio mwakilishi pekee wa Tanzania kwenye michuano ya kimataifa baada ya wawakilishi wengine kutolewa mapema.
 Kwa kufanikiwa kuchukua ubingwa wa mwaka huu Yanga itawakilisha tena Taifa mwakani,kwenye michuano ya klabu bingwa Afrika ambayo mwaka huu mwakilishi alikuwa Azam FC ambaye alitolewa na El-merreikh ya Sudan raundi ya kwanza.
Viongozi,walimu na wachezaji wa timu ya Yanga wakiwa na furaha mara baada ya ushindi.

No comments:

Post a Comment