Raia wa Nepal wakishangaa matokeo ya tetemeko jipya
                    
                
Wakati
 kukiripotiwa mvua kubwa na tetemeko kubwa na jipya nchini Nepal, Wakuu 
nchini humo wamethibitisha kuwa idadi ya watu waliokufa kutokana na 
tetemeko hilo jipya , imepanda na kufikia zaidi ya watu 60.
Wakati
 huo huo helikopta ya kikosi cha majini cha Marekani,ambayo ilikuwa 
ikifanya kazi ya kusaidia kusambaza huduma za kibinaadamu nchini Nepal, 
haijulikani.Taarifa za awali zinaeleza kuwa, ndani ya helkopta hiyo kulikuwa na watu nane,miongoni mwao, sita ni askari wa kikosi cha majini cha Marekani na askari wawili wenyeji wa jeshi la Nepal.
Maofisa wa serikali wa Marekani wamesema kwamba helkopta hiyo ilikuwa maeneo ya jirani na kijiji cha Charikot, ambacho kiliharibiwa vibaya na tetemeko la ardhi.
No comments:
Post a Comment