BENJAMINKAMINYOGE.BLOGSPOT.COM

Saturday, February 05, 2011

AZAM FC YAZIDI KUTISHA


Timu ya Azam imezidi kujiwekea mazingira mazuri ya kuwania ubingwa wa Tanzania bara baada kuwafunga Toto African mabao 3-0,mabao yao yalipachikwa dakika ya kwanza na 35 na John Boko(Adebayor) na bao la tatu lilifungwa dk ya 56 na Mrisho Ngasa baada ya kupata pasi kutoka kwa Ramadhan Chombo Ridondo,Toto African walipoteana baada ya kufungwa bao la mapema na hivyo kuwafanya Azam kumiliki mchezo huo na kufikisha 29 nyuma ya Yanga yenye pointi 31
na Simba yenye pointi 30 na hivyo kuongeza ushindani wa kuwania ubingwa,ligi hiyo itaendelea tena leo ambapo Yanga watakuwa wageni wa wanalizombe Majimaji huko Songea na AFC Arusha watawakaribisha JKT Ruvu pale Sheikh Amri Abeid mjini Arusha na kesho mabingwa watetezi Simba watashuka uwanja wa Jamhuri Dodoma kukabiliana na Polisi Dodoma.

No comments:

Post a Comment