BENJAMINKAMINYOGE.BLOGSPOT.COM

Wednesday, February 02, 2011

YANGA YAPOKEA KICHAPO CHA KWANZA.


Timu ya Yanga leo imepoteza mchezo dhidi ya Mtibwa Sugar ikiwa ni mchezo wake wa kwanza kupoteza toka ligi kuu ya msimu kuanza,kutokana na Yanga kucheza chini ya kiwango ilimulazimu kocha wake Fred Felix Minziro Kataraia(baba Isaya au Majeshi) kusimama muda wote na kuliona benchi chungu baada ya Mtibwa kutawala mchezo huo,mara baada ya mchezo huo kumalizika mashabiki wanaosadikiwa kuwa ni wa Yanga waliwafanyia vurugu wachezaji wa Yanga kwa kutoridishwa na mwenendo wa timu hiyo na kutokuwepo kwa wachezaji kama Shadrack Nsajigwa,Yaw Berko,Athman Idd kunaonekana kuwaathiri Yanga kwenye mechi ya leo bila kumsahau kocha Costadin Papic ambaye ametimkia Africa Kusini kutokana na kutokuelewana na baadhi ya viongozi wa timu hiyo ambayo pia inakabiliwa na mechi ya kombe la shirikisho Africa dhidi Dedebit ya Ethiopia kwenye mchezo wa marudiano.

No comments:

Post a Comment