BENJAMINKAMINYOGE.BLOGSPOT.COM

Monday, February 14, 2011

SIMBA YAFUTA AIBU


Mabingwa wa soka Tanzania bara wamefanikiwa kusonga mbele kwenye michuano ya klabu bingwa Afrika baada ya kuifunga Elan club de mitsoudje ya Comoro kwa jumla ya magoli 4-2,Elan ndio iliyokuwa ya kwanza kupata bao dakika ya 42 likifungwa na Madaha Mohamed,Simba walisawazisha dak 44 kupitia kwa Mbwana Samata,magoli mengine ya Simba yalifungwa na Patrick Ochan dk 47,Samata dk.56,Amri Kiemba dk.72 na goli la pili la Elan lilifungwa na Abdoulhouda Abdouleafor dk.63,nao mahasimu wao Yanga wameendelea kukumbwa na jinamizi la mechi za kimataifa baada ya kukubali kipigo cha 2-0 kutoka kwa Dedebit mchezo huo ulichezwa jana jijini Adis Ababa-Ethiopia,kwa matokeo hayo Simba itakutana na mabingwa watetezi TP Mazembe ya DRC.

No comments:

Post a Comment