BENJAMINKAMINYOGE.BLOGSPOT.COM

Saturday, September 20, 2014

UHARIBIFU WA MAZINGIRA KWA KUKATA MITI WAZIDI KUPAMBA MOTO RUKWA

Katika hali isiyokuwa ya kawaida wananchi wa kijiji cha Mtakuja njia iendayo Kapele Kasusu wilayani Sumbawanga wamekuwa wakikata misitu ili kupata maeneo ya kulima ulezi.
Wananchi hao wamekuwa wakifanya uharibifu mkubwa wa mazingira kutokana na kulima mazao ya muda mfupi ambayo faida yake ni ndogo ukilinganisha na misitu hiyo,wanachohitaji ni kupewa elimu juu ya utunzaji wa mazingira hususani ukataji miti ovyo,inabidi juhudi za haraka zichukuliwe ili kuinusuru hali hiyo ambayo inaweza kuli
fanya eneo hilo kukosa mvua kwa miaka ya baadaye.
Hizi ni baadhi ya picha ya msitu huo unaoshambuliwa kwa kasi.

Hii ni miti ambayo imeangushwa
Msitu ukiwa umekatwa na wananchi kwa ajili ya kilimo cha ulezi.

No comments:

Post a Comment