BENJAMINKAMINYOGE.BLOGSPOT.COM

Sunday, September 02, 2012

MBUYU TWITE APATA MAPOKEZI MAKUBWA.


Mchezaji wa Yanga raia wa DRC ameingia Nchini kwa mapokezi makubwa kutoka kwa mashabiki wa klabu hiyo,ambao walikuwa wakimsubiri kwa muda mrefu.
Mashabiki hao walimpatia jezi namba 4 yenye jina la Rage ambaye ni mwenyekiti wa Simba kama kumdhihaki Rage ambaye alimsajili mchezaji huyo na baadaye mchezaji huyo kurudisha fedha na kusajili Yanga kwa kitita kikubwa zaidi.
Pamoja na mapokezi makubwa aliyopata mchezaji huyo,wadau wa soka wamemtaka kufanya kile kilichomleta mashabiki huwa hawachelewi kubadilika katika mchezo wa soka na kumuona si chochote.

No comments:

Post a Comment