BENJAMINKAMINYOGE.BLOGSPOT.COM

Monday, September 22, 2014

COASTAL UNION YAIGOMEA SIMBA

Timu ya Coastal Union ya Jijini Tanga imelazimisha sare ya goli 2-2 dhidi ya Simba kwenye uwanja wa Taifa Dar es salaam,ikiwa ni mchezo wa kwanza wa ligi kuu ya Tanzania bara.
  Simba ilikianza kipindi cha kwanza kwa kasi na kujipatia magoli mawili yaliyofungwa na Shaaban Kisiga na Amisi Tambwe,mabao yalidumu hadi mapumziko.
Coastal walirudi kipindi cha pili wakiwa na machungu na kufanikiwa kusawazisha magoli yote na hivyo kuwanyima Simba ushindi ambao tayari walikuwa na uhakika nao hadi kipenga cha mwisho timu hizo zimetoka 2-2.

No comments:

Post a Comment