BENJAMINKAMINYOGE.BLOGSPOT.COM

Saturday, September 27, 2014

DAMPO JIRANI NA SHULE NI UKATILI KWA WATOTO

Eneo lililofanywa dampo
  Shule ya msingi Simike jijini Mbeya ipo katika wakati mgumu kutokana na kuwa jirani na sehemu ya kutupia takataka ambazo zinaweza kuhatarisha afya za wanafunzi hao hasa yanapotokea magonjwa ya mlipuko.
  Kumekuwa na kiasi kikubwa cha takataka ambazo zimekuwa zikitupwa bila kuondolewa kwa wakati na hivyo kufanya eneo hilo kuwa mrundikano mkubwa wa taka jirani na shule hiyo na kuwa na harufu mbaya na hewa nzito.
  Mamlaka husika zinapaswa kuangalia maeneo ya kutupia taka au kuzitoa mapema hasa maeneo ambayo yako jirani na watoto au shule ili kuwanusuru watoto na maradhi wanayoweza kuyapata,
tunaamini kwa hili linawezekana kama wahusika wakijipanga vizuri.
Lundo la taka
Huu ndio ukuta wa shule ambao uko jirani na sehemu hii ya kutupia taka.

No comments:

Post a Comment