BENJAMINKAMINYOGE.BLOGSPOT.COM

Monday, September 29, 2014

YANGA SASA YAANZA LIGI

  Baada ya kupoteza mchezo wa kwanza kwa kufungwa na Mtibwa Sugar wiki iliyopita,Yanga wamefanikiwa kupata ushindi wa goli 2-1 dhidi ya Tanzania Prison ya Mbeya kwenye mchezo uliochezwa uwanja wa Taifa Dar es salaam.
  Mchezo ulianza kwa Yanga kumiliki kipindi cha kwanza idara zote na kufanikiwa kupata goli dakika ya 34 likifungwa na Mbrazil Andre Coutinho goli hilo lilidumu hadi mapumziko.
  Kipindi cha pili Prison walirudi na kufanya mashambulizi ya kushitukiza na kufanikiwa kusawazisha bao hilo dakika ya 62,kabla ya Simon Msuva kuipatia Yanga goli la pili dakika ya 67 kwa kichwa kufuatia pasi ya Mrisho Ngassa hadi mwisho wa mchezo Yanga 2-Prison 1.
  Katika mchezo mwingine huko Chamazi Complex timu ya Kagera Sugar iliibuka na ushindi wa goli 2-0 dhidi ya JKT Ruvu.

Kikosi cha Yanga
Shabiki maarufu wa Yanga na Taifa stars anayejulikana kwa jina la Ally Yanga akiwa na wenzake uwanja wa Taifa

No comments:

Post a Comment