BENJAMINKAMINYOGE.BLOGSPOT.COM

Saturday, October 29, 2011

YANGA YAICHAPA SIMBA 1-0


Mabingwa watetezi wa Tanzania bara leo wameichapa Simba bao 1-0 kwenye mchezo wa ligi kuu uliyofanyika uwanja wa Taifa,Yanga walipata bao hilo dakika ya 72 kupitia kwa mshambuliaji wao wa kimataifa Davies Mwape baada ya walinzi wa Simba kufanya makosa,mchezo huo ulianza kwa kasi na Simba kutawala kipindi cha kwanza,Simba walipoteza nafasi kadhaa kipindi cha kwanza.
Kipindi cha pili Yanga walijipanga na kubadili mchezo na hivyo kuwafanya waibuke na ushindi huo.
Michezo mingine ya ligi hiyo imechezwa huko Mwanza kati ya Toto African na Coastal Union matokeo ni 0-0,huko Dodoma ilikuwa ni kati ya Polisi na Oljoro matokeo ni 0-0,kwa matokeo haya bado hayabadili msimamo wa ligi bado Simba inaongoza ligi ikiwa na alama 27,ikifuatiwa na Yanga yenye alama 24,Azam 21.

No comments:

Post a Comment