BENJAMINKAMINYOGE.BLOGSPOT.COM

Thursday, April 28, 2011

CHANGIA DAMU OKOA MAISHA


Waelimishaji kutoka kitengo cha taifa cha damu salama kanda ya nyanda za kusini,wakitoa elimu juu ya uchangiaji damu kwa wanafunzi wa shule ya sekondari ya Lwati wilayani Mbozi-Mbeya.Kwa kutumia blog hii nawapongeza wafanyakazi wa kitengo husika na wale wote wenye moyo wa kujitolea kwa ajili ya wahitaji-Amen.

ELIMU NA KAZI


Wanafunzi wa shule ya sekondari Lwati wilayani Mbozi,wakiwa kwenye shamba la migomba wakifanya kazi kwenye moja ya mashamba ya shule hiyo.

Sunday, April 24, 2011

PASAKA NJEMA


Bw.Benjamin J.Kaminyoge,anawatakia wakristo wote ulimwenguni heri ya sikukuu ya Pasaka,kwa kutumia sikukuu hii tusameane makosa yetu na kuwa na upendo.

MITAMBO YA KUPIMIA MITA ZA MAJI


Mdau wetu akiwa ametembelea mitambo maalumu inayotumika kupima mita za maji zenye matatizo huko Mbeya.

Sunday, April 17, 2011

MANCHESTER YAKABWA KOO


Manchester united jana imefungwa bao 1-0 na mahasimu wao Manchester City,katika michuano ya FA CUP,michuano hiyo imekuwa na msisimko mkubwa kwa timu ndogo kuzitoa jasho timu kubwa.

Saturday, April 16, 2011

AJALI MBAYA YATOKEA ARUSHA

Poleni ndugu zetu wa Arusha kwa msiba uliowapata  kutokana na ajali ya iliyohusisha basi la kampuni ya ngorika na basi dogo aina ya hiace na kusababisha vifo vya watu na wengine kujeruhiwa.

Thursday, April 14, 2011

SHITAMBALA AISALITI CHADEMA

Aliyekuwa mwenyekiti wa chama cha maendeleo mkoa wa Mbeya ameamua kuhama chama chake na kujiunga na chama cha mapinduzi (CCM,uamuzi wake umepokelewa kwa hisia tofauti na wananchi mkoani Mbeya

Monday, April 11, 2011

YANGA BINGWA


Timu ya Yanga imetwaa ubingwa wa Tanzania bara baada ya kuifunga Toto African kwa jumla ya mabao 3-0,magoli ya Yanga yalifungwa na Nurdin Bakar na Davies Mwape yote kipindi cha pili,hivyo kuifanya Yanga kufikisha pointi 49 sawa na mahasimu wao Simba lakini wanakuwa mabingwa kwa tofauti ya magoli,Simba waliifunga Majimaji ya Songea bao 4-1.

Saturday, April 09, 2011

STENDI KUU MBEYA


Ukarabati unaoendelea ndani ya kituo cha mabasi Mbeya umesababisha lango la kutokea kufungwa kwa muda na kusababisha gari zote kuingia na kutokea mlango mmoja,imekuwa ni taabu hasa asubuhi zinapoondoka gari za mikoani.

Wanafunzi wakipata elimu kwenye ukumbi wa mikutano chini ya bwana Morgan Seben.

Wanafunzi wa Swaya sekondari wakipata maelezo kutoka kwa mtaalamu wa kitengo cha damu Mbeya bwana Morgan Seben walipotembelea kitengo hicho.


ZIARA YA WANAFUNZI WA SEKONDARI YA SWAYA-MBEYA.


Wanafunzi wa Swaya walipotembelea benki ya damu kwa ajili ya mafunzo juu ya mfumo wa damu.

Eneo la Kabwe Mbeya.

MVUA NDANI YA MBEYA


Baadhi ya mitaa jijini Mbeya imekuwa ni kero kutokana na mvua inayoendelea kunyesha na kusababisha barabara kujaa maji kutokana na mashimo kama inavyoonekana moja ya barabara eneo la Soweto.

YANGA YAKARIBIA UBINGWA


Timu ya Yanga imeamusha matumaini ya kutwaa ubingwa msimu huu baada ya kuwachapa African Lyon kwa jumla ya bao 3-0 na kufikisha pointi 46 na kubakiwa na mechi moja sawa na mahasimu wao Simba ambayo nayo imebakiza mchezo mmoja dhidi ya Majimaji.

Wednesday, April 06, 2011

SIMBA ALMANUSRA KWA RUVU JKT


Mabingwa watetezi wa Tanzania bara Simba leo wamenusurika kichapo kutoka kwa maafande wa JKT RUVU baada ya kusawazisha bao kwa njia ya penati iliyofungwa na Emanuel Okwi,ilikuwa ni JKT RUVU iliyokuwa ya kwanza kujipatia bao la kuongoza kipindi cha kwanza lililowekwa kimiani na Hussein Bunu na kudumu hadi mapumziko,Simba ambao leo walionekana kubanwa vilivyo na wapinzani wao,mwamuzi wa mchezo huo alishindwa kuumudu mchezo huo na kuwatoa nje wachezaji wa JKT akiwemo Shabaan Dihile na George Minja,ligi hiyo itaendelea tena kesho kati ya Yanga dhidi ya African Lyon,Yanga wanahitaji ushindi ili kujiwekea mazingira mazuri ya kunyakua ubingwa.

VODACOM WABADILISHA RANGI YAO.


Linaloonekana ni jengo la Vodashop Mbeya,likiwa linaendelea kupigwa rangi tofauti na ile iliyozoeleka na wengi ya bluu sijui na jina litakuwaje?umekuwepo mchezo wa kubadili majina na rangi kwa baadhi ya makampuni ya simu kama vile mobitel wakaitwa Buzy na sasa tigo na Celtel wakaitwa Zain na sasa Airtel.