BENJAMINKAMINYOGE.BLOGSPOT.COM

Tuesday, March 20, 2012

FABRICE MUAMBA SASA ANAENDELEA VIZURI


Mchezaji wa Bolton ya Uingereza Fabrice Muamba sasa anaendelea vizuri baada ya kuweza kupumua mwenyewe bila msaada wa mashine na ameweza pia kuwatambua baadhi ya watu waliomtembelea hospitali leo.
Muamba alianguka ghafla kwenye mchezo wa kombe la FA kwenye uwanja wa White hart lane,wakati timu yake ikicheza na Tottenham Hotspur,mchezo huo ilibidi huahirishwe kutokana na hali ya Muamba kuwa mbaya,huku matokeo yakiwa 1-1 na kukimbizwa hospital ya Heart attack Centre jijini London.
Muamba alijiunga na Bolton 2008 akitokea Birmingham City kwa ada ya paundi (£) milion 5.
Muamba alizaliwa DRC miaka 23 iliyopita,na alipokuwa na umri wa miaka 11 alimufuata baba yake jijini London ambako alikuwa akifanya kazi.
Tukio hili limewakumbusha wanasoka na wapenzi wa soka mchezaji wa zamani wa Cameroun Mark Vivien Foe ambaye naye alianguka uwanjani na kupoteza maisha.

No comments:

Post a Comment