BENJAMINKAMINYOGE.BLOGSPOT.COM

Wednesday, July 25, 2012

AZAM FC YAICHAKAZA SIMBA 3-1 NA KUTINGA NUSU FAINALI


Simba imechezea kichapo cha aibu kutoka kwa Azam FC cha mabao 3-1,kwenye mchezo wa robo fainali kombe la Kagame.
Azam FC walipata goli la kwanza dk.17 likifungwa na John Boko ambaye alikuwa mwiba kwenye ngome ya Simba kwa kupachika mabao yote,dk ya 46 aliipatia bao la pili na Simba walipata bao la kufutia machozi kupitia kwa Shomari Kapombe dk.53 kwa juhudi zake binafsi,kama vile haitoshi John Boko alitupia tena kimiani bao la 3 na kuwafanya Simba wachanganyikiwe zaidi.
Mchezo mwingine uliochezwa mchana timu ya Vita Club ya DRC iliichapa Atletco ya Burundi 2-1,sasa Azam itakutana Vita Club huku Yanga wakicheza na APR ya Rwanda nusu fainali tarehe 26.

No comments:

Post a Comment