BENJAMINKAMINYOGE.BLOGSPOT.COM

Tuesday, July 24, 2012

YANGA YAINGIA NUSU FAINALI KAGAME CUP.


Mabingwa watetezi wa michuano ya kombe la Kagame Yanga ya Dar es salaam,wamefanikiwa kuingia nusu fainali baada ya kuwatoa timu ngumu ya Mafunzo ya Zanzibar kwa mikwaju ya penati 5-3.
Hadi dakika 90 zikimalizika matokeo yalikuwa 1-1,Mafunzo walikuwa wa kwanza kupata goli dakika ya 35 likifungwa na Othman Mmanga kwa njia ya kichwa na Yanga walisawazisha bao dakika ya 47 kupitia kwa Said Bahanuzi.
Katika mchezo mwingine wa nusu fainali APR ya Rwanda iliwachapa URA ya Uganda bao 2-1,michezo mingine ya nusu fainali itachezwa kati ya Azam na Simba,Atletco ya Burundi na Vita SC ya DRC.

No comments:

Post a Comment