BENJAMINKAMINYOGE.BLOGSPOT.COM

Thursday, July 26, 2012

YANGA NA AZAM FC KUCHEZA FAINALI KOMBE LA KAGAME


Timu ya Yanga na Azam FC zimefanikiwa kuingia fainali ya kombe la Kagame baada ya kushinda michezo yao ya nusu fainali leo iliyochezwa uwanja wa taifa jijini Dar es salaam.
Azam wamefanikiwa kuingia fainali baada ya kuwachapa Vita Club ya DRC goli 2-1,kupitia kwa John Bocco na Mrisho Ngasa kwenye mechi iliyochezwa mchana,kwenye mchezo wa pili Yanga ililazimika kucheza kwa dk.120 na hatimaye kupata bao pekee dk.99 kupitia kwa Hamis Kiiza aliyezifumania nyavu za wapinzani wao.
Kwa matokeo hayo timu hizo zitakutana kwenye fainali.

No comments:

Post a Comment