BENJAMINKAMINYOGE.BLOGSPOT.COM

Sunday, July 08, 2012

TENKI LA MAJI LAMWAGA MAJI MENGI SIMIKE MBEYA.


Hii inasikitisha sana kuona mamlaka husika ikiwa imekaa kimya kwa muda mrefu,kutokana na upotevu wa maelfu ya lita za maji kupotea bila kutumika huku maji hayo yakitiririka na kuingia mto Mabatini kutoka tenki la maji la mtaa wa Simike,jijini Mbeya na kusababisha baadhi ya wakazi wa eneo kukosa maji kwa muda kutokana na tatizo hilo.
Mamlaka husika inaombwa kushughulikia tatizo hili ambalo limekuwa kero kwa baadhi ya wakazi wa mtaa huo kutokana na maji hayo yanayovuja kwa wingi kupita milangoni mwao.

No comments:

Post a Comment