BENJAMINKAMINYOGE.BLOGSPOT.COM

Saturday, March 16, 2013

WASABATO MBEYA WAJITOKEZA KUCHANGIA DAMU.


Leo ilikuwa ya matendo ya huruma duniani kwa Wasabato na kukusanyika sehemu mbalimbali duniani kwa ajili ya kutoa elimu kwa watu juu ya ubaya wa matumizi ya Madawa ya kulevya,tumbaku na pombe.
Mbali na yote hayo Wasabato wa Mbeya Mjini walichukua nafasi hiyo kuchangia damu kwenye viwanja maarufu vya Ruanda Nzovwe jijini Mbeya,mmoja wa wachangiaji damu hao bw.Leonard Msendo alionekana kufurahia huduma ya uchangiaji wa damu na kuwaomba Watanzania kujitolea damu kwa ajili ya kuwasaidia wahitataji wa damu(wagonjwa) kwani damu ni tiba ambayo inapatikana kutoka kwa binadamu.
CHANGIA DAMU OKOA MAISHA-DAMU HAIUZWI HUTOLEWA BURE NA HOSPITALI ZOTE HAPA NCHINI,UKIUZIWA DAMU TOA TAARIFA KITUO CHA POLISI,MGANGA MKUU WA HOSPITALI HUSIKA AU KITUO CHA DAMU SALAMA KILICHO JIRANI NAWE.

No comments:

Post a Comment