BENJAMINKAMINYOGE.BLOGSPOT.COM

Sunday, March 10, 2013

SIMBA YAAMUKA USINGIZINI LEO KWA KUICHAPA COASTAL UNION 2-1


Mabingwa watetezi wa vodacom leo wamezinduka na kuichapa Coastal Union ya Tanga bao 2-1 kwenye uwanja wa Taifa Dsm.
Simba wamepata mabao ya mwishoni mwa kipindi cha kwanza kupitia kwa Mrisho Ngasa na Haruna Chanongo huku goli la kufutia machozi la Coast likifungwa na Razaq Khalfan kipindi cha pili.
Kwa matokeo hayo Simba kafikisha pointi 34 akiwa nyuma ya Azam wenye 37,huku vinara wa ligi hiyo Yanga wakiwa na pointi 45 na Coastal Union wanabaki na pointi 31 na kufanya ligi iwe ngumu kwa Azam,Simba na Coastal Union kwa mtazamo wangu Yanga hawana ugumu sana kwani wana uhakika wa nafasi moja kati ya tatu za juu,labda itokee walewe sifa na kupoteza takribani mechi nne ndio watakuwa pabaya.

No comments:

Post a Comment