Sunday, April 24, 2011
Sunday, April 17, 2011
Saturday, April 16, 2011
AJALI MBAYA YATOKEA ARUSHA
Poleni ndugu zetu wa Arusha kwa msiba uliowapata kutokana na ajali ya iliyohusisha basi la kampuni ya ngorika na basi dogo aina ya hiace na kusababisha vifo vya watu na wengine kujeruhiwa.
Thursday, April 14, 2011
SHITAMBALA AISALITI CHADEMA
Aliyekuwa mwenyekiti wa chama cha maendeleo mkoa wa Mbeya ameamua kuhama chama chake na kujiunga na chama cha mapinduzi (CCM,uamuzi wake umepokelewa kwa hisia tofauti na wananchi mkoani Mbeya
Monday, April 11, 2011
YANGA BINGWA
Timu ya Yanga imetwaa ubingwa wa Tanzania bara baada ya kuifunga Toto African kwa jumla ya mabao 3-0,magoli ya Yanga yalifungwa na Nurdin Bakar na Davies Mwape yote kipindi cha pili,hivyo kuifanya Yanga kufikisha pointi 49 sawa na mahasimu wao Simba lakini wanakuwa mabingwa kwa tofauti ya magoli,Simba waliifunga Majimaji ya Songea bao 4-1.
Saturday, April 09, 2011
Wednesday, April 06, 2011
SIMBA ALMANUSRA KWA RUVU JKT
Mabingwa watetezi wa Tanzania bara Simba leo wamenusurika kichapo kutoka kwa maafande wa JKT RUVU baada ya kusawazisha bao kwa njia ya penati iliyofungwa na Emanuel Okwi,ilikuwa ni JKT RUVU iliyokuwa ya kwanza kujipatia bao la kuongoza kipindi cha kwanza lililowekwa kimiani na Hussein Bunu na kudumu hadi mapumziko,Simba ambao leo walionekana kubanwa vilivyo na wapinzani wao,mwamuzi wa mchezo huo alishindwa kuumudu mchezo huo na kuwatoa nje wachezaji wa JKT akiwemo Shabaan Dihile na George Minja,ligi hiyo itaendelea tena kesho kati ya Yanga dhidi ya African Lyon,Yanga wanahitaji ushindi ili kujiwekea mazingira mazuri ya kunyakua ubingwa.
VODACOM WABADILISHA RANGI YAO.
Linaloonekana ni jengo la Vodashop Mbeya,likiwa linaendelea kupigwa rangi tofauti na ile iliyozoeleka na wengi ya bluu sijui na jina litakuwaje?umekuwepo mchezo wa kubadili majina na rangi kwa baadhi ya makampuni ya simu kama vile mobitel wakaitwa Buzy na sasa tigo na Celtel wakaitwa Zain na sasa Airtel.
Friday, March 11, 2011
Thursday, March 10, 2011
SIMBA YAZIKALIA AZAM NA YANGA
Timu ya Simba ambao ni mabingwa watetezi wa ligi kuu ya Tanzania bara jana walifanikiwa kuongoza ligi kwa kuifunga Ruvu shooting ya Pwani kwa bao 1-0 dakika ya 87 likifungwa na mchezaji Ally Ahmed 'Shiboli' aliyeingia dakika ya 79 kuchukua nafasi ya Mbwana Samata aliyebanwa vilivyo na mabeki wa Ruvu,sasa Simba imefikisha pointi 41 baada kucheza michezo 18,ikifuatiwa na Yanga yenye pointi 39 huku Azam ikiwa na pointi 37
Tuesday, March 08, 2011
Monday, March 07, 2011
Friday, March 04, 2011
CRDB WAFUNGUA TAWI JIPYA MWANJELWA- MBEYA
Waziri wa maji,Profesa Mark Mwandosya (watatu kushoto) akikata utepe kufungua tawi jipya la benki ya CRDB eneo la Mwanjelwa jijini MBEYA,kushoto ni mwenyekiti wa bodi ya benki hiyo bw.Martin Mmari,kulia ni mama Mwandosya,kufunguliwa kwa tawi hilo kutawasaidia wakazi wa jiji la Mbeya ambao walikuwa wakipanga foleni kwenye tawi pekee lililokuwa mjini Mbeya.
Wednesday, March 02, 2011
GADAFFI ANG'ANG'ANIA MADARAKANI
- Kiongozi wa Libya Muamar Gadaffi ameendelea kung'ang'ania madaraka,licha ya kuwepo kwa maandamano ya kumtaka kuachia madaraka hayo ya urais ambayo ameshikilia kwa zaidi ya miaka arobaini,amekuwa ahamini kinachotokea kwenye taifa lake kutokana na jinsi utawala wake kutowapa uhuru waandishi wa habari na redio.
Tuesday, March 01, 2011
Subscribe to:
Posts (Atom)