BENJAMINKAMINYOGE.BLOGSPOT.COM

Saturday, February 26, 2011


Wakazi wa Gongo la mboto wakishangaa bomu lililokita chini siku chache baada ya milipuko eneo hilo.

Thursday, February 17, 2011

MABOMU GONGO LA MBOTO


Madaktari wa hospitali ya Amana jijini Dar es salaam,wakimuhudumia mmoja wa waathirika wa mabomu hayo ambayo yalilipuka kutoka kwenye ghala la kutunzia silaha la JWTZ.

BREAKING NEWS!!!


Kuna mlipuko mkubwa unaendelea usiku huu eneo la Gongo la mboto jijini Dar es salaam,inasadikiwa ni kutoka kambi ya jeshi la wananchi Tanzania (JWTZ) na hivyo kuwafanya wakazi na majirani wa eneo hilo kuyakimbia makazi yao na kuelekea katikati ya jiji na kusababisha msongamano mkubwa kwenye baadhi ya barabara.
Tutaendelea kuwapa taarifa zaidi kutoka mfuatiliaji wa taarifa hii.

Monday, February 14, 2011

SIMBA YAFUTA AIBU


Mabingwa wa soka Tanzania bara wamefanikiwa kusonga mbele kwenye michuano ya klabu bingwa Afrika baada ya kuifunga Elan club de mitsoudje ya Comoro kwa jumla ya magoli 4-2,Elan ndio iliyokuwa ya kwanza kupata bao dakika ya 42 likifungwa na Madaha Mohamed,Simba walisawazisha dak 44 kupitia kwa Mbwana Samata,magoli mengine ya Simba yalifungwa na Patrick Ochan dk 47,Samata dk.56,Amri Kiemba dk.72 na goli la pili la Elan lilifungwa na Abdoulhouda Abdouleafor dk.63,nao mahasimu wao Yanga wameendelea kukumbwa na jinamizi la mechi za kimataifa baada ya kukubali kipigo cha 2-0 kutoka kwa Dedebit mchezo huo ulichezwa jana jijini Adis Ababa-Ethiopia,kwa matokeo hayo Simba itakutana na mabingwa watetezi TP Mazembe ya DRC.

Sunday, February 13, 2011

BOMOA BOMOA


Jengo jipya lililoko Mbeya eneo la Mafiat,likionekana limebomolewa upande kutokana na mmiliki wake kushindwa kuzingatia umbali kati ya barabara na nyumba.

Tuesday, February 08, 2011

Saturday, February 05, 2011

AZAM FC YAZIDI KUTISHA


Timu ya Azam imezidi kujiwekea mazingira mazuri ya kuwania ubingwa wa Tanzania bara baada kuwafunga Toto African mabao 3-0,mabao yao yalipachikwa dakika ya kwanza na 35 na John Boko(Adebayor) na bao la tatu lilifungwa dk ya 56 na Mrisho Ngasa baada ya kupata pasi kutoka kwa Ramadhan Chombo Ridondo,Toto African walipoteana baada ya kufungwa bao la mapema na hivyo kuwafanya Azam kumiliki mchezo huo na kufikisha 29 nyuma ya Yanga yenye pointi 31
na Simba yenye pointi 30 na hivyo kuongeza ushindani wa kuwania ubingwa,ligi hiyo itaendelea tena leo ambapo Yanga watakuwa wageni wa wanalizombe Majimaji huko Songea na AFC Arusha watawakaribisha JKT Ruvu pale Sheikh Amri Abeid mjini Arusha na kesho mabingwa watetezi Simba watashuka uwanja wa Jamhuri Dodoma kukabiliana na Polisi Dodoma.

Wednesday, February 02, 2011

YANGA YAPOKEA KICHAPO CHA KWANZA.


Timu ya Yanga leo imepoteza mchezo dhidi ya Mtibwa Sugar ikiwa ni mchezo wake wa kwanza kupoteza toka ligi kuu ya msimu kuanza,kutokana na Yanga kucheza chini ya kiwango ilimulazimu kocha wake Fred Felix Minziro Kataraia(baba Isaya au Majeshi) kusimama muda wote na kuliona benchi chungu baada ya Mtibwa kutawala mchezo huo,mara baada ya mchezo huo kumalizika mashabiki wanaosadikiwa kuwa ni wa Yanga waliwafanyia vurugu wachezaji wa Yanga kwa kutoridishwa na mwenendo wa timu hiyo na kutokuwepo kwa wachezaji kama Shadrack Nsajigwa,Yaw Berko,Athman Idd kunaonekana kuwaathiri Yanga kwenye mechi ya leo bila kumsahau kocha Costadin Papic ambaye ametimkia Africa Kusini kutokana na kutokuelewana na baadhi ya viongozi wa timu hiyo ambayo pia inakabiliwa na mechi ya kombe la shirikisho Africa dhidi Dedebit ya Ethiopia kwenye mchezo wa marudiano.

Monday, January 31, 2011

SIMBA KAMA PAKA


Mabingwa wa soka wa Tanzania bara wameshindwa kudhiirisha umwamba wao kwenye mechi za kimataifa baada ya kulazimishwa suluhu na wenyeji wao ELAN CLUB DE MITSOUDJE ya Comoro na hivyo kuwafanya wapinzani wao kuhitaji sare ya magoli ili waweze kusonga mbele kwenye mchezo wa marudiano utakaofanyika wiki mbili zijazo jijini Dar,nao mahasimu wao Yanga walishindwa kuutumia vyema uwanja wa taifa baada ya kulazimishwa sare ya mabao 4-4 na Dedebit ya Ethiopia na hivyo kujiweka katika mazingira magumu.

Friday, January 28, 2011

LILONDO


Wakina mama wa eneo la Lilondo wakifanya biashara ya ndizi kwenye mabasi yanayopita eneo hilo,mabasi yanayofanya safari kati ya Songea,Iringa,Mbeya na Dar es salaam.

KITUO CHA MABASI SONGEA.


Wafanyabiashara wa eneo la stendi kuu Songea,wakifanya biashara za vyakula katika eneo lisiloridhisha kwa afya za walaji na usalama kutokana na majiko kuwa jirani na mabasi.

PERAMIHO MISSION


Kanisa kongwe la Roman Catholic la Peramiho.

PERAMIHO HOSPITAL



PERAMIHO SONGEA


Hospital ya Peramiho ni moja ya hospital kubwa zinazotoa huduma bora za kiafya hususan kwa wakazi wa kanda za nyanda za juu kusini na maeneo mengine.

Sunday, January 23, 2011

IHANDA MBOZI


Mabaki ya gari aina ya Coaster,ambayo ilichomwa moto na wananchi wenye hasira baada ya kumgonga mkazi wa kijiji cha Ihanda na kusababisha kifo chake.

Thursday, January 20, 2011



MAMBO YA BAJAJ


Usafiri wa Bajaj umekuwa wa kawaida wa kawaida kwa baadhi ya sehemu hapa nchini,leo imetokea ajali ya Bajaj jijini Mbeya eneo la Meta baada ya Bajaj kuacha njia na kuingia kwenye mtaro kutokana na mwendo wa kasi na hivyo kusababisha dereva kushindwa kuimudu kwenye kona,wanaonekana wananchi wenye huruma wakiitoa bajaj hiyo,dereva na abiria wake walinusurika kwenye ajali hiyo.

AJALI


Daladala inayofanya safari kati ya Mbalizi na Mwanjelwa ikiwa imeigonga gari ndogo eneo la Kadege,kwa bahati nzuri hakuna majeruhi kwenye ajali hii iliyotokea jioni hii.

Wednesday, January 19, 2011

HOLIDAY HILL HOTEL-MBEYA


Moja ya hotel za kisasa jijini Mbeya,Holiday hill hotel iko jirani na kanisa la Efatha,ina huduma za internet,chumba cha mikutana,maegesho ya magari na mambo mengi.

Friday, January 14, 2011

TUCHANGIE DAMU KUWASAIDIA WAGONJWA.


Dr.MATHEO KINEMO wa mpango wa taifa wa damu salama akitoa elimu juu ya kuchangia damu kwa wanafunzi wa shule ya sekondari ya Meta iliyoko jijini Mbeya,mdau wa globu hii anawapongeza na kuwashukuru wananchi wote wenye moyo wa huruma na kuchangia damu kwa ajili ya wagonjwa wenye upungufu wa damu wakiwemo wajawazito,watoto chini ya miaka mitano na waanga wa ajali mbali mbali kama vile ajali za barabarani,moto na kadhalika.

Monday, January 10, 2011


Gari ya zimamoto likiwa eneo la tukio.

WELL DONE ZIMAMOTO


Kikosi cha zimamoto mkoani Mbeya kimefanikiwa kuinusuru hotel ya Calm inn,iliyokuwa imeshika moto,wanaonekana askari wa zimamoto wakiudhibiti moto huo.

Sunday, January 09, 2011

RC PAROKIA YA RUANDA-ILOMBA MBEYA.


Waumini wakijianda kuingia kanisani kwa ajili ya kumuomba na kumshukuru Mwenyezi MUNGU kwa mema mengi aliyotutendea.

ENZI ZA MWALIMU


Gari aina ya LEYLAND ALBION ambazo miaka ya 70 ndio zilikuwa kwenye chati kama ilivyo SCANIA leo,likiwa na mashine za kuchimbia visima vya maji.

Saturday, January 08, 2011

HAUZAN EDWARD


Mfanyakazi wa mamlaka ya maji safi na taka mkoa wa Mbeya akijitolea damu kwa ajili ya kuwasaidia wagonjwa.

MAZINGIRA


Mfanyakazi anayeshulika na utunzaji wa mazingira kwenye ya sekondari ya Pandahill,akifyeka nyasi kwa kutumia mashine aina ya SHIKUNDAIWA

NELLAS KITUNDU


Mfanyakazi wa mamlaka ya maji Mbeya,akipumzika baada kushiriki zoezi la kuchangia damu.

Friday, January 07, 2011

Tuesday, January 04, 2011

SOKO MATOLA-MBEYA


Wauzaji wa matunda, mboga za majani na viungo wakiwa wamepanga bidhaa zao mbele ya maduka na kuzipanga chini,tunawaomba viongozi wa soko na halmashauri ya jiji kuwawekea mazingira mazuri wajasiliamali hawa kwa kuwaweka eneo zuri kwa afya za walaji na wao pia.

Monday, January 03, 2011

IGURUSI MBEYA


Wakazi wa kijiji cha Igurusi,mkoani Mbeya wakiwa kwenye pilikapilika za kila siku kwa ajili ya kujipatia riziki,kijiji hiki ni maarufu kwa biashara ya mchele.

Saturday, January 01, 2011

HAPPY NEW YEAR 2011


Nights are dark but days are light,wish your life will always be bright.So my dear dont get fear coz,God gift us a "brand new year"
*HAPPY NEW YEAR*

Monday, December 27, 2010

YANGA YAILAZA AFC LEOPARD


Yanga imeifunga AFC Leopard kutoka Kenya bao 1-0,kwenye mchezo wa kirafiki uliochechwa kwenye uwanja wa uhuru jijini Dar es salaam,bao hilo lilifungwa na kiungo Kigi Makasi dakika ya 46 kwa shuti kali baada ya kumalizia pasi ya Jerry Tegete,mara baada kumalizika mchezo huo kocha mkuu wa AFC Noah Wanyama alisema mchezo utamsaidia kufanya marekebisho kadhaa kwenye kikosi chake,naye kocha wa Yanga Kosta Papic alisema mchezo huo umemsaidia kujua mapungufu kwenye kikosi chake,Yanga wanakabiliwa na michuano ya kimataifa kombb la shirikisho na imepangwa kuanza Dedebit ya Ethiopia na kama kushinda itakutana na wababe wa Simba kutoka Misri Haras el Hadood katika raundi ya pili.

CHRISTMASS


Bw.Benjamin Kaminyoge anawapongeza wakristo na watanzania wote kwa kusherekea sikukuu ya christmass kwa amani na utulivu

MAMBO YA BARABARANI


Gari ya mizigo aina ya Volvo FH 12,Likiwa limeacha njia na kusababisha magari mengine kushindwa kupita hii imetokea asubuhi ya leo eneo la Songwe darajani kwenye barabara kuu ya Mbeya-Tunduma.

Saturday, December 25, 2010

Wednesday, December 22, 2010

Mchana mwema.


Mtoto RASMONSEN BEN KAMINYOGE akipata chakula cha mchana nyumbani kwao Mlowo Mbozi.

Consolata seminary-Mafinga


Nimeipenda sana hii mbinu ya kutumia matenki yaliyokuwa kwenye magari kwa ajili ya kuhifadhia maji badala ya kuuza kama vyuma chakavu,tanki moja linaweza kuchukua kama lita 21,000


Likizo fupi


Mwanafunzi wa chuo kikuu cha Sebastian Kolowa-Lushoto Tanga,bw.FIKA-ELLY-JAMES akitafakari juu ya masomo.

MBEYA


Hivi ndivyo linavyoonekana soko la uhindini jijini Mbeya mara baada ya kuungua majuma kadhaa yaliyopita na kusababisha hasara kubwa kwa baadhi ya wafanyabiashara wa soko hilo.

MAANDALIZI YA SIKUKUU


Wakazi wa jiji la Mbeya wakiwa kwenye pilika pilika za maandalizi ya sikukuu ya Christmass na mwaka mpya eneo la Mwanjelwa ambalo ni maarufu jijini hapa kwa biashara za nguo za dukani na mitumba.


Monday, December 20, 2010

MBOZI


Madiwani wa wilaya ya Mbozi wameapishwa rasmi tarehe 17/12/10,na madiwani hao wamemchagua bwana Minga kuwa mwenyekiti wa halmashauri hiyo,nilifanikiwa kuongea na mmoja wa madiwani hao mheshimiwa Sunday Shullah diwani wa Ichesa,alisema sasa wanaanza majukumu yao kwa nguvu kwa ajili ya kuleta mabadiliko na maendeleo ndani ya wilaya hiyo ambayo kuna matatizo ya maji,shule na vituo vya afya na mengine. 


Sunday, December 19, 2010

SANAA


Benny signs and arts ni wataalam wa kuandika maandishi kwenye mabango,t.shirt,magari,sticker,kuta na michoro mbalimbali,wasiliana nao kwa simu 0715-539168,barua pepe bennsigns@yahoo.com

Saturday, December 18, 2010

MISITU NI UHAI


Utunzaji wa misitu ni muhimu kwa taifa lolote linalohitaji maendeleo,faida zake ni nyingi sana,lakini watanzania wengi faida wanayoelewa ni matumizi ya kuni na mkaa,kila mmoja wetu amuelimishe mwenzake juu ya umuhimu wa misitu-KATA MTI PANDA MTI.

Njombe


Ben James wa kushoto akiwa na wanafunzi wa shule ya sekondari ya Njombe alipotembelea shule hiyo dec 11

NJOMBE SECONDARY SCHOOL


Wanafunzi wa Njombe sec kidato cha sita wanaonekana wakipendeza siku ya mahafali yao ya umoja wa kikristo yaliyofanyika lutheran centre Njombe.

Thursday, December 16, 2010

FAMILY SEPARATION


0ne thing that children of divorce have to deal with,particularly if the divorce occurs early in their lives.....They develop emotional attachments with people who sometimes disappear from their lives.

MAKAMBAKO


Hii ni sehemu ya mji wa Makambako ambayo ni njia panda ya Songea,Dar-es-salaam,Mbeya.mji huu ni wa kibiashara zaidi,wawekezaji kazi kwenu.