BENJAMINKAMINYOGE.BLOGSPOT.COM

Saturday, September 10, 2011

MV.SPICE ISLANDER YAZAMA KASKAZINI UNGUJA NA KUSABABISHA MSIBA MKUBWA






Meli ijulikanayo kwa jina la Mv. SPICE ISLANDER inayofanya safari zake kati ya Pemba na Unguja,jana usiku ilipata dhoruba na kupinduka hatimaye kuzama na kusababisha zaidi ya watu 100 kupoteza maisha,japokuwa jitihada kuokoa watu abiria zinaendelea na mpaka sasa wameshaokolewa zaidi ya abiria 150 wakiwa hai na shughuli hiyo inaendelea.

Rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa baraza la mapinduzi  Dr. Ally M.Shein  na makamu wa rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharrif Hamad wakiwa na huzuni kubwa walipotembelea eneo la ufukwe wa Nungwi kuangalia ajali hiyo ya meli.


Askari wa vikosi mbalimbali wanashiriki katika uokoaji wa abiria na hapa wanaonekana wakiwa wamembeba bi.Mariam Mohamed Murad kutoka Tanga aliyenusurika kwenye ajali hiyo ya meli


No comments:

Post a Comment