BENJAMINKAMINYOGE.BLOGSPOT.COM

Saturday, September 03, 2011

TAIFA STARS YALAZIMISHWA SARE NYUMBANI

Timu ya taifa ya Tanzania (Taifa Stars) leo imelazimishwa sare ya bao 1-1 na timu ya Taifa ya Algeria kwenye mchezo wa kuwania tiketi ya kushiriki michuano ya kuwania kombe la mataifa ya Afrika yatakayofanyika mwakani huko Equatarial Guinea na Gabon,kwa matokeo haya ya leo yamezidi kupoteza matumaini ya kushiriki michuano hiyo kwa timu ya Taifa ambayo kwa mara ya mwisho ilishiriki michuano hiyo mwaka 1980
  Taifa stars walipata bao dakika ya 24 kupitia kwa Mbwana Samata baada ya kupokea pasi nzuri kutoka kwa Nizar Khalfan,lakini kisicho riziki hakiliki Algeria walisawazisha goli hilo na kuonyesha kandanda safi kipindi cha pili kama vile walikuwa wakisoma mchezo kipindi cha kwanza.
 Taifa Stars wakiwatumia wachezaji wengi wanaocheza nje ya nchi waliweza kucheza kandanda safi na la kuvutia tatizo likiwa ni umaliziaji na makosa kadhaa ya walinzi wetu,mchezo huu umechezwa leo kwenye uwanja Taifa Dar es salaam.


Wachezaji wa Taifa stars Amir Maftah,Mbwana Samata na Dan Mruanda wakishangilia mara baada ya kujipatia bao la kuongoza dhidi ya Algeria


No comments:

Post a Comment