BENJAMINKAMINYOGE.BLOGSPOT.COM

Monday, September 22, 2014

COASTAL UNION YAIGOMEA SIMBA

Timu ya Coastal Union ya Jijini Tanga imelazimisha sare ya goli 2-2 dhidi ya Simba kwenye uwanja wa Taifa Dar es salaam,ikiwa ni mchezo wa kwanza wa ligi kuu ya Tanzania bara.
  Simba ilikianza kipindi cha kwanza kwa kasi na kujipatia magoli mawili yaliyofungwa na Shaaban Kisiga na Amisi Tambwe,mabao yalidumu hadi mapumziko.
Coastal walirudi kipindi cha pili wakiwa na machungu na kufanikiwa kusawazisha magoli yote na hivyo kuwanyima Simba ushindi ambao tayari walikuwa na uhakika nao hadi kipenga cha mwisho timu hizo zimetoka 2-2.

Saturday, September 20, 2014

YANGA YAANZA LIGI YA VPL KWA KUCHAPWA 2-0 NA MTIBWA

Timu ya Yanga ya Dar es salaam leo imeanza ligi kuu ya Tanzania bara kwa kufungwa goli 2-0 na Mtibwa Sugar kwenye uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.
Wenyeji wa mchezo huo wakicheza kwa kujiamini na kufanya mashambulizi ya kushitukiza waliduwaza Yanga dakika ya 15 ya mchezo baada ya Mussa Hassan Mgosi kupachika bao la kwanza kwa kuwazidi ujanja walinzi wa Yanga.
Baada ya bao hilo Yanga walikuja juu na kulisakama lango la wapinzani wao na kupata goli ambalo mwamuzi wa mchezo huo alikataa na kutoa penati kwa Yanga ambayo iliota mbawa,penati hiyo ilipigwa na Mbrazil Jaja na kumgonga miguuni golikipa Said Mohamed muda mfupi baadaye Yanga waliweza tena kupata goli lakini mwamuzi aligoma kwa madai mfungaji alikuwa ameotea.
Timu hizo zilienda mapumziko huku Mtibwa ikiwa mbele kwa goli 1-0,kipindi cha pili Yanga waliingia na kutawala mchezo huo lakini bahati haikuwa yao kwani dakika ya 83 Ame Ally aliifungia Mtibwa goli la pili hadi mwisho wa mchezo Mtibwa 2 Yanga 0
Michezo mingine iliyochezwa leo na matokeo yake:-
.Azam 3-Polisi Moro 0
.Ndanda FC 4-Stand Utd 1
.Mgambo JKT 1-Kagera 0
.Ruvu shooting 0-Prisons 2
.Mbeya City 0-JKT Ruvu 0
Ligi hiyo itaendendelea kesho kwa mchezo mmoja kati ya Simba na Coast Union uwanja wa Taifa Dar es salaam.

UHARIBIFU WA MAZINGIRA KWA KUKATA MITI WAZIDI KUPAMBA MOTO RUKWA

Katika hali isiyokuwa ya kawaida wananchi wa kijiji cha Mtakuja njia iendayo Kapele Kasusu wilayani Sumbawanga wamekuwa wakikata misitu ili kupata maeneo ya kulima ulezi.
Wananchi hao wamekuwa wakifanya uharibifu mkubwa wa mazingira kutokana na kulima mazao ya muda mfupi ambayo faida yake ni ndogo ukilinganisha na misitu hiyo,wanachohitaji ni kupewa elimu juu ya utunzaji wa mazingira hususani ukataji miti ovyo,inabidi juhudi za haraka zichukuliwe ili kuinusuru hali hiyo ambayo inaweza kuli
fanya eneo hilo kukosa mvua kwa miaka ya baadaye.
Hizi ni baadhi ya picha ya msitu huo unaoshambuliwa kwa kasi.

Hii ni miti ambayo imeangushwa
Msitu ukiwa umekatwa na wananchi kwa ajili ya kilimo cha ulezi.

Saturday, September 06, 2014

WATU ZAIDI YA 30 WAFARIKI KWENYE AJALI MUSOMA LEO

 Zaidi ya watu 30 wamefariki kwenye ajali iliyohusisha magari matatu eneo la Sabasaba mjini Musoma leo,ajali hiyo imetokea leo mchana kwa kuhusisha mabasi mawili ya Mwanza Coach na J4 Express na gari ndogo aina ya Nissan Terrano baada ya J4 Express kuigonga ubavuni Nissan hiyo kuisukumia mtoni kabla ya kukutana uso kwa uso na Mwanza Coach nje kidogo ya daraja.
 Sababu kubwa ni mwendo kasi wa mabasi hayo ambayo yalikutana kwenye daraja ambalo ni jembamba na kusababisha maafa kwa abiria na wengine kujeruhiwa.
  Haraka za madereva wa mabasi zimekuwa ni vyanzo vya ajali nyingi ambazo zingeweza kuepukika lakini imekuwa ni kawaida kwa madereva kujifanya kama hawajui nini kinaweza kutokea kutokana na mwendokasi wao na hii imekuwa ikichangiwa hata na baadhi ya abiria wanaojifanya wana haraka za kuwahi biashara zao na kuwakejeli madereva wanaokwenda mwendo wa taratibu.
Hii ni sehemu ya mabaki ya basi baada ya ajali
Baadhi ya wananchi wakiangalia kwa hudhuni moja ya basi lililopata 

Saturday, August 30, 2014

YANGA YATANGAZA KAMATI YA NIDHAMU,MAADILI NA SHERIA.

  TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
 Mwanasheria Sam Mapande, Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya YANGA –(Utawala Bora) anapenda kutoa taarifa kupitia vyombo vya habari kwa wana YANGA,ameunda Kamati ndogo chini ya Kamati ya Utendaji wa YANGA zifuatazo:
1) KAMATI YA MAADILI Wajumbe:   1) Fimbo, Mgongo Prof. (Advocate) 2) Kabudi, Mpalamaganda Prof. (Advocate)  3) Njaa, Salehe Ramadhani (Advocate) 4) Rashidi, Tausi Abdallah (Advocate) 5) Tenga, Cathbert (Advocate)
 2) KAMATI YA NIDHAMU Wajumbe:
  1) Karua, Tedy  2) Lamlembe, Roger 3) Kihanga, Pascal  4) Mahenge, Burton Yesaya 5) Mudhihir, Mudhihir (Advocate) 3)
 KAMATI YA SHERIA NA KATIBA  Wajumbe:
   1) Fimbo, Mgongo Prof. (Advocate) 2) Gikas, Farija (Advocate) 3) Kabisa, Jessica (Advocate) 4) Kabudi, Mpalamaganda Prof. (Advocate)  5) Kambamwene, January (Advocate) 6) Lupogo, Herman (Advocate) 7) Madibi, Richard (Advocate) 8) Mahenge, Burton Yesaya 9) Mgongolwa, Alex (Advocate) 10) Mkucha, Elisha (Advocate) 11) Mudhihir, Mudhihir (Advocate) 12) Njaa, Salehe Ramadhani (Advocate) 13) Rashidi, Tausi Abdallah (Advocate) 14) Tenga, Cathbert (Advocate) 15) Tenga, Ringo Dr. (Advocate) 16) Vedasto, Audax (Advocate 4)
 KAMATI YA UCHAGUZI Wajumbe:
  1)  Kajole, Mustafa  2)  Lundenga, Hashim Ibrahim  3)  Makele, Bakili  4)  Mlelwa, Daniel    5) Ngongolwa, Alex (Advocate) Ifahamike kwamba, kutakuwa na nyongeza ya uteuzi wa Wajumbe wengine wa Kamati za YANGA zilizotajwa hapo juu. Mwanasheria Sam Mapande, Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya YANGA – (Utawala Bora) atakuwa Mwenyekiti wa Kamati zilizotajwa hapo juu. Kamati ya Utendaji ya YANGA, ina karibisha Wajumbe waliotajwa katika Kamati zilizotajwa hapo juu kwa dhamira njema kuwa watasaidia kujenga YANGA bora, na wanaomba ushirikiano kutoka kwa wanaYanga wote ili Wajumbe walioteuliwa waweze kutenda kazi zao vyema kwa manufaa ya YANGA. (YANGA DAIMA MBELE NYUMA MWIKO) (BENO NJOVU) KATIBU MKUU WA YANGA

Friday, August 29, 2014

AJALI KUBWA YATOKEA MBALIZI MBEYA

 Wimbi la ajali limezidi kulikumba jiji la Mbeya baada ya leo kutokea ajali eneo la Mbalizi na kugharimu maisha ya watu wasiopungua kumi na wengine zaidi ya sita wakijeruhiwa.
 Ajali hiyo imehusisha gari ya abiria(daladala) na lori dogo aina ya TATA, na kuleta simanzi kubwa kwa wakazi wa Mbalizi na maeneo ya jirani.
Wananchi wa Mbalizi wakiwa wamepigwa butwaa baada ya ajali iliyosababisha vifo vya watu.

Sunday, August 24, 2014

EL-MERREIKH MABINGWA AFRIKA MASHARIKI NA KATI 2014

  Timu ya El-merreikh ya Sudan imefanikiwa kutwaa ubingwa wa Afrika mashariki na kati kwa kuwafunga APR ya Rwanda kwa bao 1-0,bao pekee la El-merreikh limefungwa na Allan Wanga dakika ya 25 ya mchezo na kuwafanya APR kushindwa kufurukuta mbele ya mashabiki wao na kunyang'anywa tonge mdomoni na wasudan hao.
  Mechi ya kutafuta mshindi wa tatu ilichezwa mapema na Police Rwanda wamepata nafasi hiyo kwa kuitoa KCCA ya Uganda kwa penati 4-2.

Wachezaji wa El-merreikh wakishangilia ushindi dhidi ya APR.

Tuesday, August 19, 2014

BIOGESI KWA MAISHA BORA

 Biogesi ni nishati itokanayo na kinyesi cha wanyama ambacho huchachuka ndani ya mtambo wa biogesi na kuweza kutumika kwa kupikia na kuwasha taa.
  FAIDA ZA BIOGESI:- .Haina moshi wala harufu mbaya
. Hupunguza madhara yanayosababishwa na moshi wa kuni au mkaa kama vile macho kuwa mekundu na kukohoa.
 .Huokoa muda Hupunguza muda wa kutafuta kuni hivyo kufanya shughuli nyingine za maendeleo.
 Mtandao huu umekutana na mtaalamu wa kutengeneza mtambo wa biogesi maeneo ya Mbinga Kigonsela bw.Linus Komba na kuelezea jinsi mtambo huu ulivyo rafiki wa mazingira,na kuwataka wananchi wa Tanzania hususani wale wanaoishi vijijini kuwasiliana naye ili aweze kuwasaidia na kuwafanya waendelee kuyatunza mazingira kwa kutokata miti,mnaweza kuwasiliana naye kwa simu yake ya mkononi +255 762 045 808,unaweza kuwasiliana naye na yuko tayari kuwafikia sehemu yeyote kwa ajili ya ushauri na matengenezo YATUNZE MAZINGIRA ILI UWAACHIE VIZAZI VIJAVYO SEHEMU NZURI YA KUISHI
Huu ndio mtambo wa biogesi ukiendelea kujengwa
Bw.Benjamin James akipata maelekezo kutoka kwa mafundi
Bw.Linus Komba akitoa maelezo kuhusu mtambo wa biogesi
Mafundi wakiendelea na kazi ya kukamilisha mtambo huo.

Sunday, August 17, 2014

MANCHESTER UNITED YAANZA VIBAYA EPL,YAPIGWA NYUMBANI

Ligi kuu ya Uingereza imefunguliwa huku matokeo yakiiduwaza Manchester United baada ya kukubali kichapo cha bao 2-1 wakiwa nyumbani,matokeo ambayo hawajawahi kuyapata kwenye mechi za ufunguzi toka mwaka 1972.
Matokeo yalikuwa kama ifuatavyo:-
Man United 1-Swansea City 2 West Brom 2-Sunderland 2 Stoke City 0 -Aston Villa 1 Leicester City 2 Final Everton 2 QPR 0-Hull City 1 West Ham 0 -Tottenham 1 Arsenal 2-Crystal Palace 1 Sunday, August 17 Liverpool 3:30 PM Southampton Newcastle 6:00 PM Man City Monday, August 18 Burnley FC 10:00 PM Chelsea Saturday, August 23 Aston Villa 2:45 PM Newcastle Chelsea 5:00 PM Leicester City Swansea City 5:00 PM Burnley FC Crystal Palace 5:00 PM West Ham Southampton 5:00 PM West Brom Everton 7:30 PM Arsenal Sunday, August 24 Hull City 3:30 PM Stoke City Tottenham 3:30 PM QPR Sunderland 6:00 PM Man United Monday, August 25 Man City 10:00 PM Liverpool All times are in East Africa Time

Wednesday, August 13, 2014

REAL MADRID YATWAA EUROPEAN SUPER CUP

Ronaldo akishangilia moja ya gola lake


Mabingwa wa kihistoria wa UEFA CHAMPION LEAGUE,Real Madrid wamefanikiwa kuongeza kikombe kingine kwenye maktaba yao baada ya kuifunga Sevilla ya Spain bao 2-0 kwenye mchezo uliofanyika uwanja wa Cardiff,mabao ya Real Madrid yakifungwa na mchezaji hatari Christiano Ronaldo dakika ya 30 na 49.
  Sevilla walikuwa kama timu iliyokata tamaa kabla ya kuingia uwanjani kutokana na Real Madrid kuwa na washambuliaji wenye gharama kubwa na uwezo mkubwa uwanjani kama Gareth Bale,James,Kloose

Ronaldo na wenzake wakifurahia ushindi

Sunday, August 10, 2014

MAONESHO YA KILIMO KUFANYIKA MJINI NI KUMNYIMA MKULIMA ELIMU NA MAARIFA YA KILIMO.

 Wakulima wa mazao mbalimbali wamekuwa hawapatiwi elimu juu ya uzalishaji wa mazao yao,na hivyo kulazimika kufanya kilimo cha mazoea na kujikuta wakiendelea kupata mavuno kidogo.
Pia kufanyika maonesho ya kilimo maeneo ya mjini kila mara ni kumnyima mkulima maarifa zaidi ya kilimo.
Ikiwa maonesho haya yakiwa yanafanyika vijijini yanaweza kuwafanya wakulima kubadilishana ujuzi na kujifunza mambo mengi zaidi kutoka maeneo mbalimbali ya nchi yetu,kuliko kufanyika kila wakati mjini na kuyafanya kuwa ya kibiashara zaidi na kutembelewa na watu wasiokuwa walengwa na kuwaacha wakulima wakibaki vijijini kwa kunywa pombe na kucheza ngoma na kuona hiyo ndio furaha ya sikukuu ya wakulima.

Shamba la miti lililoko Vwawa Mbozi
Ndizi zikiwa zimeandaliwa kwa ajili ya kusafirishwa huko Ushirika Tukuyu

Moja ya shamba la mpunga wilayani Kyela
Kakao wilayani Kyela
Shamba la mahindi Ruanda Mbozi.
Shamba la miparachichi Itipingi Njombe.

KAGAME CUP 2014

Gor Mahia FC 1-2 KCC FC KCC FC opened their 2014 Kagame Cup campaign with victory after coming from a goal down to beat KPL champions Gor Mahia 2-1in the second of the day’s game played at Amahoro stadium. Uganda Cranes striker Daniel ‘Mzee’ Sserunkuma gave the Kenyan champions a deserved lead in the 27th minute before substitute Brian Majwega equalised for the Ugandan champions seven minutes after recess and later Umony netted the winner in the 88th minute. Gor Mahia started the brighter side and dominated proceedings launching numerous attacks on the KCC FC goal but goalie Yasin Mugabi was up to the task whenever called upon. Bobby Williamson’s charges however got a deserved lead after Musa Muhammad beat Namwanja Simon down the left to cross for Sserunkuma who tapped home despite a forest of legs inside the 18 yard area. The goal saw KCC FC coach George ‘Best’ Nsimbe react by substituting in the inefficient Steven Bengo for Brian Majwega but the Kenyan champions held on to their first half lead in a dominant display. After recess, Nsimbe made another change bringing on Brian Umony for Herman Wasswa. The Ugandan side started to dominate the game at this time and deservedly equalised through Majwega tapping home a fine cross from Tom Masiko. The Ugandan side was in ascendency at the moment but couldn’t break a resilient Gor backline manned by David Owino. At the other end, Gor Mahia threatened with Sserunkuma and later Timothy Otieno forcing a double save from Yasin Mugabi. With two minutes left on the clock, Brian Majwega broke down the left on a counter move and his low cross met Umony who slid the ball at the far corner past Onyango for KCC FC’s winner. KCC FC now top group B with maximum points and return to action on Sunday against Atletico at Nyamirambo. Last modified onFriday, 08 August 2014 18:34 200

Friday, August 08, 2014

YANGA KUTOSHIRIKI KAGAME CUP KUTAPOTEZA WAPENZI WAPYA WA NDANI NA NJE YA TANZANIA

 Yanga ni moja ya timu kubwa ukanda huu wa Afrika mashariki na kati na pengine ndio inaweza ikawa timu yenye washabiki wengi kwa ukanda huu wa Afrika mashariki.
 Kitendo cha timu hii kuwa matatizo ya maramara na shirikisho la soka la Afrika mashariki na kati(CECAFA) na kuifanya timu hii kuondolewa kushiriki michuano ya kombe la Kagame,kuna uwezekano mkubwa wa timu kupoteza wapenzi wapya kwa sababu hamna mtu anayependa kujiingiza kwenye kitu ambacho kina matatizo kila mara,na athari zake haziwezi kuonekana leo hii inaweza ikaonekana miaka ishirini ijayo au zaidi,kwa sababu wapenzi wapya ni wale ambao wana umri wa miaka mitano hadi kumi.
Wakisherekea ubingwa
Kikosi cha Yanga

Tuesday, January 14, 2014

CHRISTIAN RONALDO MCHEZAJI BORA 2014


Christian Ronaldo leo amechaguliwa kuwa mchezaji bora wa dunia kwa mwaka 2014/15 kwa kuwashinda wachezaji Leon Messi wa Argentina na klabu ya Barcelona na Frank Ribery wa Ufaransa na klabu ya Bayern Munich.
Tuzo hiyo ilikuwa ikishikiliwa na Leon Mess kwa miaka minne mfululizo.

KCC FC MABINGWA MAPINDUZI CUP 2014


Timu ya KCC ya Uganda leo imechukua ubingwa wa kombe la mapinduzi Zanzibar baada ya kuifunga timu ya Simba ya Dar es salaam kwa goli 1-0,kwenye mchezo wa fainali uliochezwa kwenye uwanja wa Amaan,mjini Zanzibar,goli pekee la KCC limefungwa na Herman Waswa dakika ya 20.
 Kwa matokeo hayo timu ya KCC inakuwa timu ya kwanza kutoka nje ya nchi kuchukua ubingwa huo,mashindano yalikosa msisimko baada ya timu ya Yanga kujitoa dakika za mwisho na hivyo kuwakatisha tamaa wapenzi wa soka wa Zanzibar.
KCC waliingia fainali baada ya kuwachapa Azam 3-2 na Simba waliingia fainali kwa kuwachapa URA ya Uganda 2-0.