BENJAMINKAMINYOGE.BLOGSPOT.COM

Saturday, April 09, 2011

YANGA YAKARIBIA UBINGWA


Timu ya Yanga imeamusha matumaini ya kutwaa ubingwa msimu huu baada ya kuwachapa African Lyon kwa jumla ya bao 3-0 na kufikisha pointi 46 na kubakiwa na mechi moja sawa na mahasimu wao Simba ambayo nayo imebakiza mchezo mmoja dhidi ya Majimaji.

Wednesday, April 06, 2011

SIMBA ALMANUSRA KWA RUVU JKT


Mabingwa watetezi wa Tanzania bara Simba leo wamenusurika kichapo kutoka kwa maafande wa JKT RUVU baada ya kusawazisha bao kwa njia ya penati iliyofungwa na Emanuel Okwi,ilikuwa ni JKT RUVU iliyokuwa ya kwanza kujipatia bao la kuongoza kipindi cha kwanza lililowekwa kimiani na Hussein Bunu na kudumu hadi mapumziko,Simba ambao leo walionekana kubanwa vilivyo na wapinzani wao,mwamuzi wa mchezo huo alishindwa kuumudu mchezo huo na kuwatoa nje wachezaji wa JKT akiwemo Shabaan Dihile na George Minja,ligi hiyo itaendelea tena kesho kati ya Yanga dhidi ya African Lyon,Yanga wanahitaji ushindi ili kujiwekea mazingira mazuri ya kunyakua ubingwa.

VODACOM WABADILISHA RANGI YAO.


Linaloonekana ni jengo la Vodashop Mbeya,likiwa linaendelea kupigwa rangi tofauti na ile iliyozoeleka na wengi ya bluu sijui na jina litakuwaje?umekuwepo mchezo wa kubadili majina na rangi kwa baadhi ya makampuni ya simu kama vile mobitel wakaitwa Buzy na sasa tigo na Celtel wakaitwa Zain na sasa Airtel.

Friday, March 11, 2011

EARTH QUACKE JAPAN

Japan yatikiswa na tetemeko na kimbunga na kuharibu mali kadhaa ikiwemo majengo na miundo mbinu mbali mbali.

YUKO WAPI HUYU ?

KUNA UWEZEKANO UNAMFAHAMU MTU HUYU,MI SIMFAHAMU KABISA.

DAVIES MWAPE

Davies Mwape ni moja kati ya wachezaji hatari katika ligi kuu ya msimu huu,ni mshambuliaji mwenye uwezo mkubwa wa kufumania nyavu za adui na mbinu kuwatoka walinzi wa timu pinzani,viongozi wa Yanga mtunzeni mchezaji huyu msije mkamfanyia AMBANI

Thursday, March 10, 2011

LOLIONDO STOP

Mch.Ambilikile Mwasapile akiwawekea dawa baadhi ya watu waliofika kwa ajili ya kupatiwa huduma hiyo,lakini hata hivyo serikali imesimamisha huduma hiyo kwa ajili ya kufanya uchunguzi na usalama wa dawa hiyo

SIMBA YAZIKALIA AZAM NA YANGA

Timu ya Simba ambao ni mabingwa watetezi wa ligi kuu ya Tanzania bara jana walifanikiwa kuongoza ligi kwa kuifunga Ruvu shooting ya Pwani kwa bao 1-0 dakika ya 87 likifungwa na mchezaji Ally Ahmed 'Shiboli' aliyeingia dakika ya 79 kuchukua nafasi ya Mbwana Samata aliyebanwa vilivyo na mabeki wa Ruvu,sasa Simba imefikisha pointi 41 baada kucheza michezo 18,ikifuatiwa na Yanga yenye pointi 39 huku Azam ikiwa na pointi 37 

Tuesday, March 08, 2011

Mchungaji AMBILIKILE MWASAPILE (kulia) akihojiwa na waandishi wa habari waliofika nyumbani kwake,mchungaji huyo amekuwa akitoa dawa kikombe kimoja kwa kila mgonjwa

WATU WAFURIKA KWA MCHUNGAJI

Umati wa watu unaendelea kufurika kwa mchungaji mstaafu mzee Ambilikile Mwasapile wilayani Ngorongoro,watu wamekuwa wakitoka sehemu mbambali kwa ajili ya kufuata tiba ya magonjwa mbalimbali ambayo yamekuwa hayatibiki hospitalini

Monday, March 07, 2011

LIVERPOOL YAWACHINJA MANCHESTER UTD.

LIVERPOOL jana imeweza kuwashikisha adabu Manchester United baada ya kuwafunga mabao 3-1,magoli ya liverpool yaliwekwa kimiani na Dirk Kuyt.

SIMBA NA YANGA NGUVU SAWA

Timu  zenye upinzani wa jadi kwenye soka la bongo Simba na Yanga jana zilitoka sare ya kufungana bao 1-1

Friday, March 04, 2011

CRDB WAFUNGUA TAWI JIPYA MWANJELWA- MBEYA

Waziri wa maji,Profesa Mark Mwandosya (watatu kushoto) akikata utepe kufungua tawi jipya la benki ya CRDB eneo la Mwanjelwa jijini MBEYA,kushoto ni mwenyekiti wa bodi ya benki hiyo bw.Martin Mmari,kulia ni mama Mwandosya,kufunguliwa kwa tawi hilo kutawasaidia wakazi wa jiji la Mbeya ambao walikuwa wakipanga foleni kwenye tawi pekee lililokuwa mjini Mbeya.

Wednesday, March 02, 2011

SOKO LA BIG BROTHER UBUNGO LAVUNJWA

Soko la big brother eneo la ubungo limevunjwa jana usiku ili ujenzi wa stend wa mabasi yaendayo kasi,hapa ni baadhi ya wafanyabiashara wakiangalia mabaki ya vibanda vyao.

GADAFFI ANG'ANG'ANIA MADARAKANI

  • Kiongozi wa Libya Muamar Gadaffi ameendelea kung'ang'ania madaraka,licha ya kuwepo kwa maandamano ya kumtaka kuachia madaraka hayo ya urais ambayo ameshikilia kwa zaidi ya miaka arobaini,amekuwa ahamini kinachotokea kwenye taifa lake kutokana na jinsi utawala wake kutowapa uhuru waandishi wa habari na redio.


WAZIRI MKUU AKIWA NA MABALOZI WA UFARANSA NA UINGEREZA

Waziri mkuu Mh.Mizengo Pinda ( kushoto) akiwa na balozi wa Ufaransa bwana Jacques Champagne De Labriolle na balozi wa Uingereza bibi Dianne Corner wakati wa mkutano wa wataalam wa uchumi leo jijini Dar es salaam.

Tuesday, March 01, 2011

Saturday, February 26, 2011


Wakazi wa Gongo la mboto wakishangaa bomu lililokita chini siku chache baada ya milipuko eneo hilo.

Thursday, February 17, 2011

MABOMU GONGO LA MBOTO


Madaktari wa hospitali ya Amana jijini Dar es salaam,wakimuhudumia mmoja wa waathirika wa mabomu hayo ambayo yalilipuka kutoka kwenye ghala la kutunzia silaha la JWTZ.

BREAKING NEWS!!!


Kuna mlipuko mkubwa unaendelea usiku huu eneo la Gongo la mboto jijini Dar es salaam,inasadikiwa ni kutoka kambi ya jeshi la wananchi Tanzania (JWTZ) na hivyo kuwafanya wakazi na majirani wa eneo hilo kuyakimbia makazi yao na kuelekea katikati ya jiji na kusababisha msongamano mkubwa kwenye baadhi ya barabara.
Tutaendelea kuwapa taarifa zaidi kutoka mfuatiliaji wa taarifa hii.

Monday, February 14, 2011

SIMBA YAFUTA AIBU


Mabingwa wa soka Tanzania bara wamefanikiwa kusonga mbele kwenye michuano ya klabu bingwa Afrika baada ya kuifunga Elan club de mitsoudje ya Comoro kwa jumla ya magoli 4-2,Elan ndio iliyokuwa ya kwanza kupata bao dakika ya 42 likifungwa na Madaha Mohamed,Simba walisawazisha dak 44 kupitia kwa Mbwana Samata,magoli mengine ya Simba yalifungwa na Patrick Ochan dk 47,Samata dk.56,Amri Kiemba dk.72 na goli la pili la Elan lilifungwa na Abdoulhouda Abdouleafor dk.63,nao mahasimu wao Yanga wameendelea kukumbwa na jinamizi la mechi za kimataifa baada ya kukubali kipigo cha 2-0 kutoka kwa Dedebit mchezo huo ulichezwa jana jijini Adis Ababa-Ethiopia,kwa matokeo hayo Simba itakutana na mabingwa watetezi TP Mazembe ya DRC.

Sunday, February 13, 2011

BOMOA BOMOA


Jengo jipya lililoko Mbeya eneo la Mafiat,likionekana limebomolewa upande kutokana na mmiliki wake kushindwa kuzingatia umbali kati ya barabara na nyumba.

Tuesday, February 08, 2011

Saturday, February 05, 2011

AZAM FC YAZIDI KUTISHA


Timu ya Azam imezidi kujiwekea mazingira mazuri ya kuwania ubingwa wa Tanzania bara baada kuwafunga Toto African mabao 3-0,mabao yao yalipachikwa dakika ya kwanza na 35 na John Boko(Adebayor) na bao la tatu lilifungwa dk ya 56 na Mrisho Ngasa baada ya kupata pasi kutoka kwa Ramadhan Chombo Ridondo,Toto African walipoteana baada ya kufungwa bao la mapema na hivyo kuwafanya Azam kumiliki mchezo huo na kufikisha 29 nyuma ya Yanga yenye pointi 31
na Simba yenye pointi 30 na hivyo kuongeza ushindani wa kuwania ubingwa,ligi hiyo itaendelea tena leo ambapo Yanga watakuwa wageni wa wanalizombe Majimaji huko Songea na AFC Arusha watawakaribisha JKT Ruvu pale Sheikh Amri Abeid mjini Arusha na kesho mabingwa watetezi Simba watashuka uwanja wa Jamhuri Dodoma kukabiliana na Polisi Dodoma.

Wednesday, February 02, 2011

YANGA YAPOKEA KICHAPO CHA KWANZA.


Timu ya Yanga leo imepoteza mchezo dhidi ya Mtibwa Sugar ikiwa ni mchezo wake wa kwanza kupoteza toka ligi kuu ya msimu kuanza,kutokana na Yanga kucheza chini ya kiwango ilimulazimu kocha wake Fred Felix Minziro Kataraia(baba Isaya au Majeshi) kusimama muda wote na kuliona benchi chungu baada ya Mtibwa kutawala mchezo huo,mara baada ya mchezo huo kumalizika mashabiki wanaosadikiwa kuwa ni wa Yanga waliwafanyia vurugu wachezaji wa Yanga kwa kutoridishwa na mwenendo wa timu hiyo na kutokuwepo kwa wachezaji kama Shadrack Nsajigwa,Yaw Berko,Athman Idd kunaonekana kuwaathiri Yanga kwenye mechi ya leo bila kumsahau kocha Costadin Papic ambaye ametimkia Africa Kusini kutokana na kutokuelewana na baadhi ya viongozi wa timu hiyo ambayo pia inakabiliwa na mechi ya kombe la shirikisho Africa dhidi Dedebit ya Ethiopia kwenye mchezo wa marudiano.

Monday, January 31, 2011

SIMBA KAMA PAKA


Mabingwa wa soka wa Tanzania bara wameshindwa kudhiirisha umwamba wao kwenye mechi za kimataifa baada ya kulazimishwa suluhu na wenyeji wao ELAN CLUB DE MITSOUDJE ya Comoro na hivyo kuwafanya wapinzani wao kuhitaji sare ya magoli ili waweze kusonga mbele kwenye mchezo wa marudiano utakaofanyika wiki mbili zijazo jijini Dar,nao mahasimu wao Yanga walishindwa kuutumia vyema uwanja wa taifa baada ya kulazimishwa sare ya mabao 4-4 na Dedebit ya Ethiopia na hivyo kujiweka katika mazingira magumu.

Friday, January 28, 2011

LILONDO


Wakina mama wa eneo la Lilondo wakifanya biashara ya ndizi kwenye mabasi yanayopita eneo hilo,mabasi yanayofanya safari kati ya Songea,Iringa,Mbeya na Dar es salaam.

KITUO CHA MABASI SONGEA.


Wafanyabiashara wa eneo la stendi kuu Songea,wakifanya biashara za vyakula katika eneo lisiloridhisha kwa afya za walaji na usalama kutokana na majiko kuwa jirani na mabasi.

PERAMIHO MISSION


Kanisa kongwe la Roman Catholic la Peramiho.

PERAMIHO HOSPITAL



PERAMIHO SONGEA


Hospital ya Peramiho ni moja ya hospital kubwa zinazotoa huduma bora za kiafya hususan kwa wakazi wa kanda za nyanda za juu kusini na maeneo mengine.

Sunday, January 23, 2011

IHANDA MBOZI


Mabaki ya gari aina ya Coaster,ambayo ilichomwa moto na wananchi wenye hasira baada ya kumgonga mkazi wa kijiji cha Ihanda na kusababisha kifo chake.

Thursday, January 20, 2011



MAMBO YA BAJAJ


Usafiri wa Bajaj umekuwa wa kawaida wa kawaida kwa baadhi ya sehemu hapa nchini,leo imetokea ajali ya Bajaj jijini Mbeya eneo la Meta baada ya Bajaj kuacha njia na kuingia kwenye mtaro kutokana na mwendo wa kasi na hivyo kusababisha dereva kushindwa kuimudu kwenye kona,wanaonekana wananchi wenye huruma wakiitoa bajaj hiyo,dereva na abiria wake walinusurika kwenye ajali hiyo.

AJALI


Daladala inayofanya safari kati ya Mbalizi na Mwanjelwa ikiwa imeigonga gari ndogo eneo la Kadege,kwa bahati nzuri hakuna majeruhi kwenye ajali hii iliyotokea jioni hii.

Wednesday, January 19, 2011

HOLIDAY HILL HOTEL-MBEYA


Moja ya hotel za kisasa jijini Mbeya,Holiday hill hotel iko jirani na kanisa la Efatha,ina huduma za internet,chumba cha mikutana,maegesho ya magari na mambo mengi.

Friday, January 14, 2011

TUCHANGIE DAMU KUWASAIDIA WAGONJWA.


Dr.MATHEO KINEMO wa mpango wa taifa wa damu salama akitoa elimu juu ya kuchangia damu kwa wanafunzi wa shule ya sekondari ya Meta iliyoko jijini Mbeya,mdau wa globu hii anawapongeza na kuwashukuru wananchi wote wenye moyo wa huruma na kuchangia damu kwa ajili ya wagonjwa wenye upungufu wa damu wakiwemo wajawazito,watoto chini ya miaka mitano na waanga wa ajali mbali mbali kama vile ajali za barabarani,moto na kadhalika.

Monday, January 10, 2011


Gari ya zimamoto likiwa eneo la tukio.

WELL DONE ZIMAMOTO


Kikosi cha zimamoto mkoani Mbeya kimefanikiwa kuinusuru hotel ya Calm inn,iliyokuwa imeshika moto,wanaonekana askari wa zimamoto wakiudhibiti moto huo.

Sunday, January 09, 2011

RC PAROKIA YA RUANDA-ILOMBA MBEYA.


Waumini wakijianda kuingia kanisani kwa ajili ya kumuomba na kumshukuru Mwenyezi MUNGU kwa mema mengi aliyotutendea.

ENZI ZA MWALIMU


Gari aina ya LEYLAND ALBION ambazo miaka ya 70 ndio zilikuwa kwenye chati kama ilivyo SCANIA leo,likiwa na mashine za kuchimbia visima vya maji.

Saturday, January 08, 2011

HAUZAN EDWARD


Mfanyakazi wa mamlaka ya maji safi na taka mkoa wa Mbeya akijitolea damu kwa ajili ya kuwasaidia wagonjwa.

MAZINGIRA


Mfanyakazi anayeshulika na utunzaji wa mazingira kwenye ya sekondari ya Pandahill,akifyeka nyasi kwa kutumia mashine aina ya SHIKUNDAIWA

NELLAS KITUNDU


Mfanyakazi wa mamlaka ya maji Mbeya,akipumzika baada kushiriki zoezi la kuchangia damu.

Friday, January 07, 2011

Tuesday, January 04, 2011

SOKO MATOLA-MBEYA


Wauzaji wa matunda, mboga za majani na viungo wakiwa wamepanga bidhaa zao mbele ya maduka na kuzipanga chini,tunawaomba viongozi wa soko na halmashauri ya jiji kuwawekea mazingira mazuri wajasiliamali hawa kwa kuwaweka eneo zuri kwa afya za walaji na wao pia.

Monday, January 03, 2011

IGURUSI MBEYA


Wakazi wa kijiji cha Igurusi,mkoani Mbeya wakiwa kwenye pilikapilika za kila siku kwa ajili ya kujipatia riziki,kijiji hiki ni maarufu kwa biashara ya mchele.

Saturday, January 01, 2011

HAPPY NEW YEAR 2011


Nights are dark but days are light,wish your life will always be bright.So my dear dont get fear coz,God gift us a "brand new year"
*HAPPY NEW YEAR*