BENJAMINKAMINYOGE.BLOGSPOT.COM

Saturday, April 07, 2012

SIMBA HAO 16 BORA KOMBE LA SHIRIKISHO


Timu ya Simba ya Dar es salaam jana ilifanikiwa kusonga mbele kwenye michuano ya kombe la shirikisho licha ya kufungwa bao 3-1 na Es Satif kwenye uwanja wa May 8 mjini Satif-Algeria.
Simba wakicheza pungufu baada ya mlinzi wake kucheza faulo ya kizembe na kutolewa kwa kadi nyekundu dk.8,walibanwa sana wapinzani wao na kujipatia magoli hayo matatu.
Simba walitulia dak 7 za mwisho na kuweza kupata goli dk.92 likiwekwa kimiani na Emanuel Okwi na kuwafanya Simba kusonga mbele kwa faida ya goli la ugenini,wiki mbili zilizopita Simba walishinda 2-0 jijini Dar es salaam.

No comments:

Post a Comment