BENJAMINKAMINYOGE.BLOGSPOT.COM

Tuesday, April 24, 2012

UPONDAJI WA KOKOTO WAZIDI KUONGEZEKA MBEYA.


Kutokana na ugumu wa maisha,vijana wengi wamekuwa wakijishughulisha na kazi mbalimbali jijini Mbeya,ikiwemo kuponda kokoto pembezoni mwa barabara kuu,kamera yetu ilipita maeneo ya Ilomba jijini Mbeya na kukuta wajasiliamali wakiponda kokoto na kuuza kwa kipimo cha debe kwa sh.1500/= bila kujali jua kali lililokuwa likiwaka na kuwa kandokando ya barabara jirani na kituo cha mafuta.
Tunawaomba viongozi na taasisi mbalimbali kuweza kuwasaidia wajasiliamali hawa kuwaboreshea mazingira yao ya kazi kwa kutoa mikopo au kuwapatia vifaa vya kujikinga wanapofanya kazi zao.

No comments:

Post a Comment