BENJAMINKAMINYOGE.BLOGSPOT.COM

Sunday, November 13, 2011

MAREKANI YAOMBA MSAMAHA KWA INDIA


Marekani imeiomba msamaha serikali ya India kutokana na kitendo cha maafisa wake wa uwanja wa ndege wa New York kumpekua rais wa zamani wa India,bwana Abdul Kalam mwezi Septemba.
Serikali ilitoa malalamiko yake kwa Marekani kufuatia kitendo hicho kilichoonekana kama udhalilishaji kwa mheshimiwa huyo,pia mcheza sinema maarufu wa India Shah Rukh Khan aliwahi kulalamikia kitendo kama hicho alichofanyiwa mwaka 2009.

No comments:

Post a Comment