BENJAMINKAMINYOGE.BLOGSPOT.COM

Saturday, December 03, 2011

KILI STARS HOI KWA ZIMBABWE

Timu ya soka ya Tanzania bara leo imefungwa magoli 2-1 na wenzao wa Zimbabwe kwenye michuano ya kombe la CECAFA inayoshirikisha mataifa ya Afrika mashariki na kati huku timu za Malawi na Zimbabwe zikiwa zimealikwa kwenye michuano hii.
  Zimbabwe walijipatia mabao yao kipindi cha kwanza kutokana na mabeki wa Kili stars kucheza kwa kutoelewana,hatimaye Kili Stars ilipata bao la kufutia machozi kwa njia ya penati iliyopigwa na Mwinyi Kazimoto baada ya Mrisho Ngasa kufanyiwa madhambi eneo la hatari zikiwa zimesalia dakika 4 mpira kumalizika.

No comments:

Post a Comment